Ndugu zetu Wa kanda ya ziwa ndio mnaongoza Kwa matukio ya Ukatili hapa nchini. Tatizo ni nini?

Ndugu zetu Wa kanda ya ziwa ndio mnaongoza Kwa matukio ya Ukatili hapa nchini. Tatizo ni nini?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Tangu napata Akili nikiwa sekondari nasikia matukio ya kikatili yanayotokea huko Kwa Ndugu zetu wa Kanda ya ziwa, mpaka nafika chuo na sasa nimekuwa mtu mzima bado nasikia matukio ya kikatili huko kanda ya ziwa.

Haiwezi kuisha siku mbili bila kusikia matukio ya kikatili kutokea kanda ya ziwa, wakijitahidi Wiki.

Geita mara Kwa mara ndio hujitokeza, kuna haja ya Serikali na wasomi kufanya utafiti kujua hawa Ndugu zetu Wana matatizo gani,

Mfano wa matukio, ni Kama;
1. Watoto kuua wazazi wao Kwa visa vya kijinga jinga,
2. Vikongwe kuuawa Kwa sababu za kishirikina na Uchawi
3. Wazazi kuua watoto Kwa sababu za kustaajabisha, utasikia ati mama au Baba aua mtoto kisa Kula mboga,
4. Kuua Albino
5. Kuua kisa mapenzi, utasikia Mume aua mke na watoto kisa wivu wa mapenzi.

Yaani kuna matukio ya kikatili ambayo yanaitia aibu kanda ya ziwa, na kuwafanya watu wake waonekane wakatili.

Nadra Sana kusikia matukio hayo yakitukia kanda ya kusini yaani Lindi, mtwara, na Songea. Nadra Sana. Inaweza kupitia hata mwaka mzima usisikie kitu Kama hicho.

Watu wa kanda ya Ziwa niwasihi kuwa, mjitahidi msiendekeze mihemko hasa ya Hasira za kijinga jinga,

✓ Acheni Hasira za kijinga jinga
✓ Wapewe Elimu
✓ Msijione Duni, tabia ya kujiona Duni husababisha mtu kutenda mambo ya kikatili ili kujitutumua kuwa ananguvu. Mfano, mwanaume ambaye hajiamini, anayejiona Duni mbele ya Mke wake hutumia mbinu ya kumpiga mkewe kila mara kuonyesha kuwa yeye ni kidume. Hapo kwenye Kupiga ndio matokeo yake mauaji wakati mwingine hutokea. Yaani anatafuta kuheshimiwa Kwa nguvu.

Zingatia, mwanaume yeyote anayependa kupigapiga au kutumia nguvu ili aheshimike lazima atakuwa anajiona Duni, anaona anadharaulika, anaona anaonekana sio lolote. Hiyo ni Kwa mtu yeyote kutoka mahali popote.

✓ Acheni kujiona miungu watu,
Watu wa kanda ya ziwa hata Kwa tuliosoma nao wakiwa viranja shuleni boarding, wanatabia ya Kupenda kuabudiwa, kunyenyekewa, Wewe kuwa Baba au mume haimaanishi wewe ni Mungu kiasi kwamba kila usemalo linapaswa kufanywa hata Kama umekosea.

Mkikutana na watu waliokinyume na mtazamo wako ndio ugomvi unatokea, Mfano wapo wanawake ambao hawataki kupelekwa pelekwa hata Kwa vitu vya kipuuzi kisa tuu wewe ni Mwanaume/mume wake.
Mpeleke ikiwa ni Jambo sahihi sio umpeleke peleke hata kwenye upuuzi. Mfano, umechelewa Kurudi NYUMBANI alafu hutaki kuulizwa, au unatumia pesa Rafu alafu hutaki kuulizwa, tabia hii pia wanayo wanaume wa kichaga.

Migogoro mingi ndani ya Nyumba pia husababishwa na Baadhi ya Sisi wanaume kujigeuza miungu watu. Mwishowe Kwa wale vichwa maji huishia kupigana na Wake zao. Hali iñayopelekea matukio ya mauaji.

✓ Kanda ya ziwa wengi wao wanamapenzi ya dhati, yaani wanapenda kweli.
Acheni hii tabia ya Kupenda kupitiliza, wapendeni wazazi wenu, Hawa wanawake WA siku hizi msiwaendekeza Sana, msiwapende kivile.
Kupenda Sana wakati mwingine ni ushamba,
Unakuta Umeoa Msichana mzuri tena wanapenda weupe, anamhudumia Kwa Hali zote alafu mwisho WA siku anamsaliti, kutokana na Asili Yao kuwa na hasira na kutopenda kudharaulika huamua kufanya mauaji Kama Suluhu.

Kuweni Kama watu wa Pwani, wao unakuta mwanamke ameachwa hata mara Saba Kwa kupewa talaka, au unakuta Mwanamke anacheza kigoma au kigodoro akivua nguo lakini ni mke WA Mtu. Waswahili huchukulia mambo simple.

Usimpangie mtu Maisha ikiwa yeye mwenyewe kaamua kuishi vile atakavyo, wewe ukishindwa toa Talaka na sio umlazimishe mtoto wa watu kufuata mambo yako ambayo yeye hataki.

Ndio hayo mambo ya kujiona mungu mtu ndio maana unaingilia Uhuru wa mwingine, MUNGU mwenyewe aliyemuumba haingilii Uhuru wa watu sembuse Sisi.

Mtu Kama hataki kufuata sheria zako, achana Naye, mpe Talaka. Na Kama unataka kumpa kipigo😀😀 subiri ukiwa huna hasira ili umpe kipigo heavy Kwa akili, chukua fimbo umchape mpaka akili imkae Sawa. Hii ni Kama umeshindwa kuachana Naye.

Ujumbe huu sio tuu Kwa Watu wa kanda ya ziwa, nimewatumia wao kama kielelezo kutokana na kuwa vinara wa matukio ya kikatili hapa nchini, Ila ni ujumbe unaohusu watu wote pia wenye tabia za ukatili.
Zingatia, sio kila mtu kutoka kanda ya ziwa anatabia za ukatili Ila matukio yanayotokea huko ndio huwaharibia mpaka wale waliowema.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Nasikia wale wa kaskazini marekani wanauna sana kikatili wanaua watoto washule. Mpaka sasa au leo hii toka watoto walivyouwawa kule Texas,Uvalde sasa waliouwawa na kujeruhiwa ni kama 120! yaani wiki mbili tu!

Wazungu wa Kaskazini wakatili sana. Wanawashinda wa kwetu wa Kaskazini Tanzania.
 
Nasikia wale wa kaskazini marekani wanauna sana kikatili wanaua watoto washule. Mpaka sasa au leo hii toka watoto walivyouwawa kule Texas,Uvalde sasa waliouwawa na kujeruhiwa ni kama 120! yaani wiki mbili tu!

Wazungu wa Kaskazini wakatili sana. Wanawashinda wa kwetu wa Kaskazini Tanzania.

Mtu mkatili mara nyingi huwa na magonjwa ya Akili, au madhara ya kisaikolojia wakati WA utoto.

Tabia ya kupigapiga au hasira zisizo na maana ni tatizo la kiakili,
 
Sisi watu, hatupendi dharau ni desturi yetu, ukijichanganya unaliwa kichwa

Mnajaribu kusema mnajiona Duni na hamjiamini.

Mtu duni ndio huwa na tabia hizo.

Embu fikiria Mungu pamoja na nguvu zake lakini unaweza kumdharau na asikufanye lolote, ni Kwa sababu anajiamini, haiendeshwi na hisia za kipumbavu, hajioni Duni, na haiendeshwi na mambo ya watu dhaifu.

Badilikeni muache kujiona Duni.
 
Huko mtu akifa kwa malaria au ugonjwa wowote wanashangaa, wamezoea vifo vyao ni kwa kuchinjwa au kuchomwa moto au risasi ilimradi umeuawa na si kifo cha kawaida
Hiyo ni Laana, maana ukiua kwa upanga nawe utakufa kwa upanga.
 
Mtu mkatili mara nyingi huwa na magonjwa ya Akili, au madhara ya kisaikolojia wakati WA utoto.
Ndio maana. Duh Wazungu hatari wakiwa na magonjwa ya Akili. Kuua ua tu.
Tabia ya kupigapiga au hasira zisizo na maana ni tatizo la kiakili,
Kweli, huko ulaya na Marekani sasa wanajaribu kupunguza makali hayo, wanawasokomeza madawa mpaka ili wapone hawaponyeki ndio kwanza wanaenda kununua silaha za kivita na kuendeleza ukatili.

Haya yananyemelea huku Tanzania. Lakini Ulaya na Marekani wamezidi.
 
Sisi watu, hatupendi dharau ni desturi yetu, ukijichanganya unaliwa kichwa
Haha Mzalendo, Unajua kule Ulaya au Marekani, scratch that. Wazungu wakitwangana wanasema wanarekebishana, weusi wakitwangana, toba! Makatili.
Ushaona vurugu za kriketi za kwao? Basi unasikia walikuwa wanarakabisha uhusiano. Ushaona vurugu kwenye netiboli yao ile inayofanana na Ragbi? Wakikunjana tu na kazi kwisha.

Wazungu makatili sana
 
Ukuaji wa mtu kuanzia utoto na imani yake kuhusu mungu huchangia hayo ndio maana tumeambiwa mke akizingua achananae tafta mwengine lakini wanaoamini ni pingu ya maisha tatzo huanzia hapo.
 
Back
Top Bottom