Hawachi
JF-Expert Member
- Nov 25, 2018
- 12,010
- 54,194
Huyu ndugu yangu alikuwa muanifu nimewahi kuweka pesa kwake mara tatu ila safari hii kanifundishaPoleni sana aiseee.
Mimi dada yangu kabla ya kuoa nilikuwa nampa pesa yangu ya upatu aniwekee maana nikikaa nazo mara ntanunua vitu nisivyokuwa na bajeti navyo.
Nakumbuka akaniwekea pesa zangu zaidi ya milioni tigopesa baada ya mda nikazihitaji nikaenda kutafutia ardhi na kutolea mahari.
Alinitunzia ile pesa na yeye sio tajiri siku ingine ya kula inampiga chenga,ila hakunidhulumu hata mia moja.
Ndio maana nasema haya mambo hayana formula pengine ndugu yako akakuliza na mwingine akakusaidia.
Muhimu mtu aangalie hali ya ndugu,kama anatunza amana basi sio mbaya na kama hatunzi usimpe
Hata mke na mume mtu aangalie kama anatunza ampe kama hatunzi amana asimpe