Ndugu zetu wa Kagera kwanini mkoa wenu unaongoza kwa umasikini?

Ndugu zetu wa Kagera kwanini mkoa wenu unaongoza kwa umasikini?

Ndio maana nikakuomba unitajie wewe ni tajiri unayetokea mkoa gani??!! Maana Ninachokiona hapa ni mihemko tu kwani viashiria vya umasikini ni vipi mkuu tajiri???
Watakuhangaisha Bure ukute mkoa anakozaliwa anaogopa hata kurudi tangu amepata bahati ya kuondoka. Wachagga huko kilimanjaro wamedumaa sasa hivi hata halmashauri zao kwenye mapato ya ndani hazina tofauti na kigoma [emoji23][emoji23]
 
Ni watu wasio na fikra pana. Soko ama liwe stand hii ni miradi mikubwa na ndo miradi kichocheo, haijengwi na na wananchi bali serikali ikiamua.

Kama sahivi wameamua itajengwa na ndo kupeleka maendeleo kwa wananchi. Na si hayo tu,

Wanaweka RC wanajeshi kila siku ili iweje, mbona kwingine wanapeleka watu wa maana wenye CV zao na madegree yao wanaojua kupambanua mambo sasa iweje washika mitutu Kagera enzi zote as if kuna vita ama ni darful. Sasa wanataka wananchi ndo wateue RC, hilo ni jukumu lao kweli?

Vyuo na taasisi za serikali tunaziona kwa mikoa ya wengine ila Kagera ahaa! Sasa wananchi waache kujenga vibanda vyao vya kuishi wakajenge ofisi za serikali?

Kilimo ndo hicho, mkoa unategemea kilimo kwa 70% lakini eti leo ndo wanaanza kujikosha, wananchi wakulima ndo wangenunua kahawa yao wenyewe ama serikali ilitakiwa kutafuta wanunuzi kwa wakulima wake. Leo sasa aliyeleta bei mpya ni wakulima ama serikali, siku zote ilikuwa wapi na walitegemea nini
nini kwa mkoa?

Usafiri si waliua meli ikawa hamna kwa miaka zaidi ya 15, walitaka wananchi wamudu vipi maisha yao?

Nchi hii basi tu, wabaya zaidi ni hawa watu wa jf waliopita shule lakini hata kuchambua mambo hawawezi na bado daily wanajaza saver. Hii siyo sawa kabisa.
Rweye umenena. Huu ndio uchambuzi wa kisomi.
Kagera imedumaa kwa sababu nyingi ikiwemo uwekezaji duni kutoka serikali kuu na kuwa na Ma RC wanajeshi mara kwa mara.

Alikuwepo RC Massawe alijitahidi sana kuendeleza mkoa wa Kagera. Alikuwa na mikakati ya kupambana na ugonjwa wa migomba wa mnyahuko. Alianza kujenga uzalendo wa kupenda mkoa wa Kagera kwa wananchi. Usafi ndani ya miji na vijiji ulikuwa unaanza kuwa tabia ndani ya jamii. Mh Masawe hakudumu.
 
ITV jana nao kwenye taarifa yao habari juu ya utaperi wa Qnet wilaya ya Ubungo wakamuonyesha mama wa Kihaya eti anashangaa "...eti na muhaya anatapeliwa na Qnet kweli?...muhaya huwa hatapeliwi kizembe..."
 
Back
Top Bottom