Ngurumo: 90% waliohudhuria huo mkutano wa Tundu Lissu alipokuwa akikinanga chama chake, walikuwa ni wana CCM waliovaa sare za CHADEMA bila yeye kujua

Dr Akili

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2011
Posts
5,119
Reaction score
4,569
Kweli ccm ni zaidi ya hatari. Ni wabobezi na welevu wa kila mbinu za ku deal na upinzani in a friendly way bila wao kujua.

Kumbe waliohudhuria ule mkutano wa Tundu Lisu alipokuwa akikinanga chama chake cha chadema, wengi waliohudhuria mkutano huo, pasipo Tundu Lissu kujua, walikuwa ni wana ccm. Ilifikia mahali wakajisahau na kumshangilia kwa kibwagizo cha ccm.

Kama una muda msikilize huyu mchambuzi makini wa siasa za Tanzania hapo chini.


View: https://youtube.com/watch?v=NU3b3IYQjhk&si=BOhK2JWMuwWTZ0kl
 
Kwani kuna utaratibu wa nivae mavazi gani ili mimi nihudhurie mkutano wa mwanasiasa?
 
Kwani kuna utaratibu wa nivae mavazi gani ili mimi nihudhurie mkutano wa mwanasiasa?
Mkutano wake haukufuata taratibu za chama chake, sasa utegemee nini? Mamuluki kutoka ccm waliingia ukumbini kirahisi. Hata kwenye sherehe hususani za harusi wazamiaji wataingia kwa wingi ukumbini kama kamati ya sherehe haikuweka utaratibu madhubuti wa mtu kuingia ukumbini. Hivyo ndivyo ilikuwa kwenye huo mkutano wa Lissu. Ukiwa na sare ya chama unaingia. Ukisalimu kwa piiiiiipoz, unaingia.
 
Wapumbavu wekeni picha tuone
Kwani hukuziona hizo picha walizopiga za wanahabari? Mkutano ulikuwa fully covered na wanahabari wa media mbali mbali. Kaziangalie YouTube, Instagram, tiktok, Facebook na kadhalika
 
Mnaongea sana lakini Mbowe atambue alama za nyakati. Chama kinamuhitaji Lissu kama Mwenyekiti, Heche kama katibu.
Chama ni nani? Wewe na Lissu na hao wachache ndiyo mnajiita chama? Kwa taarifa yako wenye kuamua hilo unalolitaka ni mkutano mkuu wa chama.
 
Maccm mnahangaika sana mnamuogopa sana Lissu
 
Ngurumo naye ni chawa wa Mbowe hana lolote.
 
Hata kama walikuwepo NIA imetangazwa haijatangazwa?
Kwamba uwepo wa wanachama wa ccm ndio umezuia kusikika kwa nia ya mh. TL kwa wanachadema?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…