Tetesi: Ndugu yetu Hasheem Thabeet anarejea NBA

Hapo ndiyo Hasheem anafanya makosa kudai kafika kwa juhudi zake. Na laana za wale waliokuwa wana mnunulia raba akiwa Makongo Secondari, wakimpa nauli ya daladala, wakimfundisha kikapu ndizo zimamtafuna kwa kuto kuwa acknowledge.

Hata kama alikutana na scouts wa Kinigeria akiwa Nairobi na ndiyo wakampeleka U-Conn, lakini akumbuke bila coach wa timu ya Sekondari, bila wale waliomtoa kwenye football na Bongo fleva isingekuwa hapo alipo. Hilo ndilo linamtafuna na litaendelea kumtafuna.
 
Huyu ni mzembe tu!! Period. Siyo kwamba tunamchukia bali tunataka liwe fundisho kwa vijana wengine wa Kitanzania, wakipata fursa wasizichezee.


Unamchukia bure wakati yeye kile ndio kiwango cha chake. Kilichompeleka Hasheem Marekani ni urefu, sio kwamba anaupiga sana. Sio yeye kaanza kucheza Basket ukubwani, Bongo hapa kulikuwa na watu wengine kama Patrick Nyembera, Jenga Mapunda na wengineo ambao ni talented lakini huwezi kuwaweka kwenye mikikimikiki ya NBA. Huyu mjomba mna mpa lawama bure, yeye kacheza best level yake kamaliza, kama unaweza na wewe nenda tukuone acha ujuba
 
Na wewe mzembe pia kama Hasheem. Kwa hiyo alipeleka urefu wake tu akadhani ndiyo utamfanya adumu NBA?
 
Sema inasikitisha hiyo article nimeisom yote, sema hii statement inaonyesha bado ana imani ya kurudi NBA.

"I'm going back to D.C.," he said. "I've got to keep training. I'm still going to make it back to the NBA."
Angerudi tu nchini awekeze vijisenti vilibyobaki. Ila kwa vile hashauriki atakuwa huko mwishowe vitaisha then aanze kupiga box
 
Huyu Jenga Mapunda aliishia wapi??

Nakumbuka alikuwa mzuri sana.Kwa nini hakufika NBA??

THABEET angeweza kutumia urefu wake kujikita katika defence kama Dikembe Mutombo.
 
Hebu Ongeza sauti kidogo!! Sentensi ya mwisho inasema "Soon tutamuona tu NBA hata ikiwa game 1 inatosha kabisa"

Labda NBA ya Buza, hata G-League wameshammwaga
Huyo TOLU tulishasema hawezi kurudi NBA ya Kina Kobe Bryant labda NBA ya TANDALE kwa TUMBO.
 

We jamaa Curry na Hasheem walikuwa drafted the same year, na HASHEEM ALIKUWA 2nd Pick overall na Curry alikuwa 7th pick, Ambapo, The Los Angeles Clippers, who won the draft lottery used their overall draft pick to draft Blake Griffin na ndio alikuwa wa kwanza kwene hiyo draft ambapo pia hakucheza msimu mzima wa 2009-10 kwakuwa alikuwa amevunjika kneecap ya mguu wa kushoto.

So ukisema ujio wa kina curry ni kama unataka kusema curry alikuja baadae wakati sio kweli, wameingia wote NBA 2009 mmoja akiwa picked na Memphis G, na Curry akiwa picked na GSW...

Wakati draft inafanyika Hasheem numbers zilikuwa zinasoma kuliko Curry, sasa hapa nnachokiona ni kwamba ye mwenyewe alimesup na career yake, sa sijui sababu mbongo au niaje, sababu watu kama kina James Harden hadi leo wanakiwasha huko NBA...


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Alafu jamaa alivyochezea Rockets stats zote zinasoma 0.0 duuh...


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwa uandishi wako unajielezea pasipo maelezo kuwa wewe ni mfuatiliaji mzuri wa huu mchezo. Unajua wazi hali ilivyo hasa kwa rookies in their first years, timu huwa haziwatumii sana kutokana na ugeni wao katika league. Kuna wachezaji with very high draft picks katika timu zao kutokana na namna timu ilivyojengeka huwachukua zaidi ya msimu uwezo wao kuweza kuonekana na kuna wengine kutokana na timu zao zilivyojengwa basi hupata nafasi mapema.

Ujio wa wachezaji Kama akina Steph Curry, ulisababisha mapinduzi katika staili ya uchezaji ambapo game ilibadilika na mkazo kuwekwa kwenye shooting zaidi kuliko traditional basketball tuliyoizoea. Katika Era hii mpya, kila mchezaji licha ya nafasi anayocheza ilimlazimu kuwa na uwezo wa kushoot. Unaona wazi game ilianza kubadilika Center hawakuwa wakikaa ndani ya D, bali walikuwa wanatafuta spots behind the Arc, hali hii ilitengeneza mazingira magumu kwa wachezaji wa dizaini ya akina Hasheem ambao wao shooting haikuwa silaha kwao. Hapa unakutana na Centers kama akina Joel Embiid, KAT, Jokic na wengine, hawa ndo wanapata nafasi the rest kama akina Bismark Biyombo hawa nafasi zao ni finyu na wanapata muda mchache sana kucheza kutokana na sababu kama hizo.
 
Game imebadilika sana.
Nina hakika ata Dikembe Mutombo na Manute Bol nao wasingeweza kuduma katika NBA ya sasa
 
Game imebadilika sana.
Nina hakika ata Dikembe Mutombo na Manute Bol nao wasingeweza kuduma katika NBA ya sasa
Ndio hapo angalia namna Bol Bol with 7"2 ambaye ni Center alivyo i-shape game yake, he can dribble, shoot 3 like a SG. SHAQ mwenyewe angekuwa na wakati mgumu sana labda apate PG wa kumchezesha kama Chriss Paul vile.
 
Mkuu kwanza mimi sijasema kama nimemfikia na inawezekana kweli nisimfikie kwa miaka yote ya utafutaji wangu ila kinachosemwa na kuangaliwa hapa ni ile nafasi aliyonayo ameitumia vipi...na hakuna aliyefurahi anguko lake lakini ila hatuwezi kumsifia kwa kilichotokea lazima usemwe ukweli ili wengine tujifunze kupitia yeye.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…