Neno gani ambalo ulishawahi kuambiwa dhahiri likakukatisha tamaa?

Neno gani ambalo ulishawahi kuambiwa dhahiri likakukatisha tamaa?

Kuna kazi ya online nilikuwa naifanya, nina shoot short video namtumia client alafu nalipwa, sasa my GF akaniona, yeye akahisi kama ni upuuzi au nafanya comedy za TikTok tu kumbe mi nimetega mingo ya kupiga kama dollar 10 ivi chap chap.

Aliniambia kauli moja tu "UKIKUA UTAACHA", lile neno linanikera mpaka leo hii na baada ya hapo nilimuapia mbele yake hawezi jua ninafanya kazi gani, as long as anacho kitaka anapewa basi asitake kujua mishe zangu na hata akitaka hato kaa asikie nikimuambia kamwe.
Wakati huo ukiwa na age ipi?
 
Wewe kufanikiwa hutaweza, halafu imagine ni mtu wako wa karibu sana


Halafu nimeamini saa nyingine chuki huja kwa njia ya utani
Ongezea na 'mazoea mazoea' ya kipuuzi. Hata uongozi, huwezi heshimika ukiwa mtu wa utani utani na mazoea, utaishia kupata kura moja au mbili tu
 
Ukweli ni kwamba kuna maneno mengi sana ambayo yanatumika na watu mbalimbali hususani pale wanapotaka kumkatisha tamaa mtu mwingine.

Binafsi, kuna neno "Sio kirahisi hivyo kama unavyodhani" Hili ni neno ambalo limeachisha mawazo ya watu wengi kuhusiana na kujihusisha na jambo fulani.

Mfano, unaweza kuwa umefikiria kuanzisha biashara katika eneo fulani, lakini watu wengi watasema kuwa "kwa hilo eneo sio rahisi kama unavyofikiria kufanya biashara hiyo" Lakini ukweli ni kwamba endapo utalianza jambo hilo utagundua sio kama lilivyokuwa likizungumziwa awali kwa maana linaweza kuonekana jepesi zaidi.

Je! Ni neno gani lingine mwana Jamii Forum umewahi kulisikia au kuambiwa ambalo dhahiri lilikurudisha nyuma katika kutekeleza jambo lako?

Hamza Nsiha ~
Nilienda ofisi moja enzi hizo nafuga Afro na midevu km yote, niliitwa kwenye interview ila kabla interview nikatambulishwa kwa boss ambae hata chembe ya unywele in short kanyoa upara na ndevu zote kanyoa, aisee alichoniambia niliduwaa aliniambia 'kijana hapa hatuajiri maustaadhi wala marasta man hivyo nenda kanyoe hayo manywele yako yote na hio midevu pia nyoa ndio uje hapa tukufanyie interview', mdogo mdogo nikaondoka Mpaka saloon nikanyofoa nywele zote na udevu wote, niliporudi cha ajabu baada ya interview nikapigwa chini pain
 
Ongezea na 'mazoea mazoea' ya kipuuzi. Hata uongozi, huwezi heshimika ukiwa mtu wa utani utani na mazoea, utaishia kupata kura moja au mbili tu
Kweli kabisa, naunga mkono hii hoja
 
Kuna mbuzi mmoja binti alinikataa baada ya form six kwa sababu yeye amepata Admission ya UDSM, mimi nimepata vyuo vya “Tanganyika”.

Baada ya kuhitimu UDSM maisha yamemchapa akanitafuta akiniuliza vipi huko bado nahitaji tuwe wote! Nilichomjibu simply “endelea na vijana wa mjini achana na mimi mkulima wa mkoani”[emoji2][emoji2][emoji2]
Duuuh! Na maisha yalimchapa hasa au siyo?
 
nilikua najiendeleza nasoma chuo kimya kimya huku nafanyakaz, baada ya mwaka kazin watu wakajua kuwa ninajiendeleza, basi wakanidodosa wakajua nasoma course gani, walinicheka sana wakasema mimi kilaza hiyo course nitafeli 😂 na kweli course ilikua na baadhi ya masomo kama matatu yananipiga chenga... Basi walivyo ona mimi nimeanza kusoma kilamtu akaanza kusema ikifika mwakani lazima asome, kuna mfanyakaz mwenzangu alikua anajiona yeye ndio yeye mtaalam wa kilakitu alikua anawaambia watu kwamba mimi nitafeli kwasabab hio course siiwez sina msingi mzuri kuliko yeye mtaalam, next year kweli akasoma the same course niliyosoma mimi na chuo hicho nilichosoma, after 2yrs ilitakiwa a graduate tukashangaa anaanza kusema Supervisor wake amemlostisha kwenye Research kwahio hadi mwakani 😂 kunasiku tupo ofisini ni jamaa fulani wambea sana walikua wanapekua majina ya watu Google wakapekua langu wakaona Research yangu imepandishwa ktk website ya chuo na kwamba nime graduate... Huku na huku wakam Google na jamaa eeeenh si wakakuta chuo wameorodhesha majina ya watu walio Disco jamaa jina lake lipo 😂 aiseee nilicheka sana. Ila nikawaambia washikaj mkaushieni msimtangaze jamaa kwamba ameDisco 😂 wakasema poa baada ya wiki tu umbea uliwashinda kuvumilia wakawaambia watu waingie kwenye website ya chuo waone jamaa alivyo disco... From there kilamtu alianza kuniheshim maana walidhani sija graduate. Yule jamaa alikonda kwa stress baada ya siri yake kuvuja hadi leo ananionea aibu bahat nzuri nilihama kazi nikapata nyingine nzuri zaid
Chai,hakuna chuo kinapublish watu waliodisco
 
Chai,hakuna chuo kinapublish watu waliodisco
Wee mtoto niheshimu nimezaa na mama yako usidhani humu kilamtu ni mtoto mwenzako... Hushangai zaman NECTA walikua wanatoa matokeo na majina ya watu, lakin sikuhiz nyie mnamaliza form4/6 wanatoa namba zenu tu badala ya jina..? Nimesoma chuo wew ukiwa unachambwa na house girl ndio maana hujui lolote... Next time jifunze kuhoji kiustarabu ujibiwe kistaarabu
 
Wee mtoto niheshimu nimezaa na mama yako usidhani humu kilamtu ni mtoto mwenzako... Hushangai zaman NECTA walikua wanatoa matokeo na majina ya watu, lakin sikuhiz nyie mnamaliza form4/6 wanatoa namba zenu tu badala ya jina..? Nimesoma chuo wew ukiwa unachambwa na house girl ndio maana hujui lolote... Next time jifunze kuhoji kiustarabu ujibiwe kistaarabu
Pumbavu mzee mzima eti umesoma zamani ila unaandika grammar mbovu kuliko hata house girl wangu.h iyo zamani unayosema majibu yalikuwa kwenye google ni zamani ipi,unajua google imeanza lini,na vyuo vimeanza lini kutumia mitandaokupost matokeo,eti nimesoma zanani,wadabganye wajinga sio mimi,ndio maana kazini kwako walikuona kiazi usikute ni standard seven tu wewe
 
Ukweli ni kwamba kuna maneno mengi sana ambayo yanatumika na watu mbalimbali hususani pale wanapotaka kumkatisha tamaa mtu mwingine.

Binafsi, kuna neno "Sio kirahisi hivyo kama unavyodhani" Hili ni neno ambalo limeachisha mawazo ya watu wengi kuhusiana na kujihusisha na jambo fulani.

Mfano, unaweza kuwa umefikiria kuanzisha biashara katika eneo fulani, lakini watu wengi watasema kuwa "kwa hilo eneo sio rahisi kama unavyofikiria kufanya biashara hiyo" Lakini ukweli ni kwamba endapo utalianza jambo hilo utagundua sio kama lilivyokuwa likizungumziwa awali kwa maana linaweza kuonekana jepesi zaidi.

Je! Ni neno gani lingine mwana Jamii Forum umewahi kulisikia au kuambiwa ambalo dhahiri lilikurudisha nyuma katika kutekeleza jambo lako?

Hamza Nsiha ~
Boss mmoja aliniambia "Chura hufiki mbali" .......
 
Nilienda ofisi moja enzi hizo nafuga Afro na midevu km yote, niliitwa kwenye interview ila kabla interview nikatambulishwa kwa boss ambae hata chembe ya unywele in short kanyoa upara na ndevu zote kanyoa, aisee alichoniambia niliduwaa aliniambia 'kijana hapa hatuajiri maustaadhi wala marasta man hivyo nenda kanyoe hayo manywele yako yote na hio midevu pia nyoa ndio uje hapa tukufanyie interview', mdogo mdogo nikaondoka Mpaka saloon nikanyofoa nywele zote na udevu wote, niliporudi cha ajabu baada ya interview nikapigwa chini pain
Kama mwenzio master J
 
Back
Top Bottom