Netumbo Nandi-Ndaitwah aweka Historia, awa Rais wa kwanza mwanamke wa Namibia

Netumbo Nandi-Ndaitwah aweka Historia, awa Rais wa kwanza mwanamke wa Namibia

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Netumbo Nandi-Ndaitwah wa chama tawala cha Swapo nchini Namibia amechaguliwa kuwa Rais, na hivyo kuwa kiongozi wa kwanza mwanamke nchini humo.

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la Afrika Kusini (SABC), matokeo yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi ya Namibia leo Jumanne Desemba 3, 2024 yameonyesha kuwa Swapo imepata kura 583,300, huku chama kikuu cha upinzani, Independent Patriots for Change (IPC), kikishika nafasi ya pili kwa kura 220, 809.

IMG_1228.jpeg

Kura hizo zimeiwezesha Swapo kupata viti 51 katika Bunge la Kitaifa, na IPC viti 20. Nandi-Ndaitwah mwenye umri wa miaka 72, amekuwa Makamu wa Rais tangu Februari 2024.

Mwaka 2017, alikua Makamu wa Rais wa kwanza mwanamke kupitia Swapo.

Namibia sasa itafuata nyayo za Tanzania kwa kuwa na Rais mwanamke Afrika, huku pia ikiungana na Mexico inayoongozwa na Rais Claudia Sheinbaum.
 
Watu wetu wasivyo na akili wataona hii ni agenda kwao kumbe Namibia na sisi ni tofauti kabisa mchi ile ndogo na jangwa na Rais pale hana nguvu kubwa kama hapa Rais anaamua kila kitu hata mambo ya Kuteua DED
 
Wanabodi

TAAMULI HURU: Wamarekani hawajawa tayari kuongozwa na Rais mwanamke Wamarekani, japo ndio the oldest democracy,lakini sio kila kitu!,bado wanakabiliwa na mfumo dume,hawajawa tayari kumchagua rais mwanamke,Sisi Afrika tumewatangulia,jana Namibia wamefanya kweli,wamechagua rais mwanamke,swali ni je na sisi Tanzania, 2025, tunakwenda kuwaonyesha?.

Paskali
 
Wanabodi

TAAMULI HURU: Wamarekani hawajawa tayari kuongozwa na Rais mwanamke Wamarekani, japo ndio the oldest democracy,lakini sio kila kitu!,bado wanakabiliwa na mfumo dume,hawajawa tayari kumchagua rais mwanamke,Sisi Afrika tumewatangulia,jana Namibia wamefanya kweli,wamechagua rais mwanamke,swali ni je na sisi Tanzania, 2025, tunakwenda kuwaonyesha?.

Paskali
Hizi notion za ajabu Sana, tunatakiwa kuchagua mtu mwenye maono regardless ya gender yake! TUACHANE na UJINGA wa kuiga.
 
Wanabodi

TAAMULI HURU: Wamarekani hawajawa tayari kuongozwa na Rais mwanamke Wamarekani, japo ndio the oldest democracy,lakini sio kila kitu!,bado wanakabiliwa na mfumo dume,hawajawa tayari kumchagua rais mwanamke,Sisi Afrika tumewatangulia,jana Namibia wamefanya kweli,wamechagua rais mwanamke,swali ni je na sisi Tanzania, 2025, tunakwenda kuwaonyesha?.

Paskali
Não Wamarekani,mababa wa Democrasia week chache zilizopita WAMEMKATAA MWANAMKE kuwa Rais wao😀😀😀🤔🤔
 
Wanabodi

TAAMULI HURU: Wamarekani hawajawa tayari kuongozwa na Rais mwanamke Wamarekani, japo ndio the oldest democracy,lakini sio kila kitu!,bado wanakabiliwa na mfumo dume,hawajawa tayari kumchagua rais mwanamke,Sisi Afrika tumewatangulia,jana Namibia wamefanya kweli,wamechagua rais mwanamke,swali ni je na sisi Tanzania, 2025, tunakwenda kuwaonyesha?.

Paskali
Kwani Tanzania huwa mnafanya uchaguzi au mnafanya maigizo ya uchaguzi ili kuwaridhisha donor kantre mkitegemea wataendelea kuwapa vimisaada vyao.
 
Back
Top Bottom