NECTA yatoa ufafanuzi kuhusu mjadala wa ufaulu kati ya shule ya Wasichana ya Anwarite na ya Wavulana ya Feza

NECTA yatoa ufafanuzi kuhusu mjadala wa ufaulu kati ya shule ya Wasichana ya Anwarite na ya Wavulana ya Feza

Kisiasa Malisa GJ anaweza akawa na hoja, lakini kitaalamu NECTA wako sahihi kutegema na namna wanavyokokotoa. Mfano, division one za points 7 zipo zaidi ya mia, lakini bado kuna wa kwanza hadi wa mwisho. Kwa maneno ya Malisa GJ wote walitakiwa wawe wa kwanza sio?
 
Hoja yako Ina mashiko ,ila hapo mwishoni umeharibu ...

Skia, mpangilio wa shule Bora haufanywi Kwa kuangalia idadi ya division 1....Bali wanaangalia wastani wa pointi ( average grade points ) za hizo division 1 ,2 ,3 etc

Inawezekana hao Feza wamepata division 1 za 7 ,8 na 9 nyingi , division 2 za mwanzoni kbs na division 3 ya mwanzoni, huku hao Anwarite wakipata 1 za 7,8 9 chache na 1 za 17 ,16 ,15 nyingi ...

Inawezekana kbs ( japokuwa sijaona hayo matokeo )
Nimepandisha matokeo cheki mwenyewe
 
Hili jambo kuna mahali nimelielezea vizuri.
Nakupa home work.
Chukua wastani wa shule hizo mbili kisha njoo uandike tena Uzi mwingine
 
Nafasi za shule zinapangwa kwa kuzingatia wastani wa jumla, yaani overall GPA sasa ukiangalia GPA ya anwarite ni 1.3409 wakati ua feza boys ni 1.3107

Kwa kifupi tu ni kuwa wastani wa feza ni mkubwa kuliko wa anwarite. Nadhani utakuwa umeelewa
Aelewenini ktk huu utopolo, yaani Anwarite 1.3409 na Feza 1.3107 number ipi ni kubwa hapo ambazo unaziita GPA? mbn hamuoni ht aibu?
 
Tatizo la wanaharakati wetu kupenda kubakia relevant mitandaoni.
 
Mbona hilo swali jepesi mkuu.
Kujua nafasi ya shule wanaangalia wastani wa maksi mwanangu.
Kuna mtu anapata one ya 7
kila somo kapata 100
Chukulia wote wamepata hivyo

Kuna mtu anapata one ya 7
kila somo kapata 81

nadhani umeelewa
 
Kwa hiyo zile seminari za kushinda miaka ile kila kukicha nazo zilikuwa zinapewa michongo....🤔 inawezekana....
Je Tosamaganga, Ilboru, Tabora boyz, ?
Kweli kutesa kwa zamu....
Lakini kwa sasa ukweli ni kwamba wazazi wenye hela ndio watoto wao wanafanya vizuri na huu ukweli ndio upo hata kwa nchi za mabeberu..
Na inawezekana hao wa hizo shule za Div 1 walipasi vizuri kwenda za shule za serikali lakini wazazi pesa ndefu wanawapeleka za kulipia ndio maana matokeo yanajieleza.....
 
Elimu kutumika kisiasa ni jambo la hatari sana maana nchi itazalisha vilaza wa bora liende.Kinachonisikitisha zaidi TZ inamalengo ya kuwa Taifa la viwanda sasa unabaki unajiuliza kwa mfumo huu wa elimu hivyo viwanda si vitaongozwa na wageni wenye ujuzi huku wazawa wakibaki manamba?

Serikali kwa kiu yake ya kutaka kuaminika kua ubora wa elimu umekua na ufauru umeongezeka imejikuta ikifuta adhabu ya penati kwa waliopata F somo la hesabu, awali ilikua kwamba mwanafunzi akiwa na cutpoints zinazomruhusu apate aidha div 1 au 2 lakini akapata F ya somo la Hesabu au uraia basi moja kwa moja atapigwa penati na matokeo yake yatakua sio 1 au 2 bali div 3..Umeona sasa wataka sifa walivyo! Ufaulu wa kidato cha nne 2021umeongezeka kwa kiwango cha kutisha huku one na two ikiwa si kitu tena(thaman ya ufaulu kwisha habari yake) maana wapo waliotakiwa kuwa na div 3 yani wana F ya hesabu ila serikali ilipeta kuongeza idadi ya ufaulu.

Hayo si maajabu maajabu zaidi ni kuwa vijana wanaosoma special wale wenye ufaulu mkubwa sana na vijana wanaosoma shule za Kishua kwa mazingira na ufundishaji kama Feza, St Francis, KEMOBOS nk eti wanapimwa kwa mtihani sawa wa Taifa na kijana anayesoma Nyanembe Sekondari ya kata ambayo picha linaanza shule waalimu hawatoshi kuanzia form 1 hadi four mwalimu wa hesabu na fizikia yupo mmoja shule nzima, darasa moja linawanafunzi zaidi ya 100, madarasa hayaleweki umeme hakuna, maji kilomita buku mwanafunzi ambaye lazima atembee zaidi ya KM 5 kutoka anapokaa hadi shule ndo apate elimu, mwanafunzi huyu hana cha library wala huduma ya Internet desa pekee analotegemea atoboe nalo nekta ni kutoka kwa mwalimu shija ambaye naye mda mrefu anashinda Town akipiga madili ya tuition kweli kabisa mnawapima kwa viwango sawa hawa wanafunzi? Hii ni aibu


Ajabu la ziada elimu hii ni huu uhuni wa kupanga matokeo usioleweka lengo tu ionekane ufaulu umeongezeka tuangalie mfano mdogo hapa Shule Ya ANAWARITE GIRLS ina Wanafunzi 76 Na Wote Wamepata Division 1, Alafu Imekua Shule Ya 11 Kitaifa, Wakati Huohuo FEZA BOYS Yenye Wanafunzi 62 Na Inayo Division 1, 2 Hadi 3 Lakini Imekua Shule Ya 7 Kitaifa(Credit Malisa G) .Hapa unajiuliza Wataalamu Walitumia Vigezo Gani Kuzi Rank Hizi Shule? Wamenunuliwa, bahati mbaya au shida ya kimfumo.

Wanasiasa msitumie elimu kujinufaisha mnaua msingi wa Taifa la kesho

View attachment 2092707

View attachment 2092841

View attachment 2092842
Sion sababu ya kujadili minor case kama hizi..
Wote wapate one, two, three nk sion tatzo.
Tatzo linakuja tunaoanza kudai impact ya hizo point kwenye maisha yetu ya kila siku
na ujenzi wa taifa.
 
Imagine one zote za Anuarite ziwe ile ya mwisho kabisa; then wale 59 wa Feza ni wani kali, the best ya pointi ^sir-bar.^ Hapo ni wazi kama mchana wa mwanga kwamba GPA ya Feza lazima iwe kubwa kuliko hao jamaa wa wani zote. (Just trying to be reasonable!)
 
Back
Top Bottom