Ndumba za hii timu ni hatari mno

Ndumba za hii timu ni hatari mno

Ni nadra sana ukifanya vizuri kwenye hii timu kisha ukaondoka bado wanakuhitaji ukatoboa unakokwenda.Ndio maana wana jeuri ya kukutunia muda wowote unapodai haki yako.

Upo uwezekano kuwa huenda kuna nguvu ya ndumba huwa nyuma ya uchezaji bora wa wachezaji wao na makocha wao.

Angalia makocha wao waliofanya vizuri wanapoenda timu nyingine.Wengine walipachikwa majina ya ubobevu eti tu kwa kudhaniwa wana uwezo mkubwa sana,lakini huko waliko sasa,huo ubobevu umeyeyuka.

Wengine walipata ufungaji bora Afrika lakini sasa huko waliko wanasikitisha.

Kwa nyie mliopo sasa kwenye hii timu,msianze kuzingua maana huo ndio utakuwa mwisho wenu.Hamuwezi kwenda popote hadi viwango vyenu vishuke.Ondoeni ndoto za kwenda ulaya
Ingekuwa vizuri ukatutajia hiyo timu ili tuje na mifano kabisa, badala ya kuleta mafumbo hapa. Mimi wachezaji ninaowafahamu walioondoka Tanzania wakachemka huko walikoenda ni hawa wafuatao:
1. Makambo - Toka Yanga
2. Chama - Toka Simba
3. Miquison - Toka Simba
Haya tuendelee sasa kuwataja wengine walioathirika na ndumba za timu zao baada ya kuondoka.
 
Ingekuwa vizuri ukatutajia hiyo timu ili tuje na mifano kabisa, badala ya kuleta mafumbo hapa. Mimi wachezaji ninaowafahamu walioondoka Tanzania wakachemka huko walikoenda ni hawa wafuatao:
1. Makambo - Toka Yanga
2. Chama - Toka Simba
3. Miquison - Toka Simba
Haya tuendelee sasa kuwataja wengine walioathirika na ndumba za timu zao baada ya kuondoka.
Nadhani wanajielewa tu na utawaona hapa wanakuja wamepanic
 
Ni nadra sana ukifanya vizuri kwenye hii timu kisha ukaondoka bado wanakuhitaji ukatoboa unakokwenda.Ndio maana wana jeuri ya kukutunia muda wowote unapodai haki yako.

Upo uwezekano kuwa huenda kuna nguvu ya ndumba huwa nyuma ya uchezaji bora wa wachezaji wao na makocha wao.

Angalia makocha wao waliofanya vizuri wanapoenda timu nyingine.Wengine walipachikwa majina ya ubobevu eti tu kwa kudhaniwa wana uwezo mkubwa sana,lakini huko waliko sasa,huo ubobevu umeyeyuka.

Wengine walipata ufungaji bora Afrika lakini sasa huko waliko wanasikitisha.

Kwa nyie mliopo sasa kwenye hii timu,msianze kuzingua maana huo ndio utakuwa mwisho wenu.Hamuwezi kwenda popote hadi viwango vyenu vishuke.Ondoeni ndoto za kwenda ulaya
Unazungumzia Simba ambao walikuwa na hawa baadhi ya watu

Kocha Sven, kocha Gomez, kocha Ausems waliifanya Simba ifike robo fainali michuano ya CAF na walipotoa Simba tu hawakuvuma tena.

Chama na Miquison walipoondoka Simba walipoenda timu mpya wameshindwa kutamba huko
 
Sisi ndio tunashangaa.Kocha anapewa sofa za ubobevu,je huu ubobevu unayeyukia wapi akihama timu?Kama si ndumba ni nini?
Huyo kocha mbobevu hakupatia mafanikio yake Yanga tu, mkoba wake una kombe la shirikisho alilochukua akiwa na As Leopard ya Congo, timu aliyoikuta ikiwa haina mafanikio yoyote ya mashindano ya Afrika...
Kushindwa kwake kwenda makundi hakumaanishi kwamba uwezo umeisha kutokana na hiyo imani yako potofu, hata alipokuja Yanga msimu wa kwanza alitolewa na Rivers, msimu wa pili akatolewa na Al Hilal na kuangukia shirikisho alikofika fainali...
Kumbuka Karma inafanya kazi, watu wakikupenda sana kisha ukavimba kichwa na kuwaacha kwa ubaya lazima yakukute, mfano mzuri ni Eden Hazard
 
Ingekuwa vizuri ukatutajia hiyo timu ili tuje na mifano kabisa, badala ya kuleta mafumbo hapa. Mimi wachezaji ninaowafahamu walioondoka Tanzania wakachemka huko walikoenda ni hawa wafuatao:
1. Makambo - Toka Yanga
2. Chama - Toka Simba
3. Miquison - Toka Simba
Haya tuendelee sasa kuwataja wengine walioathirika na ndumba za timu zao baada ya kuondoka.
Usisahau Uchebe na Da Rosa
 
Unazungumzia Simba ambao walikuwa na hawa baadhi ya watu

Kocha Sven, kocha Gomez, kocha Ausems waliifanya Simba ifike robo fainali michuano ya CAF na walipotoa Simba tu hawakuvuma tena.

Chama na Miquison walipoondoka Simba walipoenda timu mpya wameshindwa kutamba huko
Sasa hapo ndio ujue Simba ni timu nzuri yenye mifumo na mazingira mizuri ambayo wachezaji na makocha wanafanikiwa kirahisi, wakivimba kichwa na kujiona ni wakubwa kuliko timu inakula kwao

Hao makocha nawafananisha na mwalimu ambaye alikuwa anafaulisha vizuri wanafunzi akavimba kichwa akadhani ni uwezo wake binafsi tu bila kujua pia mazingira mazuri ya shule na wanafunzi bora wanaosajiliwa na shule vinachangia, akahama na kwenda shule za vichochoroni na kujuta

Hata wachezaji wanapaswa kutambua kuwa mwanafunzi kufanya vizuri mazingira ya shule yanachangia sana
 
Maisha ya mayele yanaendeleaje huko pyramids?
 
Unazungumzia Simba ambao walikuwa na hawa baadhi ya watu

Kocha Sven, kocha Gomez, kocha Ausems waliifanya Simba ifike robo fainali michuano ya CAF na walipotoa Simba tu hawakuvuma tena.

Chama na Miquison walipoondoka Simba walipoenda timu mpya wameshindwa kutamba huko
Ulisikia kuna profesa hapo?
 
Hakuna mchezaji mkubwa kuliko timu. Mimi sio shabiki wa hio timu na wala sipo hapa kutoa utetezi ila kuna mifano mikubwa tunaiona hata huko ulaya mchezaji akiondoka kwa kufosi huku timu ikiwa inahitaji huduma yake safari yake ya soka hua inakua ngumu.
Cheki mane coutinho eden hazard hao ni wachache
Mane anakula bata uarabuni tena anaporomosha majumba ya kifahari kwako maybe hao wengine
 
Back
Top Bottom