Nehemia Mchechu bila ya ‘speed governor’ ni tatizo. Ndugu zangu wa mitaa ya ‘Al Muntazir’ Upanga mjipange

Nehemia Mchechu bila ya ‘speed governor’ ni tatizo. Ndugu zangu wa mitaa ya ‘Al Muntazir’ Upanga mjipange

Hivi hii sera ya ubia ya NHC ilipelekwa kabisa kwenye baraza la mawaziri, wakailewa na kusema sawa.

Mtu ana mpango wa kwenda kuvunja majengo kadhaa kisa tu yapo prime areas na kuwatoa wapangaji sio tu hana hela ya kuendeleza yeye mwenyewe bali the immorality of it all is beyond me.

Kama hela kila kitu basi sasa hivi kusingekuwa na nyumba za ovyo Mikocheni, Msasani, Tetegeta, Kariakoo, Ilala na prime areas zingine za bongo.

Kila mwenye nyumba tokea miaka ya 80 isiyoendana na nyumba zinazojengwa leo maeneo hayo sasa hivi ingekuwa keshahama kitambo kwa kuuza.

Uwezi kunyanyasa watu kwa sababu eneo ni prime na serikali ina miliki nyumba kwa hivyo vunja tu.

Juzi raisi Samia katoka kwenye msiba uingereza eneo alilopanda basi maeneo ya ‘Marble Arch’ mbele kidogo tu ‘Oxford Street’ sidhani kama kuna prime area duniani kama hapo (labda Tokyo) na kuna council flats zilijengwa zamani. Safari yake ya mile mbili kufika msibani mpaka Westminster njia nzima ina sehemu kuna nyumba za serikali in short ‘west end’ yote ina maeneo yana council flats ambazo ingelikuwa ni matakwa ya matajiri tu wangeshanunua zote na kuzivunja. Lakini hata kwa nchi za mabeberu it’s immoral and inhumane uwezi fanya ivyo.

Na ndio sera inayofanya watu matajiri watafute maeneo mengine ya kuendeleza na kutengeneza future prime areas.

Ni hivi huyu Nehemia hana uwezo na nafasi anayopewa hapo NHC alianza Tibaijuka kumfunga speed governor alizuia huu mpango alipokuwa waziri, Lukuvi nae akamfunga tena speed governor kwenye kuwapandishia kodi wapangaji kwa asilimia 200% na kumtaka aache tena kupandisha kodi ovyo (hizo zilikuwa zama za J.K) na Magufuli ndio akamtibua kabisa kwa kutaka kuendelea serikali kumpatia dhamana ya mikopo ambayo inaishia kuhudumiwa na walipa kodi badala ya miradi anayojenga.

Huyo mtu hana uwezo wa kufanya miradi ya kibiashara inayohitaji mbinu anataka vitu rahisi tu kutekelezeka.

Hiyo sera inaenda waumiza watu kwa sababu ambazo hazina msingi wa kibiashara ya shirika la umma ata kidogo.
Mkajenge nyumba zenu, mmekaa hapo miaka na miaka, acha shirika lijiendeshe kibiashara, yaani uko katika nyumba ya ghorofa moja, unazuia zisijengwe ghorofa 20 ili wapangaji wawe maradufu
 
Ushawahi ata kuusoma mkataba wa NHC au washirika la nyumba yoyote duniani kuhusu contract terminations au rules za kuachiana mikataba and the logic behind it?

Halafu issue sio watu kuishi maisha yao yote hapo, swala ni cheap business strategy.

Ukishawatoa hao watu unawapeleka wapi? Umeshaona shirika la serikali linavunja jengo lake bila ya kuwalipa watu fidia ya decorations wali ifanya na kuwatafutia wapangaji makazi mapya kwanza sambasamba na kodi zinazoendana kabla ya kuwatoa.

Hata Magomeni quarters kulikuwa na utaratibu sahihi na hizo kodi walizoweka ingekuwa bado JPM yu hai sidhani kama angeafiki.
Hebu acha mdomo mdomo, hama humo serikali inataka kufanya maendelezo, unafanya decoration, hiyo nyumba ni yako? Ulipata consent ya land lord? Quic quid......what is attached to the land is part of the land
 
Naunga mkono sera hii, kuna majengo ya serikali yaliyopo kwenye very prime area ila hali za majengo hayo ni pathetic!, hayakarabatiki, kilichobaki ni wapangaji wahamishwe, majengo yapigwe chini, vijengwe vitu vya maana vinavyoendana na eneo husika!.
Mchechu is very right!.
Usilinganishe jiji la Dar na London, Rome, Greece na Mji Mkongwe, zile ni acient cities zenye majengo ya zamani yanayohifadhiwa!, tena kusema ukweli hata kuijenga Ikulu yetu ya Chamwino kwa ramani ya Ikulu ya Magogoni ni ... tuu!, tulipaswa kujenga ultra modern structure sio ule mjengo wa Kiarabu!.
Ushamba ni kazi kwel kwel!.
Tubadilikeni jameni tuwe na foward looking atitude, tuachane na backward thinking!.

Subiria 7-11 itakapo kamilika!, hata Kenyatta Drive bado kuna takataka nyingi tuu, Mchechu ataibadili iwe kama Acapulco au Miami!.
P
Leo umetema madini
Ukweli haiwezekan nyumba za ajabu ajabu ziwepo upanga....
Kama unataka shiriki mradi au chanika panakuhusu!!!!
 
Mkuu, watu wanajitoa ufahamu tu na huenda wengine ni machawa wanatumika, hapo kuna uonevu ulio wazi ili kuwanufaisha wajanja wachache. Kuwasemea wanaoonewa siyo lazima kwamba sisi ni wapangaji kwenye hizo nyumba, wengine tunaishi kwenye nyumba zetu lakini hatupendi watu wa hali ya chini waonewe.
Huyo mtu wa hali ya chini anaishi upanga, almuntzar ?
Watu wachache weusi wameshika zile nyumba wanawakodishia wahindi kwa bei ghali huku wenyewe wakiilipa NHC hela kiduchu.
Majina ya wapangaji ni wamatumbi ila wanaoishi ni wahindi
Haya mambo yapo pia kota za urafiki sheklango
 
Hivi hii sera ya ubia ya NHC ilipelekwa kabisa kwenye baraza la mawaziri, wakailewa na kusema sawa.

Mtu ana mpango wa kwenda kuvunja majengo kadhaa kisa tu yapo prime areas na kuwatoa wapangaji sio tu hana hela ya kuendeleza yeye mwenyewe bali the immorality of it all is beyond me.

Kama hela kila kitu basi sasa hivi kusingekuwa na nyumba za ovyo Mikocheni, Msasani, Tetegeta, Kariakoo, Ilala na prime areas zingine za bongo.

Kila mwenye nyumba tokea miaka ya 80 isiyoendana na nyumba zinazojengwa leo maeneo hayo sasa hivi ingekuwa keshahama kitambo kwa kuuza.

Uwezi kunyanyasa watu kwa sababu eneo ni prime na serikali ina miliki nyumba kwa hivyo vunja tu.

Juzi raisi Samia katoka kwenye msiba uingereza eneo alilopanda basi maeneo ya ‘Marble Arch’ mbele kidogo tu ‘Oxford Street’ sidhani kama kuna prime area duniani kama hapo (labda Tokyo) na kuna council flats zilijengwa zamani. Safari yake ya mile mbili kufika msibani mpaka Westminster njia nzima ina sehemu kuna nyumba za serikali in short ‘west end’ yote ina maeneo yana council flats ambazo ingelikuwa ni matakwa ya matajiri tu wangeshanunua zote na kuzivunja. Lakini hata kwa nchi za mabeberu it’s immoral and inhumane uwezi fanya ivyo.

Na ndio sera inayofanya watu matajiri watafute maeneo mengine ya kuendeleza na kutengeneza future prime areas.

Ni hivi huyu Nehemia hana uwezo na nafasi anayopewa hapo NHC alianza Tibaijuka kumfunga speed governor alizuia huu mpango alipokuwa waziri, Lukuvi nae akamfunga tena speed governor kwenye kuwapandishia kodi wapangaji kwa asilimia 200% na kumtaka aache tena kupandisha kodi ovyo (hizo zilikuwa zama za J.K) na Magufuli ndio akamtibua kabisa kwa kutaka kuendelea serikali kumpatia dhamana ya mikopo ambayo inaishia kuhudumiwa na walipa kodi badala ya miradi anayojenga.

Huyo mtu hana uwezo wa kufanya miradi ya kibiashara inayohitaji mbinu anataka vitu rahisi tu kutekelezeka.

Hiyo sera inaenda waumiza watu kwa sababu ambazo hazina msingi wa kibiashara ya shirika la umma ata kidogo.
cjui ni mimi cjakuelewa. Umeongelea vitu vingi mpaka cjaelewa point yako ulitaka kusemaje
 
Mleta mada hauko sahihi, nahisi una maslahi binafsi.

Kuweka sawa hili, ngoja niandike machache kufafanua.

1. Hatuwezi kuwapangia nini cha kufanya NHC kwenye nyumba wanazozimiliki. Lolote watakaloliamua ni haki yao, kwa kuwa nyumba ni zao.
Naunga mkono hoja!.
2. Hakuna upangaji wa kudumu au milele kwenye nyumba za NHC. Mpangaji yoyote anaweza kuondolewa mkataba wake ukiisha. Shirika litakupa notice ya miezi mitatu kabla ya mkataba wako kwisha kuwa uondoke, baada ya hapo utajua utakapokwenda, na shirika haliwajibiki.
Nauga mkono hoja na hii ndio sheria ya upangaji.
3. Unapopangishwa ndani ya nyumba za NHC kisheria hupaswi kuendeleza, kukarabati au kuboresha chochote. Mambo hayo ni jukumu la shirika sio la kwako, na ikitokea umefanya hayo kwa nia njema kabisa hiyo itakuwa ni hisani (hupaswi kudai kufidiwa chochote)
Naunga mkono hoja, na mkataba unakutaka kabla hujafanya maboresho yoyote, you have to inform the land lord for consent in writings, na siku ukihama ni ama uache kila kitu ulichoboresha, ama ubomoe maboresho yako na kuiresha nyumba kama ulivyoikuta!. Ukijiboreshea ni wewe na haulipwi chochote!.
otherwise uwe na mapatano ya kisheria katika hilo na NHC. Na ikiwa sheria/mkataba utakiukwa ni vyema kukimbilia mahakamani kupinga.
Hapa ndipo hii sera mpya ya ubia ilipoingia!
4. Sehemu kubwa ya wapangaji wa asili kwenye nyumba za NHC (nyingi zikiwa Prime area) ni kama wanakaa bure, kodi wanayolipishwa ni ndogo mnoo kuliko kodi ya kupangishwa mitaa ya uswahili tena nyumba iliyochoka vibaya sana. Na kwa hali hiyo hakuna mpangaji wa NHC ambaye yuko tayari kutoka kwenye nyumba za NHC kirahisi.
True
5. NHC ilishabadilisha sera zake kutoka kwenye ujamaa (umaskini, huduma, hisani, umma) na kuingia kwenye ubebari (soko, ushindani, biashara, faida), hivyo ni lazima wawe na nyumba za kisasa na mwenye nguvu ya pesa ndio akae kwenye nyumba zake. Hayo yalifanyika ili NHC iweze kufufuka baada ya kuwa imeshakufa!
True
7. Suala la NHC kuwekeza kwa ubia au kibebari haliwezi kuepukika kwa sasa, ndio dunia ya real estate ilipofikia. Japokuwa katika uwekezaji huo kuna upigaji wa kutisha, suluhisho sio kuzuia ubebari au ubia wa uwekezaji, suluhisho ni kuwa na uwazi na umakini katika uwekezaji huo.
Naunga mkono hoja.
P
 
Kwamba pakishajengwa hayo majengo ya kisasa, hao wenyeji watapata uwezo wa kukaa hizo prime area na sio wageni tena!? Bila shaka unaota, ukiamka utakutana na reality. Naomba tu usifie usingizini.
Kama tu ghorofa za Magufuli pale usalama wenyeji wameanza kuambiw mara sijui hawaendani na hadhi ya jengo. Mara sijui wanachafua jengo na figisu za aina hio sitoshangaa humo mjini wakiondolewa kibabe bila fidia.
 
Mleta mada,

Nimejaribu kupitia andiko lako kuhusu sera ya ubia ya NHC na nia ya kuwaondoa wakazi ambao kimsingi ni wapangaji kwenye maeneo yote ambayo ni prime na kisha kujenga maghorofa ili kuendana sio tu na mahitaji ya sasa ya mipango miji, bali pia kukidhi mahitaji ya makazi hususani mijini.

Pamoja na umakini wa kusoma andiko lako, bado sijapata kuona logic yoyote ile zaidi ya majungu na kulialia.

Nimeona kwanza unapendekeza wakazi walipwe fidia! Hivi utakuwa unafahamu kwamba kwenye mikataba ya upangishaji, standard lease agreement yoyote ile, kuna kifungu kipo very clear kinachosema Landlord akihitaji nyumba yake kwa matumizi yoyote anayojua yeye, atatoa notisi tu ya mwezi au miezi mitatu na so called "Mpangaji" anafungasha virago?

Just because wapangaji wa NHC wanekaa kwenye hizo nyumba for over 40 years does not make them the owners wa kuwa eligible kulipwa fidia! Hili liondoe kabisa kichwani kwako.

Halafu huu mjadala wako, ukiachana na mambo mwngine yote, umejaa ubinafsi ndani yake. Nitaeleza kwanini, haiwezekani kuwepo na kijengo uchwara mjini ambacho kinaweza ku-accomodate watu 6, mbaya zaidi hata thamani ya ardhi inakuwa imezidi maendelezo yaliyopo juu, halafu bado unataka Shirika liendelee kung'ang'ania hicho kijengo kisa tu England wanafanya hivyo!? Huu ni ubinafsi usio wa kawaida na roho mbaya ndani yake ya kutotaka Wananchi wengi zaidi wasipate fursa ya kuishi mijini!

Faida za kubomoa vijengo uchwara na kutafuta ubia kisha kuendelea kwa kujenga ghorofa nyingi zaidi sio tu kutaongeza mapato kwa Shirika, lakini pia kutafanya maendelezo kuendana na thamani halisi ya ardhi wakati huo huo kuwapata fursa Wananchi wengi zaidi na familia nyingi zaidi kuishi "Downtown".

Hivyo mleta mada nikuombe sana usiwe kizabizabina wa kukataa maendeleo kwa chuki zako binafsi dhidi ya huyo sijui Mchechu. Mimi binafsi I'm not the fun of him, but kwenye hili lazima tumuunge mkono kwa kuwa litaleta faida kubwa kwa Nchi.

It's about time wapenda mserereko wanaojiita wapangaji wa kudumu wa NHC wote waliopo "downtown" na wao wakaishi Madale kwa kupenda au kutokupenda, au kama hawataki basi wapange nyumba kwa developers wengine hapo hapo downtown. Ila ni lazima wapishe NHC ifanye what's necessary.
 
Kama tu ghorofa za Magufuli pale usalama wenyeji wameanza kuambiw mara sijui hawaendani na hadhi ya jengo. Mara sijui wanachafua jengo na figisu za aina hio sitoshangaa humo mjini wakiondolewa kibabe bila fidia.
Wapangaji wafidie kwa sababu gani?
Yaani mpangaji muda wa kukaa umekwisha, mwenye nyumba ameamua kubadili muundo wa nyumba yake na biashara zake, wewe mpangaji uliyekuwa umepangishwa hapo awali uje udai kufidiwa, ufidiwe nini?
 
Mleta mada hauko sahihi, nahisi una maslahi binafsi.

Kuweka sawa hili, ngoja niandike machache kufafanua.

1. Hatuwezi kuwapangia nini cha kufanya NHC kwenye nyumba wanazozimiliki. Lolote watakaloliamua ni haki yao, kwa kuwa nyumba ni zao.

2. Hakuna upangaji wa kudumu au milele kwenye nyumba za NHC. Mpangaji yoyote anaweza kuondolewa mkataba wake ukiisha. Shirika litakupa notice ya miezi mitatu kabla ya mkataba wako kwisha kuwa uondoke, baada ya hapo utajua utakapokwenda, na shirika haliwajibiki.

3. Unapopangishwa ndani ya nyumba za NHC kisheria hupaswi kuendeleza, kukarabati au kuboresha chochote. Mambo hayo ni jukumu la shirika sio la kwako, na ikitokea umefanya hayo kwa nia njema kabisa hiyo itakuwa ni hisani (hupaswi kudai kufidiwa chochote) otherwise uwe na mapatano ya kisheria katika hilo na NHC. Na ikiwa sheria/mkataba utakiukwa ni vyema kukimbilia mahakamani kupinga.

4. Sehemu kubwa ya wapangaji wa asili kwenye nyumba za NHC (nyingi zikiwa Prime area) ni kama wanakaa bure, kodi wanayolipishwa ni ndogo mnoo kuliko kodi ya kupangishwa mitaa ya uswahili tena nyumba iliyochoka vibaya sana. Na kwa hali hiyo hakuna mpangaji wa NHC ambaye yuko tayari kutoka kwenye nyumba za NHC kirahisi.

5. NHC ilishabadilisha sera zake kutoka kwenye ujamaa (umaskini, huduma, hisani, umma) na kuingia kwenye ubebari (soko, ushindani, biashara, faida), hivyo ni lazima wawe na nyumba za kisasa na mwenye nguvu ya pesa ndio akae kwenye nyumba zake. Hayo yalifanyika ili NHC iweze kufufuka baada ya kuwa imeshakufa!

6. Pamoja na ufisadi mwingi, makando makando mengi ya Mchechu, lakini kiukweli ndio mtu aliyeweza kuinua upya NHC kuwa ya kisasa na kuweza kuwekeza kibebari. Yule jamaa ni mwizi kweli lakini ni mwamba haswaa.

7. Suala la NHC kuwekeza kwa ubia au kibebari haliwezi kuepukika kwa sasa, ndio dunia ya real estate ilipofikia. Japokuwa katika uwekezaji huo kuna upigaji wa kutisha, suluhisho sio kuzuia ubebari au ubia wa uwekezaji, suluhisho ni kuwa na uwazi na umakini katika uwekezaji huo.
Mkuu nakuunga mkono kwa hoja zako zote ulizowasilisha hapa. Ni matumaini yetu kwamba itafafanua kwa watu wachache hapa ambao kwa namna moja ama nyingine wamepotoshwa na mleta mada.

Labda kwa kuongezea, mabadiliko ya NHC kutoka kwenye ujamaa na kufanya kazi kibiashara yakifanywa kisheria kwanza kwa Serikali kuondoa sheria ya Rent Restriction Act mwaka 2005 na kuipa uhuru NHC kutoa kodi ya pango kwa kuangalia hali ya soko. Kuanzia hapo NHC ilitakiwa kisheria kufanya kazi kibiashara.

Hivyo utawezaje kufanya kazi kiabishara ukiwa na vijengo uchwara kwenye maeneo ambayo yana command highest rental charges in the country!? Lazima tu ukubali kubadilika kwa kujenga majengo ya kisasa na kama huna mtaji basi unawaalika wabia wenye mitaji ili kufikia lengo.
 
Wapangaji wafidie kwa sababu gani?
Yaani mpangaji muda wa kukaa umekwisha, mwenye nyumba ameamua kubadili muundo wa nyumba yake na biashara zake, wewe mpangaji uliyekuwa umepangishwa hapo awali uje udai kufidiwa, ufidiwe nini?
Si nyumba zao zilivunjwa ili kujenga hayo maghorofa
 
Mleta mada,

Nimejaribu kupitia andiko lako kuhusu sera ya ubia ya NHC na nia ya kuwaondoa wakazi ambao kimsingi ni wapangaji kwenye maeneo yote ambayo ni prime na kisha kujenga maghorofa ili kuendana sio tu na mahitaji ya sasa ya mipango miji, bali pia kukidhi mahitaji ya makazi hususani mijini.

Pamoja na umakini wa kusoma andiko lako, bado sijapata kuona logic yoyote ile zaidi ya majungu na kulialia.

Nimeona kwanza unapendekeza wakazi walipwe fidia! Hivi utakuwa unafahamu kwamba kwenye mikataba ya upangishaji, standard lease agreement yoyote ile, kuna kifungu kipo very clear kinachosema Landlord akihitaji nyumba yake kwa matumizi yoyote anayojua yeye, atatoa notisi tu ya mwezi au miezi mitatu na so called "Mpangaji" anafungasha virago?

Just because wapangaji wa NHC wanekaa kwenye hizo nyumba for over 40 years does not make them the owners wa kuwa eligible kulipwa fidia! Hili liondoe kabisa kichwani kwako.

Halafu huu mjadala wako, ukiachana na mambo mwngine yote, umejaa ubinafsi ndani yake. Nitaeleza kwanini, haiwezekani kuwepo na kijengo uchwara mjini ambacho kinaweza ku-accomodate watu 6, mbaya zaidi hata thamani ya ardhi inakuwa imezidi maendelezo yaliyopo juu, halafu bado unataka Shirika liendelee kung'ang'ania hicho kijengo kisa tu England wanafanya hivyo!? Huu ni ubinafsi usio wa kawaida na roho mbaya ndani yake ya kutotaka Wananchi wengi zaidi wasipate fursa ya kuishi mijini!

Faida za kubomoa vijengo uchwara na kutafuta ubia kisha kuendelea kwa kujenga ghorofa nyingi zaidi sio tu kutaongeza mapato kwa Shirika, lakini pia kutafanya maendelezo kuendana na thamani halisi ya ardhi wakati huo huo kuwapata fursa Wananchi wengi zaidi na familia nyingi zaidi kuishi "Downtown".

Hivyo mleta mada nikuombe sana usiwe kizabizabina wa kukataa maendeleo kwa chuki zako binafsi dhidi ya huyo sijui Mchechu. Mimi binafsi I'm not the fun of him, but kwenye hili lazima tumuunge mkono kwa kuwa litaleta faida kubwa kwa Nchi.

It's about time wapenda mserereko wanaojiita wapangaji wa kudumu wa NHC wote waliopo "downtown" na wao wakaishi Madale kwa kupenda au kutokupenda, au kama hawataki basi wapange nyumba kwa developers wengine hapo hapo downtown. Ila ni lazima wapishe NHC ifanye what's necessary.
Ipo siku watu kama nyie mtasema polisi iache kuangaika na panya road uswazi kwa hoja za kwamba kwanza ni watoto waliokulia huko huko kwa ivyo ni matatizo ya malezi ya ovyo huko wacha yawakute.

Halafu hayo maeneo yenu nyumba zenu zinawalinzi wa private security companies wenye miguu ya kuku tena mnawalipa kwa mishahara inayotokana na kodi hizo hizo za hao wa uswazi mnaodai panya road ni tatizo la malezi yao sio serikali.

That’s how cheap hoja zako zilivyo

Hakuna serikali makini itakayo kubali aina ya ubia NHC inayotaka kufanya duniani na wala si business model ya shirika lolote la nyumba duniani, na uwezi kuweka mfano wa mtu mwingine yeyote aliefanya icho kitu duniani.

People do regenerations ya maeneo, majengo and sometimes entire cities, nonetheless responsibly.

Ni hivi hilo jambo sio rahisi morally ndio maana hakuna serikali yoyote itakayo support aina hiyo ya ufanyaji biashara labda serikali ya Tanzania tu.

Hakuna shida kubomoa baadhi ya nyumba lakini hekima ni kuwatafutia wapangaji sehemu kwanza, ivyo ndivyo watu wanafanya mambo dunia ya leo ata kama hayo sio matakwa ya sheria za nchi au mkataba; but it’s canon law today unapobomoa nyumba.

Only in 1920’s watu walikuwa wanaweza fanya hayo mambo ila kwa ethics demands.za leo ata hizo central control economies kama China awawezi fanya ivyo; it’s just immoral.
 
Si nyumba zao zilivunjwa ili kujenga hayo maghorofa
Namaanisha wapangaji wa NHC iweje wadai kulipwa fidia baada ya nyumba walizokuwa wamepangishiwa kuvunjwa baada ya mikataba yao kwisha?

Wale wakazi wa Magomeni kota, zile nyumba zilikuwa ni mali yao kwa 100%, walipovunjiwa nyumba zao kisheria, patano lao na serikali ilikuwa kulipwa fidia ya kukaa kwenye yale majengo. Hilo sina tatizo nalo.
 
Hivi hii sera ya ubia ya NHC ilipelekwa kabisa kwenye baraza la mawaziri, wakailewa na kusema sawa.

Mtu ana mpango wa kwenda kuvunja majengo kadhaa kisa tu yapo prime areas na kuwatoa wapangaji sio tu hana hela ya kuendeleza yeye mwenyewe bali the immorality of it all is beyond me.

Kama hela kila kitu basi sasa hivi kusingekuwa na nyumba za ovyo Mikocheni, Msasani, Tetegeta, Kariakoo, Ilala na prime areas zingine za bongo.

Kila mwenye nyumba tokea miaka ya 80 isiyoendana na nyumba zinazojengwa leo maeneo hayo sasa hivi ingekuwa keshahama kitambo kwa kuuza.

Uwezi kunyanyasa watu kwa sababu eneo ni prime na serikali ina miliki nyumba kwa hivyo vunja tu.

Juzi raisi Samia katoka kwenye msiba uingereza eneo alilopanda basi maeneo ya ‘Marble Arch’ mbele kidogo tu ‘Oxford Street’ sidhani kama kuna prime area duniani kama hapo (labda Tokyo) na kuna council flats zilijengwa zamani. Safari yake ya mile mbili kufika msibani mpaka Westminster njia nzima ina sehemu kuna nyumba za serikali in short ‘west end’ yote ina maeneo yana council flats ambazo ingelikuwa ni matakwa ya matajiri tu wangeshanunua zote na kuzivunja. Lakini hata kwa nchi za mabeberu it’s immoral and inhumane uwezi fanya ivyo.

Na ndio sera inayofanya watu matajiri watafute maeneo mengine ya kuendeleza na kutengeneza future prime areas.

Ni hivi huyu Nehemia hana uwezo na nafasi anayopewa hapo NHC alianza Tibaijuka kumfunga speed governor alizuia huu mpango alipokuwa waziri, Lukuvi nae akamfunga tena speed governor kwenye kuwapandishia kodi wapangaji kwa asilimia 200% na kumtaka aache tena kupandisha kodi ovyo (hizo zilikuwa zama za J.K) na Magufuli ndio akamtibua kabisa kwa kutaka kuendelea serikali kumpatia dhamana ya mikopo ambayo inaishia kuhudumiwa na walipa kodi badala ya miradi anayojenga.

Huyo mtu hana uwezo wa kufanya miradi ya kibiashara inayohitaji mbinu anataka vitu rahisi tu kutekelezeka.

Hiyo sera inaenda waumiza watu kwa sababu ambazo hazina msingi wa kibiashara ya shirika la umma ata kidogo.
mkuu ufisadi una sura nyingi sana.
 
Back
Top Bottom