Nguvu ya matajiri itakapoanza kuchukua nafasi yake, kilio cha wanyonge kumlilia Dkt. Magufuli itazidi kusikika na wa kuwazuia hatakuwepo

Nguvu ya matajiri itakapoanza kuchukua nafasi yake, kilio cha wanyonge kumlilia Dkt. Magufuli itazidi kusikika na wa kuwazuia hatakuwepo

Mkuu umenena mazito na makubwa na siku zote chizi naye huwasema wenye akili zao njema eti nao hawana akili, sio ajabu mkuu, mambo haya yapo Tu

Vigeugeu Wapo na hawataisha
Hakika mkuu
 
naona umeandika mashahiri haha.
its simple nilicho hoji ni logic not ushabiki. and because sina interest na upande wowote ule. just a concerned citizen
Hata mm sina Chama chochote ila nazungumza ukwl mtupu.
 
Ningeenda lakini nina majukumu mengine sehem nyingine lakini nayo yanahusu msiba huohuo,, kwahiyo naamini nitapata nafasi ya kuwepo, usijali ndugu yangu.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Judas Iscariot muda huo huna.

Usaliti wako umeshatimia basi ndy furaha kwako..

a traitor is always a traitor
 
Pombe Magufuli hajawai kumtetea mnyonge yeyote bali alitumia wanyonge kujijenga kiaiasa. Kama ni kutetea wanyonge alipaswa kuwafidia wale wananchi wa Kimara- Kibaha aliowavunjia nyumba kupisha barabara.

Angekuwa mtetezi wa wanyonge asingetumia mabilioni kujenga Chato kijijini kwao miundombinu inayostahili kuwa makao makuu ya Mkoa wa Geita. Huku watoto wa Watanzania wanasoma kwenye kwenye miti na wengine hawana madawati. Au kununua madreamliner wakati 80% ya Watanzania hawapati maji safi.

Magufuli ilikuwa ni LAANA, na Mungu ametuepushia, tujenge Tanzania yetu nzuri isiyo na ubaguzi wa kiitikadi, kikabila na kikanda.
Naam huo ndo ukweli japo umeeleza kwa ufupi muelewa kaelewa,
 
Yetu macho, kama hii leo tu tunaanza kuona wizi wa makontena bandarini!! Hii inaashilia nini
 
Ndiyo!
Nguvu ya matajiri ikiilemea serikali hii mpya, wanyonge watalitaja Jina la JPM Kwa uchungu mkubwa na hakuna atakayewazuia

Pale rushwa itakapowafanya wanyonge, wamachinga, wamama ntilie, bodaboda, bajaji n.k ambao idadi Yao ni kubwa mno Kwa sasa katika nchi hii kuanza kufukuzwa kwenye maeneo Yao ya kazi aliyokuwa amewaruhusu Jembe Lao JPM R.I.P kufanyia biashara zao,

Ndipo sauti zao na Kwa uchungu mkubwa zitasikika, wakimlilia Kwa upya tena JPM na Jina lake litatawala Kwa upya kwenye vyombo mbalimbali za habari kote Tanzania na hata duniani

Pale majambazi ya kupora muda wowote asubuhi mchana na Wakati wowote yatakapojitokeza, iwapo Serikali hii haitasimama Kiume, sauti za wananchi wengi watakapoanza kumlilia JPM Kwa upya, na watu watasema ni Bora alipokuwepo Jembe haya yalikoma,

Pale matajiri wakubwa watakapoizidi serikali ujanja aidha Kwa rushwa Ili wasilipe Kodi, na Kodi nyingi kuelekezwa Kwa wafanya biashara wadogo wadogo, watu hawa wataanza kumlilia upya Jembe lao, watasema, ni Kwa sababu hayupo JPM ndio Maana wananyanyaswa?

Ingawa Nina Imani kuuubwa Sana na Raisi wetu Madame SHS, kwamba ni jemedali na jasiri asiyeogopa na asiyerudishwa nyuma, Kwa kuwa pia ufanisi wa serikali hii Naamini ni Kwa sababu mama alisimama nyuma yake kuhakikisha tunakuwa hapa tulipo

Mbali na hayo, Sisi ni binadamu tunaweza kujisahau yakarudi hayo na yakawa sababu ya Jina la Jembe kutajwa kila pahala kuwa yeye alikuwa mwanvuli wa watu wa Chini na kujikuta Jina lake likitawala fikra zao na hata kutajwa Sana Kwa mema hayo kwenye midomo ya watu wanyonge!

Hayo yasipozingatiwa yataibua vilio vya watu hao

Mh Raisi Madame Samia suluhu Hasan Tunakuombea, kwani tunajua ilivyongumu kuongoza nchi bila ya Mungu Kusimama Mbele yako

Wasalaam
Unajua wala rushwa,wakwepaji kodi,n.k walikuwepo na watakuwepo.sababu kuu ya baadhi yetu kuamini kuwa wakati wa utawala wa hayati JPM vitu hivi havikuwepo ni kuwa vyama vya upinzani vilibanwa sana,(opposition parties),pili hakukuwa na uhuru wa vyombo vya habari.
 
Unajua wala rushwa,wakwepaji kodi,n.k walikuwepo na watakuwepo.sababu kuu ya baadhi yetu kuamini kuwa wakati wa utawala wa hayati JPM vitu hivi havikuwepo ni kuwa vyama vya upinzani vilibanwa sana,(opposition parties),pili hakukuwa na uhuru wa vyombo vya habari.
Lakini hatujaona ule Uonevu mkubwa kama kipindi cha nyuma
 
Mapema mnoo.. Acheni uchuro..
Well said brother.Umuhimu wa mtu huthibitika baada ya kufa. Waliokuwa wanashinda mitandaoni wakitukana na kudhihaki uongozi wa JPM sasa wataanza kumkumbuka kinafiki.

Uongozi ni kuwawezesha watu kwa kuwawekea miundombinu ili iwasaidie katika shughuli zao,na Magufuli alifanikiwa kwenye hilo.
 
Watu waliovunja mageti uwanja wa ndege JNA ndio watakaolia mara nyingine ikiwa yataachwa mambo yajiendee

..baada ya wapinzani kushughulikiwa na kuzimwa kabisa, kundi lililokuwa linafuata kushughulikiwa ni wananchi wa aina ya hao waliovunja mageti uwanja wa ndege.

..iko siku waTz waliovunja mageti uwanja wa ndege watachoka kuishi kwa matumaini na ahadi hewa za maisha bora. wataanza kuwazonga watawala na matatizo yataanzia hapo.
 
Wachovu mna wasiwasi kweli, muda wote mmepewa bado mnalalamika hii ndio shida ya kuendekeza watu wanaojiita wanyonge. Na mihela mlikuwa mnajichotea hakuna hata auditing wala bunge kuhoji lakini bado mnalalamika tu. Ndege zinanunuliwa kama mananasi tu , hakuna budget inajadiliwa zaidi ya kusema ndiooooo, na bado mnalalamika tu mwenzenu baar shit alijisemea katika watu wanaokula raha ni yeye sasa nyie wanyonge wengine mlikuwa wapi kula raha au mmesahau raha mlizopata labda niwakumbushe;
1. Mlifurahia sana watumishi kufukuzwa kazi kama mbwa.

2. Mlifurahia kuweka biashara kila sehemu hata mabarabarani bila utaratibu hata kukodi frame za biashara as long una kitambulisho mkaua biashara za wenye frame na walipakodi.

3. Mlishangilia sana manunuzi yasiyofuata utaratibu na kushangilia watu wazima wanapotukanwa hovyo kwa jambo hata dogo tu.

Sasa ni wakati wa waliolia nao kucheka, mbona wenzenu walikaa kimya na mkawa mnashangilia wakakaa kimya ni nini nyie mnapiga kelele nanyi mtulie sasa sindano ziwaingie . Maneno.liyoyatumia yanawarudi Mungu sio Athumani.
 
Hao wanyonge siku zote, miaka yote 6 wameshindwa kujiondoa unyonge baada ya kupata mtetezi ???
Wanasema alifanya mengi zaidi kushinda miaka yote ya wenzake sasa hawa wanyonge si watakuwa ndio matajiri maana alisema wanyonge wataishi kama malaika na matajiri wataishi kama mashetani. Tulishukudia matajiri wakiumizwa sana na tukakaa kimya he hawa wanyonge bado wanalalamikia tu? Tulishasema huwezi kunyanyua uchumi kwa kuwaendekeza wanaojiita wanyonge, wengi wao ni watu wavivu,, wanaopenda majungu na wanafiki wasiopenda kujishughulisha muda wote wao ninwalalamishi tu. Yani ulikosa barabara unalalamika badala ya kujichanga mjenge. Hizi ndio akili za wanyonge naona watupishe sasa tunataka kwenda kadi maana tumerudi nyuma miaka 30
 
Wachovu mna wasiwasi kweli, muda wote mmepewa bado mnalalamika hii ndio shida ya kuendekeza watu wanaojiita wanyonge. Na mihela mlikuwa mnajichotea hakuna hata auditing wala bunge kuhoji lakini bado mnalalamika tu. Ndege zinanunuliwa kama mananasi tu , hakuna budget inajadiliwa zaidi ya kusema ndiooooo, na bado mnalalamika tu mwenzenu baar shit alijisemea katika watu wanaokula raha ni yeye sasa nyie wanyonge wengine mlikuwa wapi kula raha au mmesahau raha mlizopata labda niwakumbushe;
1. Mlifurahia sana watumishi kufukuzwa kazi kama mbwa.

2. Mlifurahia kuweka biashara kila sehemu hata mabarabarani bila utaratibu hata kukodi frame za biashara as long una kitambulisho mkaua biashara za wenye frame na walipakodi.

3. Mlishangilia sana manunuzi yasiyofuata utaratibu na kushangilia watu wazima wanapotukanwa hovyo kwa jambo hata dogo tu.

Sasa ni wakati wa waliolia nao kucheka, mbona wenzenu walikaa kimya na mkawa mnashangilia wakakaa kimya ni nini nyie mnapiga kelele nanyi mtulie sasa sindano ziwaingie . Maneno.liyoyatumia yanawarudi Mungu sio Athumani.
Unataka kusema kutesa kwa zamu

Ova
 
..baada ya wapinzani kushughulikiwa na kuzimwa kabisa, kundi lililokuwa linafuata kushughulikiwa ni wananchi wa aina ya hao waliovunja mageti uwanja wa ndege.

..iko siku waTz waliovunja mageti uwanja wa ndege watachoka kuishi kwa matumaini na ahadi hewa za maisha bora. wataanza kuwazonga watawala na matatizo yataanzia hapo.
Mkuu, walivunja si Kwa sabb nyingine, ni kumsindikiza kipenzi chao hadi kwenye ndege ilipokuwa imesimama
 
Mkuu, walivunja si Kwa sabb nyingine, ni kumsindikiza kipenzi chao hadi kwenye ndege ilipokuwa imesimama

..Ni kipenzi chao kwasababu aliwapa MATUMAINI fulani.

..sasa wale ni watu wa kipato cha chini ktk nchi yetu.

..na ukichunguza serikali haina mpango wowote wa maana wa kuwainua wasogee ktk kipato cha kati, au juu.

..na kila miaka inavyozidi kwenda kundi hilo linazidi kuongezeka haswa maeneo ya mijini.

..hali hii isiporekebishwa tutajikuta tuna tatizo kubwa sana la kiuchumi, kijamii, na kisiasa, hapa Tanzania.

NB:

..Nimeliona kundi hilo likiongezeka toka utawala wa Raisi Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli, na sasa Samia Suluhu.
 
Back
Top Bottom