wakimataifa
JF-Expert Member
- Nov 16, 2014
- 942
- 168
nimesoma gazeti moja kuwa kuna habari ngasa ameenda afrika kusini kufanya majaribio.
mimi nampa tano lakini uongozi wa yanga unadai kuwa hauna habari eti ikibainika kama kweli itampa adhabu.
nyie vikaragosi wa yanga acheni ujinga huo wa kumng'ang'ania mchezaji kama mmemzaa nyinyi.
nimesoma gazeti moja kuwa kuna habari ngasa ameenda afrika kusini kufanya majaribio.
mimi nampa tano lakini uongozi wa yanga unadai kuwa hauna habari eti ikibainika kama kweli itampa adhabu.
nyie vikaragosi wa yanga acheni ujinga huo wa kumng'ang'ania mchezaji kama mmemzaa nyinyi.
Ngasa alishachezea Azam na Simba lakini hawakumpeleka South Afrika. Kunya anye kuku, bata anaharisha.
nasikie eti ngassa ana miaka 19?
Hapana ni miaka 17 mkuu
Kama kumbukumbu zako ziko sawa...simba walimtafutia ngassa nafasi kwenda kucheza El Merekh
Ila yeye kwa sababu ya kupenda sana chupi akagoma
Akadanganywa na matapeli wa Yanga...akavunja mkataba na simba ...sasa hivi kila mwezi anakatwa milion kuilipa simba...
Yanga walimuahidi watamsaidia kulipa laki tano kila mwezi...wamemtelekeza ...hawataki tena
Yanga ni timu ya hovyo sana
Kama kumbukumbu zako ziko sawa...simba walimtafutia ngassa nafasi kwenda kucheza El Merekh
Ila yeye kwa sababu ya kupenda sana chupi akagoma
Akadanganywa na matapeli wa Yanga...akavunja mkataba na simba ...sasa hivi kila mwezi anakatwa milion kuilipa simba...
Yanga walimuahidi watamsaidia kulipa laki tano kila mwezi...wamemtelekeza ...hawataki tena
Yanga ni timu ya hovyo sana
Tatizo lako unaandika habari nusu nusu, unasema Samata alikataa kucheza kwa sababu hakupewa gari hapo hapo unasema kwamba ilibidi auzwe kwa sababu alikataa kucheza kwa hiyo unataka kuniambia TP Mazembe walimununua Samata bila kumwona akicheza? Ukweli ni kwamba ni kweli Simba walimwahidi kumpa gari lakini hawakumpa kwa wakati naye akafanya mgomo lakini baadaye wakampa gari na mechi ya kwanza tu kucheza alifunga goli mbili sikumbuki ilikuwa ni mechi dhidi ya timu gani.Mkuu, weka ushabiki pembeni kwanza. Uhovyo wa Yanga ndio uhovyo wa Mikia. Kumbuka Mbwana Samata alifikaje TP Mazembe. Simba ilishindwa kumpa Mark II waliyoahidi akagoma kucheza. Simba wakawa hawana jinsi lazima auzwe!
Issue ya Simba kumtafutia Ngasa El Mereikh ya Sudan ina siasa ambazo labda huzijui. Walishaona kwa vyovyote Ngasa angeondoka hivyo walitaka kumtumia kupata hela sio kupenda maendeleo yake. Mambo ya wachezaji kupenda chupi si la Ngasa pekee. Huyo Kapombe kwa nini alishindwa France? Hayo ni matitizo binafsi ya wachezaji.
Yanga ni timu pekee Tanzania ambayo mchezaji wake kacheza ulaya kwa mafanikio. Waulize wenzio wakuambie ni nani huyo.
Tatizo lako unaandika habari nusu nusu, unasema Samata alikataa kucheza kwa sababu hakupewa gari hapo hapo unasema kwamba ilibidi auzwe kwa sababu alikataa kucheza kwa hiyo unataka kuniambia TP Mazembe walimununua Samata bila kumwona akicheza? Ukweli ni kwamba ni kweli Simba walimwahidi kumpa gari lakini hawakumpa kwa wakati naye akafanya mgomo lakini baadaye wakampa gari na mechi ya kwanza tu kucheza alifunga goli mbili sikumbuki ilikuwa ni mechi dhidi ya timu gani.
TP Mazembe walimwona Samata kwenye match mbili ambazo hizi timu mbili zilikutana na Samata akiwa uwanjani ndo TP Mazembe wakavutiwa naye pamoja na Ochan na kuwasajili wote wawili sasa kama alikuwa hachezi TP Mazembe wangemsajili vipi bila kumwona kumbuka Samata hakuwahi kufanya majaribio TP Mazembe ili asajiliwe.
Na kuhusu Ngasa hata kama ni kweli Simba walijua kwamba Ngasa hatacheza Simba ingawa alikuwa ameshasaini mkataba tayari sasa kulikuwa na ubaya gani kumpeleka timu kubwa kama El Mereikh na hiyo ingekuwa ni kwa faida yake mwenyewe na kwa timu yake ya Simba pia.
Kuhusu huyo mchezaji unayemsema naye hakuondoka kwa ruhusa kutoka kwa uongozi wa Yanga, alichofanya ni kutoroka na kwenda South Afrika na timu ya huko South Afrika ndo ilifaidika naye wakati alipouzwa Ulaya, Yanga haijawahi kufaidika naye zaidi ya nyie kujisifia tu kwamba alichezea Jangwani. Kwa sababu yule alifanikiwa baada ya kutoroka mwacheni Ngasa naye huenda akafanikiwa ingawa ametoroka.
kweli mkuu u17
Hela za Okwi zimeishafika au bado? Za Kapombe je? Maana Simba ndio inajua kufaidi ikiwauza wachezaji!
Naamini una ufahamu na uelewa mkubwa sana wa masuala madogo madogo kama haya, na naamini pia una uwezo mkubwa wa kuweza kutofautisha kati mzazi aliyepeleka mwanae shule akashindwa mwenyewe na mzazi ambaye hataki kusikia wanae wakienda shule. Na pia tofautisha kati ya mzazi ambaye anamruhusu mwanae kwenda kwenda mbali kujaribu maisha lakini kama atashindwa ni juu yake kuchagua kwingine.
Suala la Okwi linafahamika kuvunja kwa makubaliano kwa timu iliyomchukua Okwi ndo kumesababisha imani waliyokuwa nayo viongozi wa Simba kuonekana wajinga na waongo.
Kapombe hata wewe unajua kuna viongozi wa timu mbili walikuwa wanamrubuni Kapombe asirudi Ufaransa na bahati mbaya naye akarubunika ila angalau alipata watu wakamshauri vizuri akaenda timu aliyoenda na angejidanganya tu akaenda ile timu nyingine lazima yangemkuta ya Ngasa na Kaseja, hawataki kukuacha uondoke halafu hawataki ucheze hata dakika 15 za mwisho.
To be honest, hayo yapo Yanga peke yake?
La Kaseja lipo wazi. Simba walimwacha kwa kushuka kiwango lakini nakiri viongozi Yanga walifanya makosa kumsajili. Kiwango chake ndio tatizo. Kumbuka mechi ya Yanga na Coast Union kule Tanga. Vinginevyo tuseme aliuza mechi lakini tusifike huko tuseme kiwango kimeshuka.
Ngasa pamoja na mapenzi yake kwa Yanga ni kielelezo cha soka la Tanzania. Si Yanga, Azam wala Simba. Viongozi wa timu zetu kongwe pamoja na Azam ambao ungetegemea wabadilike kutokana na umilika wa Club, bado wapo kwenye ujima wa namna ya kuendesha soka.
Tuone VPL mwaka huu itaisha vipi safari bado ni ndefu