Kijukuu cha ngoyayi
JF-Expert Member
- Oct 27, 2018
- 1,384
- 2,880
Shukurani sana. Nimeongea sana na wife. Uzuri ana kazi yake japo hailipi sana. Hofu yake ni kwamba vipi tusipofanikiwa. Anaona ni bora nifanye kazi hadi umri wa kustaafu nitapata angalau 150m. Nmwambia sintakuwa na nguvu za kufanya biashara wakati huo, na nisipofanya kitu cha kuzalisha hazitatutosha.
Ila uzuri ni kwamba tayari tuna kibanda chetu, kwa hiyo hatukai nyumba ya kupanga.
Very good starting point, shukurani Mkuu. Kwa hiyo unasema nikubali kuacha kazi?
Hicho kihunzi kimoja. Cha pili, niingie kwenye shughuli gani? Kuna mtu kaniambia Tshs 200m ni hela ndogo sana!
Mie mawazo yangu hao ilikuwa niingie kwenye Coaster, nianze na mbili.
Mkuu, huyu sio rafiki, ni ndugu yangu ambae si mara ya kwanza anani-support. Kwake USD100,000 sio jambo kubwa.Huyo una ugomvi anataka kukuangamiza huku unacheka nae. Sasa ukiacha kazi asipokupa utapata wapi kazi?? Usikubali kutapeliwa kijana
Hujawahi fanya biashara ndio maana. Hapo una hofu kibao ya kushindwa. Sikuambii ni ipi. Nakushauri tafuta mtu aliyefanikiwa katika biashara na unaemumini awe mentor wako. Hela zipo katika biashara ndugu. Na hiyo biashara ni ile ambayo mwenyewe unashiriki sio ambao hujui chochote.
Mara nyingi nimetetea uraia pacha ili wana Diaspora wapewe nafasi za kuwekeza nchini. Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kwamba nina ndugu yangu huko nje alichukua uraia wa huko, na sasa anasema inakuwa vigumu kuwekeza Tanzania kwa kuwa yeye sio raia tena wa Tanzania.
Sasa juzi hapa kanishauri niachane na kazi za kuajiriwa (mshahara wangu ni kama Tshs 1.5m kwa kwenzi). Ananiambia yuko tayari kunipa mtaji wa Tshs 200m kwa shart moja tu, niachane na kazi ya kuajiriwa ili nijikite kwenye kuzitumia hizo Tshs 200m zizalishe. Kaniambia hatanipangia cha kufanya, ni juu yangu, na kwamba kama nikizipoteza pia ni juu yangu, wala hatanidai. Ila hataki anipe hizo hela huku naendelea na kazi ya kuajiriwa.
Naombeni ushauri - kwanza kama ni wazo zuri mie kuacha kazi kwa hiyo Tshs 200m, na kama ndivyo nikiacha kazi nizitumie kwenye biashara gani? Nikiacha kazi, nina mafao yangu ya kama Tshs 70m, kwa hiyo nitakuwa na jumla ya kama Tshs 270m, lakini bado sielewi nifanye shughuli gani. Kilimo? Daladala? Nyumba? Biashara ya mazao? Niziweke tu benki niwe nachukua interest? Au niendelee tu na kazi yangu ya kuajiriwa yenye uhakika wa mshahara kila mwe
Mkuu, mke wangu anaelewa wazi kwamba pale asipokubaliana jambo na mimi haina maana lazima nifuate anachotaka yeye. Kuna wakati nafanya ninachotaka mimi tofauti na anachotaka yeye. Ndio kuna wakati nitafanya anachotaka yeye tofauti na ninachotaka, lakini sio siku zote. Kwa mfano, ingekuwa issue ni yeye kuacha kazi akapinga, nisingemlazimisha, lakini issue ni mimi kuacha kazi, hivyo sio lazima nifuate anachotaka. At the end of it all, mimi ndio captain wa familia.Kumbe mkeo ameshakushauri boss..!? Sasa unataka sisi huku tukuvunjie ndoa aiseeh!
Kwaani ukimdanganya umeshaacha kazi ili aweke kabisa huo mzigo inawezekana?? Maana ukipata hiyo pesa humu ndani kuna wafanyabiashara wengi na wanayo mawazo mazuri ila wanakosa kuchangia maana wanaona unazingua.Mkuu, huyu sio rafiki, ni ndugu yangu ambae si mara ya kwanza anani-support. Kwake USD100,000 sio jambo kubwa.
Basi jitafakari
Unapenda au hupendi hio kazi?
Inakutesa ama haikutesi
Ina future nzuri au la?
Nitamdanganya ndugu yangu ambae kila siku tuko pamoja kama jamaa moja? Na atakapojua nimemdanganya itakuwaje? Nadhani gharama ya uhusiano kati yangu na ndugu yangu ina thamani sana kuliko Tshs 200m. Nina principles MkuuKwaani ukimdanganya umeshaacha kazi ili aweke kabisa huo mzigo inawezekana?? Maana ukipata hiyo pesa humu ndani kuna wafanyabiashara wengi na wanayo mawazo mazuri ila wanakosa kuchangia maana wanaona unazingua.
jini makata1. Acha kazi
2. Chukua mil 200
3. Nitafute nikupeleke kwa pisi Kali na viwanja high class.
4. Hela ikikata, tafuta kazi tena
mkuu mbona unakosa uaminifu hata kwenye ideas?.uaminifu na ukweli ni kitu muhimu na cha kwanza kwenye kila kitu iwe biashara au ajira....wizi, utapeli, uongo-uongo hautakufikisha mbali..ni jambo la muda mfupi tu lenye hasara kubwa mbeleni.Hapa ndo Tanzania bro
Mtengenezee fake papers..
Akija unachuka likizo unakaa kwny ile biashara ndogo uloanzisha
Mfano mini supermarket...
Wenye uzoefu watasema
Usiache kazi. Natumaini unajua Hali ya biashara ilivyo tete na isiyoeleweka. Tshs 200M utasema ni nyingi, Ila laana iliyopi ndani ya nchi yetu, zitapukutika na usifanye lolote, hivyo kuwa muangalifu sana, na kama ni kuwekeza, fanya kidogo kidogo. Maeneo gani ya kuwekeza, Hilo ni la kufanya utafiti wa kina, maana sijaona biashara yoyote yenye uhakika Tz.Mara nyingi nimetetea uraia pacha ili wana Diaspora wapewe nafasi za kuwekeza nchini. Sababu kubwa ya kufanya hivyo ni kwamba nina ndugu yangu huko nje alichukua uraia wa huko, na sasa anasema inakuwa vigumu kuwekeza Tanzania kwa kuwa yeye sio raia tena wa Tanzania.
Sasa juzi hapa kanishauri niachane na kazi za kuajiriwa (mshahara wangu ni kama Tshs 1.5m kwa kwenzi). Ananiambia yuko tayari kunipa mtaji wa Tshs 200m kwa shart moja tu, niachane na kazi ya kuajiriwa ili nijikite kwenye kuzitumia hizo Tshs 200m zizalishe. Kaniambia hatanipangia cha kufanya, ni juu yangu, na kwamba kama nikizipoteza pia ni juu yangu, wala hatanidai. Ila hataki anipe hizo hela huku naendelea na kazi ya kuajiriwa.
Naombeni ushauri - kwanza kama ni wazo zuri mie kuacha kazi kwa hiyo Tshs 200m, na kama ndivyo nikiacha kazi nizitumie kwenye biashara gani? Nikiacha kazi, nina mafao yangu ya kama Tshs 70m, kwa hiyo nitakuwa na jumla ya kama Tshs 270m, lakini bado sielewi nifanye shughuli gani. Kilimo? Daladala? Nyumba? Biashara ya mazao? Niziweke tu benki niwe nachukua interest? Au niendelee tu na kazi yangu ya kuajiriwa yenye uhakika wa mshahara kila mwezi?
Mpambanaji hawezi kuja kuuliza jf kwamba afanye biashara gani200milioni mtaani kama kweli wewe ni mpambanaji unatoboa faster wala usiogope..