Ngoja nikwambie sasa, sisi wahuni wa miaka ya 90 na tulivyo sasa

Ngoja nikwambie sasa, sisi wahuni wa miaka ya 90 na tulivyo sasa

Unajua nawacheki vijana wa kisasa naona kama wanaigiza uhuni kuliko uhalisia. Sisi tuliishi nyakati za hatari miaka ya 90 halafu bado tumebaki na akili za kusimulia vijana.

Umetoka Ubungo ukapita External, ukapita Garage kituo kinachofuata ni Tabata Relini (Mwananchi)

Ukishuka pale unavuka barabara unaingia kulia unafuata barabara au unaambaa ambaa na reli ile mpaka unaposhuka tena kulia na kupandisha kamlima kadogo ukiacha ile Bar ya Mtaita. (Pale walikuwa pia wanauza Sambusa nzuri sana za Nyama miaka ya 90) ukiendelea mbele utakutana na uliokuwa MJI MPYA.

Ukitembea sana utakuja kutana na Uwanja wa Twiga. Mimi ndo ulikuwa uwanja wangu wa kuangalia mpira jioni, mazoezi au mechi.

Miaka hiyo kuna team ta Twiga iliyokuwa na jersey za utumbo zenye namba kubwa mgongoni 60, 78, 86, 97 n.k

Pale mlangoni ulikuwa unamkuta gollie mmoja mbabe sana anaitwa Omary. Sijui yu wapi huyu bwana. Nataman sana kumwona. Jamaa alikuwa anapendeza sana mlangoni, hasa kwa udakaji wake na alivyokuwa akiwagonga vichwa wachezaji pinzani kwa usiri mkubwa sana.

Kulikuwa na wachezaji wazuri wenye speed mmoja wapo alikuwa Martin Kiberenge. Huyu jamaa alikuwa anakimbia na mpira balaa. Maskini alikuja ishia kuwa mpiga picha tu. But huyu jamaa hakupaswa kucheza soka la Bongo.

Alikuwepo Kiruguru. Huyu alikuwa amekomaa sana na mfupi asiye na woga uwanjani. Kisha unakuja kutana na Mluguru mwingine mrefu ambaye miaka hiyo wenzake wanacheza mpira wamevaa viatu yeye alikuwa anacheza peku na alikuwa anaçhana sana mipira kwa miguu yake.

Alikuwa na nguvu na amekomaa sana. Mechi zilikuwa zinachezwa huku refarii ameweka panga kiunoni maana ilikuwa kipigo nje nje kwa marefa. Kama refa unaonekana umeshindwa kuumudu mchezo basi wananchi wanaonesha wanaweza kukumudu.

Mara nyingi sana kulikuwa kunatokea vipigo vya mawe, mapanga n.k so si ajabu wakati wa kumaliza mpira refa akawa ameenda simama eneo ambalo anajua anaweza chomoka kwa urahisi kukimbia kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali.

Wakati huo kundi kubwa la masela lina check mpira huku linavuta bhangi pembeni ya uwanja. Sasa usiwe na kiherehere ukataka uangalie mpira peke yako kwa kusimama na kuwaziba wengine. Utapigwa makonzi mpaka kichwa kibonyee halafu baadaye ndo kivimbe utadhani ndani kimewekwa kokoto pasipo mpangilio maalum.

Maisha mtaani yalikuwa ya ubabe. Demu unampata kwa ubabe na unadumu naye ukiwa mbabe, otherwise watu watakuchukulia tu.

Nakumbuka miaka hiyo ndo kukatokea kutokuelewana katika team ya Twiga ikavunjika na kuwa na Team Mbili. Twiga (Wastaarabu) na Begeju (watoto wa Mbwa) ilikuwa inapigwa game zikikutana team hizi mbili ni hatari na nusu. Na mwishowe si ajabu kutokea kipigo

But kumbuka ni team za hapo hapo na zinatumia uwanja mmoja. Mimi walikuwa mara nyingi wakinishawishi niende nao tunapoenda kucheza mechi mbali,Temeke, Ubungo n.k ili ikitokea tunahitaji kuchapana mkono nami niwape msaaada wangu.

Mimi nlikuwa napenda ugomvi.napenda sana miaka hiyo nmemaliza shule ya Msingi Makubuli/Mabibo then nasoma Tambaza ( wababe wa Dar) so nlikuwa mbabe ila nina akili.

Kulikuwa na wapiga mnanda maarufu miaka hiyo akina Furahisha(alikuja kuwa teja) Fikirini, Ali, Masud na wengine nmewasahau. Bhangi, Mademu na Pombe.

Mimi sasa naonekana mambo safi mtoto wa kidosi ila niliyechangamka.maana nlikuwa naweza kugonga sana ngumi.jamaa wengi kitaa walikuwa wanaishia darasa la saba na wengine hawamalizi hata hilo darasa la saba.

Late 2000 nikiwa mwaka wa 2 UDSM. Mzee aliamua tuhame tuhamie Sinza ambako pia tulikuwa na nyumba na ilikuwa wazazi wanakaa kule sisi na baba mdogo tunaishi huku Tabata Kimanga. Nakumbuka ile picha iliyokuwa na maneno HII NGUNA LAZIMA IISHE LEO,IWE IWEJE!

Miaka ile mitaani ulikuwa huwezi kuta shoga.utampata wapi na vijana tulifunzwa ukakamavu mapema sana? Nilikuwa mhuni sana ambaye leo hii natamani niende fanya visiting yale maeneo niwatafute wana. Zaidi ya miaka 20 sijafika tena huko.

Najitizama najiona nmebadilika sana.nlichange kwa ghafla sana katika maisha na leo hii nmekuwa hivi nilivyo mpole na mwenye aibu sielewi sababu ni nini hasa.

Hapohapo kiwanda cha unga cha Nyati nyuma kulikuwa na uwanja na timu flani nimeisahau jina, jioni ni mwendo wa wahuni kuvuta bangi huku wakicheki mazoezi, sasa pita kuanzia saa 12 na nusu jioni uone utakavyokabwa
 
unenikumbusha tuliokuwa tunakaa kurasini
uwanja wa Ugimbi
na pia hapa kanisani ambako sasa kuna ofisi za Radio ya wapo
lakini pia keko uwanja wa KJ
hatari tupuuuuuu
kuna timu ilikua inaitwa Cyborg wanatokea keko
hatari tupuuu haoooo
ngumi mkononiii
 
unenikumbusha tuliokuwa tunakaa kurasini
uwanja wa Ugimbi
na pia hapa kanisani ambako sasa kuna ofisi za Radio ya wapo
lakini pia keko uwanja wa KJ
hatari tupuuuuuu
kuna timu ilikua inaitwa Cyborg wanatokea keko
hatari tupuuu haoooo
ngumi mkononiii
Tupe mikasa yao....
 
Mkuu huo uhuni fresh.....lkn kwa miaka hio hio nikikuletea mambo yaliokua yakitendeka pale Mbeya....haki utabaki mdomoa wazi....

Mbeya town pale nilishudia vijana maeno ya ilemi chini walikua kama nane hivi.....wanapigana kwa visu afu kumbe ni pambano kabisa walishaambiana wakutane wazichape......makundi mawili tofauti........watu watatu walifia pale pale.....!!!

Mzee moja jirani yetu alishushwa kwenye landrover yake kama masihara.....afu watu wakashika uskani wakasepa....kina Nani hao.....Jombi baba
R.I.P uncle jombi.
Mpwa wake nimehamishia ubabe kwenye Kusaka mapesa.
 
unenikumbusha tuliokuwa tunakaa kurasini
uwanja wa Ugimbi
na pia hapa kanisani ambako sasa kuna ofisi za Radio ya wapo
lakini pia keko uwanja wa KJ
hatari tupuuuuuu
kuna timu ilikua inaitwa Cyborg wanatokea keko
hatari tupuuu haoooo
ngumi mkononiii
Oy uwanja wa Ugimbi bdo upo masta.?
Ni ile bar pale ndani uwanjani tulikuwa tunacheza disco toto back then bado ipo..?
 
Mkuu huo uhuni fresh.....lkn kwa miaka hio hio nikikuletea mambo yaliokua yakitendeka pale Mbeya....haki utabaki mdomoa wazi....

Mbeya town pale nilishudia vijana maeno ya ilemi chini walikua kama nane hivi.....wanapigana kwa visu afu kumbe ni pambano kabisa walishaambiana wakutane wazichape......makundi mawili tofauti........watu watatu walifia pale pale.....!!!

Mzee moja jirani yetu alishushwa kwenye landrover yake kama masihara.....afu watu wakashika uskani wakasepa....kina Nani hao.....Jombi baba
Binafsi mm nlishakutana na jombi uso kwa uso mitaa ya soweto pale garage kwake wkt huo nlikuwa chali sanaa
Alafu mbeya mitaa ya nzovwe kulikuwa na jamaa mmja anaitwa Mike maisumbe alikuwa nunda sana makesi kibao vp yupo au maana kama akiwa Hai mpaka leo basi atakuwa kaokoka 😂

Ova
 
Kulikuwa na mbabe mmja hko anaitwa santana sjui yupo bd au uzee tayari

Ova
Yap Santana alikuwa na nyumba yake pale kwa mfuga mbwa,nami nimetoka muda mrefu sijui anaendeleaje,ila tulishawahi kukutana kwenye vurugu kati ya wavete wa pale manzese kwa wachonga visu dhidi ya Chicago ya manzese kwa mfuga mbwa ila timbwili halikutokea kwa kuwa wavete tulikuwa na support ya wahuni mpaka Mabibo na Mburahati ikabidi Santana na Chicago yake watulie tukayamaliza kwa makaratasi na wao kwenda kufuta kesi polisi Urafiki.
Nalog off
 
Unajua nawacheki vijana wa kisasa naona kama wanaigiza uhuni kuliko uhalisia. Sisi tuliishi nyakati za hatari miaka ya 90 halafu bado tumebaki na akili za kusimulia vijana.

Umetoka Ubungo ukapita External, ukapita Garage kituo kinachofuata ni Tabata Relini (Mwananchi)

Ukishuka pale unavuka barabara unaingia kulia unafuata barabara au unaambaa ambaa na reli ile mpaka unaposhuka tena kulia na kupandisha kamlima kadogo ukiacha ile Bar ya Mtaita. (Pale walikuwa pia wanauza Sambusa nzuri sana za Nyama miaka ya 90) ukiendelea mbele utakutana na uliokuwa MJI MPYA.

Ukitembea sana utakuja kutana na Uwanja wa Twiga. Mimi ndo ulikuwa uwanja wangu wa kuangalia mpira jioni, mazoezi au mechi.

Miaka hiyo kuna team ta Twiga iliyokuwa na jersey za utumbo zenye namba kubwa mgongoni 60, 78, 86, 97 n.k

Pale mlangoni ulikuwa unamkuta gollie mmoja mbabe sana anaitwa Omary. Sijui yu wapi huyu bwana. Nataman sana kumwona. Jamaa alikuwa anapendeza sana mlangoni, hasa kwa udakaji wake na alivyokuwa akiwagonga vichwa wachezaji pinzani kwa usiri mkubwa sana.

Kulikuwa na wachezaji wazuri wenye speed mmoja wapo alikuwa Martin Kiberenge. Huyu jamaa alikuwa anakimbia na mpira balaa. Maskini alikuja ishia kuwa mpiga picha tu. But huyu jamaa hakupaswa kucheza soka la Bongo.

Alikuwepo Kiruguru. Huyu alikuwa amekomaa sana na mfupi asiye na woga uwanjani. Kisha unakuja kutana na Mluguru mwingine mrefu ambaye miaka hiyo wenzake wanacheza mpira wamevaa viatu yeye alikuwa anacheza peku na alikuwa anaçhana sana mipira kwa miguu yake.

Alikuwa na nguvu na amekomaa sana. Mechi zilikuwa zinachezwa huku refarii ameweka panga kiunoni maana ilikuwa kipigo nje nje kwa marefa. Kama refa unaonekana umeshindwa kuumudu mchezo basi wananchi wanaonesha wanaweza kukumudu.

Mara nyingi sana kulikuwa kunatokea vipigo vya mawe, mapanga n.k so si ajabu wakati wa kumaliza mpira refa akawa ameenda simama eneo ambalo anajua anaweza chomoka kwa urahisi kukimbia kipigo kutoka kwa wananchi wenye hasira kali.

Wakati huo kundi kubwa la masela lina check mpira huku linavuta bhangi pembeni ya uwanja. Sasa usiwe na kiherehere ukataka uangalie mpira peke yako kwa kusimama na kuwaziba wengine. Utapigwa makonzi mpaka kichwa kibonyee halafu baadaye ndo kivimbe utadhani ndani kimewekwa kokoto pasipo mpangilio maalum.

Maisha mtaani yalikuwa ya ubabe. Demu unampata kwa ubabe na unadumu naye ukiwa mbabe, otherwise watu watakuchukulia tu.

Nakumbuka miaka hiyo ndo kukatokea kutokuelewana katika team ya Twiga ikavunjika na kuwa na Team Mbili. Twiga (Wastaarabu) na Begeju (watoto wa Mbwa) ilikuwa inapigwa game zikikutana team hizi mbili ni hatari na nusu. Na mwishowe si ajabu kutokea kipigo

But kumbuka ni team za hapo hapo na zinatumia uwanja mmoja. Mimi walikuwa mara nyingi wakinishawishi niende nao tunapoenda kucheza mechi mbali,Temeke, Ubungo n.k ili ikitokea tunahitaji kuchapana mkono nami niwape msaaada wangu.

Mimi nlikuwa napenda ugomvi.napenda sana miaka hiyo nmemaliza shule ya Msingi Makubuli/Mabibo then nasoma Tambaza ( wababe wa Dar) so nlikuwa mbabe ila nina akili.

Kulikuwa na wapiga mnanda maarufu miaka hiyo akina Furahisha(alikuja kuwa teja) Fikirini, Ali, Masud na wengine nmewasahau. Bhangi, Mademu na Pombe.

Mimi sasa naonekana mambo safi mtoto wa kidosi ila niliyechangamka.maana nlikuwa naweza kugonga sana ngumi.jamaa wengi kitaa walikuwa wanaishia darasa la saba na wengine hawamalizi hata hilo darasa la saba.

Late 2000 nikiwa mwaka wa 2 UDSM. Mzee aliamua tuhame tuhamie Sinza ambako pia tulikuwa na nyumba na ilikuwa wazazi wanakaa kule sisi na baba mdogo tunaishi huku Tabata Kimanga. Nakumbuka ile picha iliyokuwa na maneno HII NGUNA LAZIMA IISHE LEO,IWE IWEJE!

Miaka ile mitaani ulikuwa huwezi kuta shoga.utampata wapi na vijana tulifunzwa ukakamavu mapema sana? Nilikuwa mhuni sana ambaye leo hii natamani niende fanya visiting yale maeneo niwatafute wana. Zaidi ya miaka 20 sijafika tena huko.

Najitizama najiona nmebadilika sana.nlichange kwa ghafla sana katika maisha na leo hii nmekuwa hivi nilivyo mpole na mwenye aibu sielewi sababu ni nini hasa.
kwa mtazamo wangu, pamoja na yote, hapo (kwenye nyekundu) ndipo ilipo hoja kuu ya mtoa mada......nikitumia maarifa ya o'level ya uchambuzi wa kazi za kifasihi naona kabisa mtoa mada anasumbuliwa na aina ya maisha iliyopo sasa kwa vijana wetu;

mifumo ya maisha imebadilika badilika, imevurugwa vurugwa! hakuna ukakamavu wala kugangamala....vijana wamekuwa lainiiiiii, wanashindana na dada zao kutembea na vioo vya kujirembea kwenye vipochi na hatimae ushoga umetapakaa.....wajanja wa siku hizi ni wale wanaoweza kucheza video games vizuri au kuyaelezea mavazi ya kina diamonds vizuri, lakini si wale tena wanaofanya, angalau, mambo ya kishujaa.

watoto wa kiume sasa wanalindwa kama wanavyolindwa watoto wa kike maana ukishangaa tu utakuta wameraruliwa malinda, hawawezi hata kujitetea.....wako lainiiiiii. kijana wa kidato cha nne anagoma kwenda shule eti kisa mama yake hajamtumia hela ya kutumia shuleni.

kijana wa kidato cha nne anaomba ruhusa shule aende kwa mama yake ili akamshonee suruali yake iliyotatuka kidogo mapajani.


mnaokejeli uzi huu mmenishangaza sana!

ahsante sana mtoa mada, umenitafakarisha sana kuhusu yajayo ya vijana wetu hawa!!
 
unenikumbusha tuliokuwa tunakaa kurasini
uwanja wa Ugimbi
na pia hapa kanisani ambako sasa kuna ofisi za Radio ya wapo
lakini pia keko uwanja wa KJ
hatari tupuuuuuu
kuna timu ilikua inaitwa Cyborg wanatokea keko
hatari tupuuu haoooo
ngumi mkononiii
Kj wavurana bango au si wavuta bangi ukuta wa kanisani apo.
 
Kipindi hicho chugaa kulikuwa na makonseti...cresto aka shimoni....Metropol...Arusha bye night...risk club....mechii za mashule naboishuu vs Arusha sec,soweto.bondeni na ilboru....makumira na Arusha day.achaa kabisaa
 
Back
Top Bottom