Mkuu Erythrocyte naomba kujua mambo kadhaa kwenye hii logo tafadhali
Kwanza kabisa wachangiaji wengi wameipenda Kwa sababu ya mwonekano wake wa 3D(MOCK UP),lakni ukiondoa huu mwonekano wa mock up ukaiacha ktk mwonekano wake halisi inabaki kuwa logo ya kawaida sn..
Lkn pia hii mock up imefanana Kwa ukaribu sn na logo ya Toyota pia kidogo na logo ya kampuni ya mafuta ya Total
Na tukumbuke katika logo yoyote Ile kila unachokiweka lazima kilete maana na kubeba ujumbe wa hiyo logo husika.Kwa hiyo swali langu mkuu ni kwamba Mimi Kama mtanzania nataka kufahamu maana ya hiyo logo
Note:
sina tatizo na maana ya neno 'CHADEMA DIGITAL wala rangi zake Ambazo ndy identity ya chadema (Branding colours )
Ila nataka kujua maana ya hiyo michoro mitatu iliyojinyongorota km sifuri isiyoungana au duara lisilokamilika' mlikusudia kutuletea ujumbe gani
Vinginevyo ni logo ya kawaida sn na ni 80%-90%
C&P ya logo ya Toyota (pragrialism) na designer hapaswi kupewa kazi kubwa Kama hizi