Nguvu ya Kutokukata Tamaa: Mdau, Hadithi Yako ya Mafanikio ni Ipi?

Nguvu ya Kutokukata Tamaa: Mdau, Hadithi Yako ya Mafanikio ni Ipi?

Aggrey sallah

Member
Joined
Sep 15, 2022
Posts
31
Reaction score
45
Katika safari yako ya mafanikio, ni wakati gani ulijikuta karibu sana na kukata tamaa? Ni nani au nini kilikusukuma uendelee mbele?

Tunapenda kujua hadithi yako na mambo yaliyokupa nguvu ya kusimama tena na kuendelea kupigania ndoto zako.
 

Kwa upande wangu, Mr Kenzy kutokukata tamaa kumekuwa msingi wa mafanikio yangu. Nilipokuwa mdogo, niliishi katika mazingira yenye changamoto nyingi, lakini nilijifunza kwamba kila changamoto ni fursa ya kujifunza na kukua. Licha ya kukosa rasilimali nyingi, niliendelea kusoma kwa bidii na kufanya kazi za vibarua ili kujimudu na kufikia ndoto zangu.

Nikiwa chuo kikuu, nilikumbana na changamoto nyingi za kifedha, lakini sikukata tamaa. Nilitafuta msaada na fursa za kujifunza zaidi. Baada ya kuhitimu, nilianzisha Kampuni ambayo inafanya masuala ya Kilimo , lengo ni ili kusaidia wakulima vijana kama mimi kuboresha kilimo na maisha yao. Kwa kupitia Kampuni hii sasa tumefanikiwa kusaidia wakulima wengi kuongeza mavuno na kipato chao, na hivyo kuboresha maisha ya familia nyingi.

Kwa hiyo, kwa maoni yangu, kutokukata tamaa ni nguzo muhimu sana katika safari ya mafanikio. Ni nguvu inayotusaidia kusimama imara wakati wa changamoto na kuendelea kusonga mbele hadi tufikie malengo yetu.

Ningependa kusikia maoni yenu na uzoefu wenu pia kuhusu jambo hili.
 
Nyuma ya changamoto Kuna mafanikio, tuzikubali, tuziishi, tujifunze lakini kamwe tusikate tamaa.
 
Aisee siku ile nambiwa nipo hiv positive kwa kweli nilikata tamaa ya maisha yaani niliwaza nikajinyonge kwenye mpapai lakini ikashindikana.
Anyways sikukata tamaaa nikaendelea kusema yote maisha
 
Safari ya kukatisha tamaa ilikuja pale nilipo risk nilivyonavyo/nilivyotafuta kwa muda mrefu kupotea katika jambo ambalo nili-hope naenda kubadilisha maisha lakini ukawa ndio mwanzo wa upotevu.

Niliamua kutokukata tamaa kwa sababu 1 kubwa nilipo jiuliza swali kwanini nilianza? Nikajiambia sababu kubwa nikufanikiwa na bado sijafanikiwa, nikasimama tena kwa kujifunza kwanza na kuanza kutake calculated risks.

Nimeamua Kuiishi falsafa ya "Get Rich or Die Trying" bado sijapata lakini kombe linapambaniwa.

I have choose to be reall to myself, Nyakati na Bahati zitakapokaa upande wangu We shall meet there.

Umasikini unaumiza lakini kutokufanya kitu kunaumiza zaidi, tupambane tu .
 
Hakika
Nyuma ya changamoto Kuna mafanikio, tuzikubali, tuziishi, tujifunze lakini kamwe tusikate tamaa.
Hakika Ndugu yangu hakuna Nafasi ya kukata Tamaa, consistency is the key to success. Hakikisha ukianza jambo mpaka lifike mwisho, hakuna kuishia njiani. Let keep fight ✨ 💪
 
Safari ya kukatisha tamaa ilikuja pale nilipo risk nilivyonavyo/nilivyotafuta kwa muda mrefu kupotea katika jambo ambalo nili-hope naenda kubadilisha maisha lakini ukawa ndio mwanzo wa upotevu.

Niliamua kutokukata tamaa kwa sababu 1 kubwa nilipo jiuliza swali kwanini nilianza? Nikajiambia sababu kubwa nikufanikiwa na bado sijafanikiwa, nikasimama tena kwa kujifunza kwanza na kuanza kutake calculated risks.

Nimeamua Kuiishi falsafa ya "Get Rich or Die Trying" bado sijapata lakini kombe linapambaniwa.

I have choose to be reall to myself, Nyakati na Bahati zitakapokaa upande wangu We shall meet there.

Umasikini unaumiza lakini kutokufanya kitu kunaumiza zaidi, tupambane tu .
"Get rich or Die trying" 🔥 🔥 thanks brother Miguel wa II for sharing.
Tajiri mmoja nilimuuliza Ndugu yangu ni Nini Siri ya mafanikio Yako. Alinijibu, "when I start anything, I fight until it complete no matter what obstacle on my way" lkn akanisisitiza on doing the right things on right time, alisema amejifunza kitu kikubwa sana kwenye kitabu Cha "eat that frog" (Kama sijakosea) kuwa "many people are loosing alot of time doing thing that are good but are not required on the time" anaendeleaje kusema kuwa kabla hujapanda ngazi make sure it's on the right building. Hii ilinijenga Kwa sehemu yake pia
 
Back
Top Bottom