Uchaguzi 2020 NEC: Kila Chama cha Siasa kimeruhusiwa kuweka wakala kwenye kila kituo ili kulinda maslahi ya Chama na Wagombea

Uchaguzi 2020 NEC: Kila Chama cha Siasa kimeruhusiwa kuweka wakala kwenye kila kituo ili kulinda maslahi ya Chama na Wagombea

Umehitimisha vema, lakini pia njaa haihalalishi 'rushwa' kwa mnunuaji.
Ungepewa nafasi ya kuhakikisha hili tatizo linaisha ungeshuri nini kibadilike,hii hoja ya wanaosema wapige kura kisha wabaki vituoni kuzilinda,unaichukuliaje?
 
Ungepewa nafasi ya kuhakikisha hili tatizo linaisha ungeshuri nini kibadilike,hii hoja ya wanaosema wapige kura kisha wabaki vituoni kuzilinda,unaichukuliaje?

Elimu kwa wapiga kura, mfumo wa kisasa wa upigaji kura.... huwezi kulinda masanduku ikiwa hayo hapo juu yamezingatiwa.
 
Siku ya uchaguzi msije mkasema ati kwamba nakala za matokeo ya kura hazitoshi hivyo hamtawapatia mawakala wa vyama!!
 
Elimu kwa wapiga kura, mfumo wa kisasa wa upigaji kura.... huwezi kulinda masanduku ikiwa hayo hapo juu yamezingatiwa.
🙏🙏, Siioni hoja ya kulinda kura Kama suluhisho,hiyo Ni sawa na kuboresha nyumba yenye msingi mbovu.Mabadiliko yanapaswa kuanzia kwenye mfumo wa kisiasa.Naungana na wewe.
 
Hivi ni kwanini kuna Chama cha Siasa kinapinga sana suala la kubaki kulinda kura mara baada ya kupiga kura? Sheria siinasema ubaki mita 200? Au hiyo Sheria mwaka huu haipo?
 
Baada ya kupiga kura wanachama wataruhusiwa kulinda kura zao?
Kazi ya kulinda usalama wa shughuli zote za uchaguzi ni kazi ya polisi sio wanachama wa CHADEMA au chaumma,

Unakwama wapi mkuu?
 
Na asipoenda nyumbani? Mathlani akienda kanisani au msikitini? Kazini? Shambani? Kwa mpango wake wa kando? Kwenye kijiwe cha jirani? Akifanya vyote badala ya kwenda nyumbani atakuwa amekiuka kifungu kipi cha sheria ipi?

Amandla....

hatavucha kifungu cha sheria yoyote,ila akikaa hapo kwa nia ya kulinda kura,akikaa hapo kwa nia ya kucheza mpira,akikaa hapo kwa nia ya kufanya mnada atakuwa navunja sheria.
 
Shida sio kuruhusu au kutoruhusiwa kwa vyama kuweka mawakala wao, bali shida ni figisu na hujuma wanazokumbana nazo mitaani kwenye vituo vya kupigia kura! Kuna wengine huzuiwa kuapishwa kwa sababu tu za kubumba ili chama kikose wakala! Hata walioapishwa kuna sehemu nyingine wan atolewa nje wakati wa kuhesabu kura kwa visingizio vya uongo eti wanafanya fujo!
Tunashauri kama kweli NEC imejipanga kusimamia uchaguzi huu kwa haki na usawa, iandae pia mazingira ya kuhakikisha maazingira ya kuhujumu mawakala hawa hayapewi nafasi!
 
Mi nashauri NEC ingeruhusu mawakala wawepo jimboni tu,,kuweka wakala kila kituo ni gharama sana,bora pesa zinazobaki ziende kwenye mradi wa reli ya umeme,,
 
hatavucha kifungu cha sheria yoyote,ila akikaa hapo kwa nia ya kulinda kura,akikaa hapo kwa nia ya kucheza mpira,akikaa hapo kwa nia ya kufanya mnada atakuwa navunja sheria.
Sheria ipi inamzuia mtu kukaa karibu na kituo cha kupigia kura? Sheria ipi inasema ni activity zipi zimezuiwa kufanywa karibu na kituo cha kupigia kura? Ninavyojua mimi mtanzania ana haki ya kukaa bila kubughudhiwa katika maeneo yote ambayo ni "public" ili mradi hafanyi vitendo ambavyo vimekatazwa na sheria ( kuvuta bangi, kunywa gongo, kupigana n.k.). Mtu atachukuliwa hatua kwa vitendo anavyofanya na sio kwa kujikalia tu. Mtu kama hauna nia mbaya kwa nini uogope watu kushuhudia unachofanya? Mimi ningetegemea kuwa ungependa uwe na mashahidi wengi iwezekanavyo ili pasiwe na shaka juu ya weledi wako.

Amandla...
 
Shida sio kuruhusu au kutoruhusiwa kwa vyama kuweka mawakala wao, bali shida ni figisu na hujuma wanazokumbana nazo mitaani kwenye vituo vya kupigia kura! Kuna wengine huzuiwa kuapishwa kwa sababu tu za kubumba ili chama kikose wakala! Hata walioapishwa kuna sehemu nyingine wan atolewa nje wakati wa kuhesabu kura kwa visingizio vya uongo eti wanafanya fujo!
Tunashauri kama kweli NEC imejipanga kusimamia uchaguzi huu kwa haki na usawa, iandae pia mazingira ya kuhakikisha maazingira ya kuhujumu mawakala hawa hayapewi nafasi!
Tumeona hivi karibuni watu wakijitokeza kugombea kwa niaba ya chama ambacho hakijawateua. Na wasimamizi kukataa kata kata kusikiliza hoja za chama ambacho wanadai kimewateua. Haitakuwa ajabu kukuta mawakala wapo tayari wa vyama ambavyo havijawateua. Huu ndio wasiwasi wa wengi. Njia pekee ya kuwaondoa watu huu wasiwasi ni kufanya kila kitu kwa uwazi kabisa na kuvishirikisha vyama vyote kikamilifu katika hali ya usawa.

Amandla...
 
utatolewa kwa kufanya mkusanyiko usio na kibali.
Hahaha yaani kipindi hiki kumekuwa na makosa mengi mpaka shetani mwenyewe anatushangaa. Ukiingia kwenye mikono ya polisi tu hutoki salama
 
Jumla ya Makundi 16 ya waangalizi wa nje wapewa fursa na vibali vya kufuatilia mwenendo wa shughuli ya uchaguzi Tanzania huku asasi za kiraia na taasisi 97 za ndani pia zikipata nafasi hiyo.

Amebainisha hilo Kamisha wa tume ya taifa ya uchaguzi (NEC) Jaji mstaafu Mary Longway wakati wa mkutanao na wadau wa uchaguzi uliofanyika ukumbi wa halmashauri ya mji wa Njombe mkoani humo.

“Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeruhusu watazamaji wa ndani na nje,katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ambapo imetoa vibali kwa asasi za kiraia na taasisi 97 za ndani na vibali kwa makundi 16 ya watazamaji wa nje” alisema Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi

Anasema “Siku ya uchaguzi vyama vya siasa vimepewa nafasi ya kuweka wakala katika kila kituo cha kupigia kura, wakala atakuwepo kituoni kwa ajili ya kuangalia utaratibu wa uchaguzi zinazoendelea kituoni pale na kama zinazingatia sheria, kanuni, taratibu na maelekezo yanayotolewa na tume, lengo kubwa ni kulinda maslahi ya Chama na wagombea wake”amesema Jaji mstaafu Mary Longway Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi

Hata hivyo amesema “Tayari vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki uchaguzi, vimepata nakala tepe ya orodha ya wapiga kura waliomo katika orodha ya daftari la kudumu la wapiga kura hii ni kuwawezesha mawakala kutimiza wajibu wa kuhakiki wapiga kura wanaofika kituoni” Jaji mstaafu Mary Longway Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi

Jaji mstaafu Mary Longway amesisitiza kuwa “Tume inasisitiza umuhimu wa vyama vya siasa na wagombea kuzingatia maadili ya uchaguzi katika kampeni zao, ikwemo kuepuka Lugha za kashfa, maneno ya uchochezi yanayotishia usalama na amani ya Nchi” Jaji mstaafu Mary Longway

Aidha amesema“Wakati tume inaendelea kuratibu, kusimamia na kuendesha uchaguzi huu kwa kutumia sheria za uchaguzi. Vyama vya siasa, wagombea na wananchi wanakumbushwa kuwa katika kipindi hiki sheria nyingine za nchi hazijasimama” Jaji mstaafu Mary Longway Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi

Amewahakikishia wananchi kuwa tume itaendelea kufuata katiba na sheria katika utekelezaji wa majukumu yake.

“Tume inawahakikishia wananchi kuwa, imejipanga katika kusimamia uchaguzi wa mwaka huu kwa kufuata katiba, sheria, kanuni na miongozo mbali mbali na inaamini kuwa kila mdau akitimiza wajibu wake kwa kufuata taratibu basi watanzania wataweza kupiga kura kwa amani” Jaji mstaafu Mary Longway Kamishna wa tume ya taifa ya uchaguzi
hao mawakala waapishwe mapema kuepusha habari za Akwilina
 
Mwakala wa vyama vingine 13 wakiungana dhidi ya wakala 1 kubadilisha matokeo ataweza kujitetea peke yake?
Kama umeshindwa kumwamini wakala wako atizame kura zako sasa umemweka wa Nini?
 
Kwa sababu wanaweza kuhongwa wakabadili matokeo au wakazidiwa nguvu na mawakala wengine wengi wa vyama tofauti lakini wenye mrengo mmoja.
Sikutaka kuizingatia phrase ya mleta mada, nimezingatia maelezo yako kwamba "huwa ni utaratibu mawakala kuwepo",jambo ambalo ndio ukweli wenyewe, hivyo sikupingi kumkosoa mleta mada.
Swali langu ni, kwanini baadhi ya vyama hulalamika kuibiwa Kura baada ya uchaguzi, licha ya kuwepo kwa Hawa watu?
 
Hili nalo linahitaji ruhusa...., au its a given na ni obvious...., Hii nchi unaweza kuambiwa siku moja kwamba tumekupa ruhusa ya kupumua.... na kuvuta oxygen
 
Back
Top Bottom