Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Afariki kwa kupondwa jiwe kichwani akichimba madini.
Mkazi wa Kijiji cha Masungura wilayani Meatu, Simiyu Michael Salum (30), amefariki dunia kwa kupondwa na jiwe kichwani wakati akichimba dhahabu ndani ya duara katika machimbo ya Mwakitolyo, wilayani Shinyanga.
Ofisa Madini Mkoa wa Shinyanga, Joseph Kumburu, akizungumza hivi karibuni na wachimbaji wadogo wa Mwakitolyo, alisema kuwa tukio hilo limetokea Julai 17, mwaka huu na kuwa ajali hiyo ilitokea katika kitalu cha wachimbaji wadogo wa namba 5.
Kumburu alisema ajali hiyo imetokea majira ya saa 6:00 mchana wakati wachimbaji zaidi ya watano walipokuwa wakitoka ndani ya duara baada ya kumaliza kazi.
Kumburu alisema, kwa mujibu wa Mtaalam wa afya aliyekuwa kwenye uchunguzi huo, mtu huyo alipasuka kichwani na kusababisha umauti kutokana na kuanguka kutoka umbali wa mita 20, baada ya kuteleza na jiwe kumponda kichwani na kusababisha kifo chake.
“Marehemu hakuwa na majeraha yoyote zaidi ya kupasuka kichwa, niwashauri tu ndugu zangu wachimbaji muhakikishe mnazingatia taratibu na sheria za uchimbaji mnazoelekezwa na wataalamu wenu ili kufanya shughuli hizo kwa hali ya usalama zaidi kwa kuwa chanzo cha tukio marehemu alikosa nguvu,” alisisitiza Kumburu.
Kutokana na ajali za mara kwa mara zinazotokea kwenye machimbo hayo, Ofisa Madini huyo alifunga eneo kulipotokea ajali kwa siku tatu kupisha ukaguzi.
Kumburu aliandaa timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Madini, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Salawe pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Shinyanga ili kusimamia ukaguzi huku akishauri hatua za haraka za kuchukuliwa kwa maduara yote yatakayobainika kuhatarisha maisha ya watu.
Ofisa Madini Kumburu aliwataka wachimbaji hao kuzingatia Sheria za madini na maelekezo wanayopewa na wakaguzi kufukia mashimo yote ambayo yameachwa wazi ili kuepusha ajali.
Chanzo: Nipashe
Mkazi wa Kijiji cha Masungura wilayani Meatu, Simiyu Michael Salum (30), amefariki dunia kwa kupondwa na jiwe kichwani wakati akichimba dhahabu ndani ya duara katika machimbo ya Mwakitolyo, wilayani Shinyanga.
Ofisa Madini Mkoa wa Shinyanga, Joseph Kumburu, akizungumza hivi karibuni na wachimbaji wadogo wa Mwakitolyo, alisema kuwa tukio hilo limetokea Julai 17, mwaka huu na kuwa ajali hiyo ilitokea katika kitalu cha wachimbaji wadogo wa namba 5.
Kumburu alisema ajali hiyo imetokea majira ya saa 6:00 mchana wakati wachimbaji zaidi ya watano walipokuwa wakitoka ndani ya duara baada ya kumaliza kazi.
Kumburu alisema, kwa mujibu wa Mtaalam wa afya aliyekuwa kwenye uchunguzi huo, mtu huyo alipasuka kichwani na kusababisha umauti kutokana na kuanguka kutoka umbali wa mita 20, baada ya kuteleza na jiwe kumponda kichwani na kusababisha kifo chake.
“Marehemu hakuwa na majeraha yoyote zaidi ya kupasuka kichwa, niwashauri tu ndugu zangu wachimbaji muhakikishe mnazingatia taratibu na sheria za uchimbaji mnazoelekezwa na wataalamu wenu ili kufanya shughuli hizo kwa hali ya usalama zaidi kwa kuwa chanzo cha tukio marehemu alikosa nguvu,” alisisitiza Kumburu.
Kutokana na ajali za mara kwa mara zinazotokea kwenye machimbo hayo, Ofisa Madini huyo alifunga eneo kulipotokea ajali kwa siku tatu kupisha ukaguzi.
Kumburu aliandaa timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Madini, kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Salawe pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Shinyanga ili kusimamia ukaguzi huku akishauri hatua za haraka za kuchukuliwa kwa maduara yote yatakayobainika kuhatarisha maisha ya watu.
Ofisa Madini Kumburu aliwataka wachimbaji hao kuzingatia Sheria za madini na maelekezo wanayopewa na wakaguzi kufukia mashimo yote ambayo yameachwa wazi ili kuepusha ajali.
Chanzo: Nipashe