Neno gani ambalo ulishawahi kuambiwa dhahiri likakukatisha tamaa?

Neno gani ambalo ulishawahi kuambiwa dhahiri likakukatisha tamaa?

Ukweli ni kwamba kuna maneno mengi sana ambayo yanatumika na watu mbalimbali hususani pale wanapotaka kumkatisha tamaa mtu mwingine.

Binafsi, kuna neno "Sio kirahisi hivyo kama unavyodhani" Hili ni neno ambalo limeachisha mawazo ya watu wengi kuhusiana na kujihusisha na jambo fulani.

Mfano, unaweza kuwa umefikiria kuanzisha biashara katika eneo fulani, lakini watu wengi watasema kuwa "kwa hilo eneo sio rahisi kama unavyofikiria kufanya biashara hiyo" Lakini ukweli ni kwamba endapo utalianza jambo hilo utagundua sio kama lilivyokuwa likizungumziwa awali kwa maana linaweza kuonekana jepesi zaidi.

Je! Ni neno gani lingine mwana Jamii Forum umewahi kulisikia au kuambiwa ambalo dhahiri lilikurudisha nyuma katika kutekeleza jambo lako?

Hamza Nsiha ~
Sina hisia hisia na wewe
 
Kuna mbuzi mmoja binti alinikataa baada ya form six kwa sababu yeye amepata Admission ya UDSM, mimi nimepata vyuo vya “Tanganyika”.

Baada ya kuhitimu UDSM maisha yamemchapa akanitafuta akiniuliza vipi huko bado nahitaji tuwe wote! Nilichomjibu simply “endelea na vijana wa mjini achana na mimi mkulima wa mkoani”[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Mama huyu mtoto wa kaka yako angekuwa msichana ,sasa hivi angekuwa amesha kuzalia wajukuu wangapi?[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mama mtu akajibu kama wawili hivi!!dah,, yaani kwa lugha nyingine ninge kuwa malaya nagawa uroda [emoji56][emoji56] hayo yote kwa kuwa nime kwama life ina nichapa na nina wategemea wao
 
Kuna mwaka mzee wangu alifariki sasa kuna ishu nikawa nafuatilia kwenye ofisi moja ya serikali nikaambiwa nikamuone boss mmoja nakumbuka jina lake ni shirima....alichonijibu yule mzee sintosahau japo ni more than 20 years ago. Na nilishamlaani sintomsamehe..nilitamani nikajiunge alshabaab nirudi kumuonesha show kwa kauli ile ya kudharau kifo cha mzee wangu na kunifukuza kama mbwa. Ukizingatia jinsi tulivyomuuguza mzee kwa mda mrefu na alivyoteseka. Siku hiyo nilirudi home maza akaniuliza feedback sikumjibu nikaenda kwanza kujifungia geto...badae nikamwambia tu maza ningekua na uwezo wa kupata bunduki leo ningetafuta...na hapo nilikua o level tu. Sometimes nikiona madogo wameingia kwenye makundi ya kigaidi siwalaumu sana. Life pushes them to the limit na hawaoni option sababu kila mtu kama kawatenga
Pole sana!
 
"Hivi nelly ukipaangalia kwenu na kwetu unaweza kuwa na girl kama mimi"

Ilipelekea nika-fail mtihani muhimu sana shule ila mungu sio massawe demu ameolewa ila mimi ndio kama mume vile.


Kuna siku aliwahi kuniambia ile kauli anaijutia sanaa hata kama nilishamsamehe na kuahidi kunipenda mpaka kufa
'Usitamani mke wa mtu'.
 
Nilikuwa nasoma FTC wakati huo, halafu kuna jirani yetu home, yeye alikuwa anasoma pale chuo cha ardhi Dar. Sasa wakati wa likizo tukakutana kitaa, mwana alikuwa third year pale ardhi na mimi ndo first year. Si akaniuliza nasoma kupata leve gani pale chuo ninaposoma. Nikamjibu FTC..!! AKANIAMBIA DAH..!! WATU SAA HII WANASOMA ADVANCED DIPLOMA NA DEGREE WEWE UNANGÁNGÁNA NA FTC..!! Aisee, alinipa hasira. Nikapambana mpaka nikamaliza FTC na kuingia FoE na kufanikiwa kupata BSc in Eng.

Wakati mwingine maneno makali tunayoambiwa na wanaotuzunguka, yanatutia nguvu ya kusonga, kwa maana ya kuwa-pruvu wrong walioyatamka
Hongera kwako!
Kwa ujumla hili ni fundisho, haijalishi unaanzia wapi au kwa namba gani, je lengo lako ni kufika wapi?
Inawezekana hukuwa na mtazamo wowote wakati huo, bali ulijiunga ili Uwe shule. Hivyo jamaa kakufungua macho.
Kuna watoto muda huu, hawajui nini cha kufanya kitaaluma, uliyopitia yatafungua macho wengi ambap kwa njia moja au nyingine hawakupitia hatua zilizo wazi za kielimu.
Kuwa waweza kuchukua masomo ya Cheti cha ufundi FTC, ukaenda Diploma, hadi ukajiunga na Faculty of Engineering chuo kikuu ukapata, shahada ya kwanza, ya pili na kuendelea.
 
Mama huyu mtoto wa kaka yako angekuwa msichana ,sasa hivi angekuwa amesha kuzalia wajukuu wangapi?[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Mama mtu akajibu kama wawili hivi!!dah,, yaani kwa lugha nyingine ninge kuwa malaya nagawa uroda [emoji56][emoji56] hayo yote kwa kuwa nime kwama life ina nichapa na nina wategemea wao
Pole! Pambana!
 
Mjomba aliniambia masuala ya computer programming yanahitaji aina fulani ya wenye akili na kwamba mimi simo baina yao kwamba siwezi, nitafute shughuli nyepesi.....leo mimi developer mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka kumi napiga codes hadi basi na kuachia systems......usikatishwe tamaa na yeyote, pambana.
 
Ukweli ni kwamba kuna maneno mengi sana ambayo yanatumika na watu mbalimbali hususani pale wanapotaka kumkatisha tamaa mtu mwingine.

Binafsi, kuna neno "Sio kirahisi hivyo kama unavyodhani" Hili ni neno ambalo limeachisha mawazo ya watu wengi kuhusiana na kujihusisha na jambo fulani.

Mfano, unaweza kuwa umefikiria kuanzisha biashara katika eneo fulani, lakini watu wengi watasema kuwa "kwa hilo eneo sio rahisi kama unavyofikiria kufanya biashara hiyo" Lakini ukweli ni kwamba endapo utalianza jambo hilo utagundua sio kama lilivyokuwa likizungumziwa awali kwa maana linaweza kuonekana jepesi zaidi.

Je! Ni neno gani lingine mwana Jamii Forum umewahi kulisikia au kuambiwa ambalo dhahiri lilikurudisha nyuma katika kutekeleza jambo lako?

Hamza Nsiha ~
Neno "Sio kirahisi kihivyo kama unavyodhani" nimeambiwa last month..!!
 
Kuna mwaka mzee wangu alifariki sasa kuna ishu nikawa nafuatilia kwenye ofisi moja ya serikali nikaambiwa nikamuone boss mmoja nakumbuka jina lake ni shirima....alichonijibu yule mzee sintosahau japo ni more than 20 years ago. Na nilishamlaani sintomsamehe..nilitamani nikajiunge alshabaab nirudi kumuonesha show kwa kauli ile ya kudharau kifo cha mzee wangu na kunifukuza kama mbwa. Ukizingatia jinsi tulivyomuuguza mzee kwa mda mrefu na alivyoteseka. Siku hiyo nilirudi home maza akaniuliza feedback sikumjibu nikaenda kwanza kujifungia geto...badae nikamwambia tu maza ningekua na uwezo wa kupata bunduki leo ningetafuta...na hapo nilikua o level tu. Sometimes nikiona madogo wameingia kwenye makundi ya kigaidi siwalaumu sana. Life pushes them to the limit na hawaoni option sababu kila mtu kama kawatenga
Umeeleza mengi mno halafu hujafanya uzi ulichokusudia. Issue ni useme maneno yaliyokukatisha tamaa. Sio porojo nyiiingi halafu unaishia kutoka nje ya mada
 
Miaka hiyo GLF wangu kabla ya kulana alikuja getto kafika chumba kilikuwa kidogo sana so nikawa nina sweat akaniambia " UNATIA HURUMA NIKIKUKUPA WEWE SI UTAKUFA KAMA UMEONA CHUPI TU UNATOKA MAJASHO" Huwezi amini ile siku iliniuma sana ikabidi nihame nitafute chumba kizuri next time alivyo kuja ndo mwisho wa maneno yake ya kebehii na dharauu alinipenda mpaka leo ameolewa ila bado yupo na mimi na anaomba sana nikamchakate.
 
Utaniharibia watoto...... mwanaume mbaya wewe...... Mvuto huna ukiondoa hivo vipesa vyako huna kingine cha kuringia.......
😅😅😆 wanawake bhana akija kwa social media wanajidai black men tall mgumu mgumu ni amazing....hahahah
 
Back
Top Bottom