Nguvu ya matajiri itakapoanza kuchukua nafasi yake, kilio cha wanyonge kumlilia Dkt. Magufuli itazidi kusikika na wa kuwazuia hatakuwepo

Pslmp

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2021
Posts
1,622
Reaction score
2,458
Ndiyo!
Nguvu ya matajiri ikiilemea serikali hii mpya, wanyonge watalitaja Jina la JPM Kwa uchungu mkubwa na hakuna atakayewazuia

Pale rushwa itakapowafanya wanyonge, wamachinga, wamama ntilie, bodaboda, bajaji n.k ambao idadi Yao ni kubwa mno Kwa sasa katika nchi hii kuanza kufukuzwa kwenye maeneo Yao ya kazi aliyokuwa amewaruhusu Jembe Lao JPM R.I.P kufanyia biashara zao,

Ndipo sauti zao na Kwa uchungu mkubwa zitasikika, wakimlilia Kwa upya tena JPM na Jina lake litatawala Kwa upya kwenye vyombo mbalimbali za habari kote Tanzania na hata duniani

Pale majambazi ya kupora muda wowote asubuhi mchana na Wakati wowote yatakapojitokeza, iwapo Serikali hii haitasimama Kiume, sauti za wananchi wengi watakapoanza kumlilia JPM Kwa upya, na watu watasema ni Bora alipokuwepo Jembe haya yalikoma,

Pale matajiri wakubwa watakapoizidi serikali ujanja aidha Kwa rushwa Ili wasilipe Kodi, na Kodi nyingi kuelekezwa Kwa wafanya biashara wadogo wadogo, watu hawa wataanza kumlilia upya Jembe lao, watasema, ni Kwa sababu hayupo JPM ndio Maana wananyanyaswa?

Ingawa Nina Imani kuuubwa Sana na Raisi wetu Madame SHS, kwamba ni jemedali na jasiri asiyeogopa na asiyerudishwa nyuma, Kwa kuwa pia ufanisi wa serikali hii Naamini ni Kwa sababu mama alisimama nyuma yake kuhakikisha tunakuwa hapa tulipo

Mbali na hayo, Sisi ni binadamu tunaweza kujisahau yakarudi hayo na yakawa sababu ya Jina la Jembe kutajwa kila pahala kuwa yeye alikuwa mwanvuli wa watu wa Chini na kujikuta Jina lake likitawala fikra zao na hata kutajwa Sana Kwa mema hayo kwenye midomo ya watu wanyonge!

Hayo yasipozingatiwa yataibua vilio vya watu hao

Mh Raisi Madame Samia suluhu Hasan Tunakuombea, kwani tunajua ilivyongumu kuongoza nchi bila ya Mungu Kusimama Mbele yako

Wasalaam
 
Well said brother.Umuhimu wa mtu huthibitika baada ya kufa. Waliokuwa wanashinda mitandaoni wakitukana na kudhihaki uongozi wa JPM sasa wataanza kumkumbuka kinafiki.

Uongozi ni kuwawezesha watu kwa kuwawekea miundombinu ili iwasaidie katika shughuli zao,na Magufuli alifanikiwa kwenye hilo.
 
Hakuna mjadala wamachinga wanatakiwa kytafutiwa maeneo ya kufanyia biashara sio barabara zinazojengwa na walipa kodi fullstop.

...umekuwa mmachinga miaka mi5 hujafanikiwa kubuni kitu hata ukipewa 100 hutaweza,mmachinga gani ana msingi wa milioni 5!!
 
Pombe Magufuli hajawai kumtetea mnyonge yeyote bali alitumia wanyonge kujijenga kiaiasa. Kama ni kutetea wanyonge alipaswa kuwafidia wale wananchi wa Kimara- Kibaha aliowavunjia nyumba kupisha barabara.

Angekuwa mtetezi wa wanyonge asingetumia mabilioni kujenga Chato kijijini kwao miundombinu inayostahili kuwa makao makuu ya Mkoa wa Geita. Huku watoto wa Watanzania wanasoma kwenye kwenye miti na wengine hawana madawati. Au kununua madreamliner wakati 80% ya Watanzania hawapati maji safi.

Magufuli ilikuwa ni LAANA, na Mungu ametuepushia, tujenge Tanzania yetu nzuri isiyo na ubaguzi wa kiitikadi, kikabila na kikanda.
 
Na nyinyi mpunguze sasa kudeka! Mtu ameshatangulia mbele za haki, nyinyi kutwa kulia lia tu. Mnaona ni sifa kujiita wanyonge?
 
Mkuu, yasipozingatiwa hayo, ninao uhakika watu watalitaja Jina la JPM huku wakilia
 
Utajiri ni Baraka, umasikini na unyonge ni laana, na Matajiri ndio wanatengeneza ajira kwenye nchi na kodi kwa Serikali ili Nchi iwe tajiri, Serikali haiwezi endelea kama haiwezi tengeneza matajiri, matajiri ni JESHI la uchumi ktk Nchi, na ndio Jeshi muhimu sana. Kibaya ni rushwa na uonevu kwa Wananchi. Tusipandikize chuki na kutoa maoni potufu ambayo yanaiumiza nchi. Roho mbaya,wivu na husuda hazisadii, Fanya Kazi na HAPA KAZI TU INAENDELEA
 
Mawazo yako ni mazuri Ila nilichokiandika rudia tena Kusoma utaelewa tu mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…