Ngumi rasharasha manusura nijifie

Ngumi rasharasha manusura nijifie

Mkanganyiko kukanganya

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2022
Posts
1,204
Reaction score
5,053
Wiki juzi almanusura nife miaka ya nyuma kidogo nilikuwa naweza kutupa ngumi mbili tatu pumzi ya kati😂😂😂😂 Majuzi tuko huko baani nikiwanashtua kidogo, mara jamaa akaanzisha ugomvi, chap kasogeza meza tuzipange.

Sikutaka kubaki mnyonge nikijiamini na kale ka pumzi kangu!! Nimerusha ngumi ya kipekee kabisa jamaa kachomoa gafla aliniteketeza kwa mapigo ya juu na wastani bila kutarajia mi kule chali damu walawala.

Ugomvi wenyewe kisa waiter mwenye kawowowo ambaye ni best yangu kitambo mzigo mara chache na vimichongo vya vidili haramu kidogo!

Waiter wangu Julie ndo alinipepea kuzinduka, namshukuru

NB: Vijana tufanyeni mazoezi dah💪💪💪💪

Share nasi ulishawahi kupigana!!?
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Daah jamaa kachukua point 3 nyumbani.

Ugomvi sio poa kubaya zaidi ni mwanamke ndio mnagombea. Kwa sababu ni mrupo wako(ubabe) ungeweza kufanya ubabe wa kuhakikisha una ondoka nae hapo jamaa ungemshinda pakubwa. Sasa unaruhusu mnafikia kwenye ugomvi wengine wanakuaga na bastola ukimzidi anachomoa chuma.

Kitu nachoepuka ni ugomvi nikishanusa harufu hiyo nakusanya vilivyo vyangu naambaa. Ndio tutakufa ila sio kwa style hiyo ambayo unaweza kuepuka
 
Kuna jamaa alipigwa ngumi ya taya na polisi .Alikuwa anapiga mihayo siku nzima na kujiongelesha na kujijibu mwenyewe.Epuka ugomvi kwa namna yoyote ile hasa wa bar kuitwa marehemu ni dk 0 tu.
 
Pole mkuu

Usifikiri wazungu hawakuona ilo mpaka kuamua kutengeneza silaha.
Screenshot_20230130-222657.jpg
 
Back
Top Bottom