Masalu Jacob
JF-Expert Member
- Jul 26, 2017
- 1,013
- 1,183
U hali gani Tanzania !
Naomba niweke mchango wangu wa mawazo hapa Jamii Forums.
Napenda kuweka wazo rasmi kwa National Housing Corporation (NHC) kuwa ipewe umakini, umuhimu na umaanani katika ujenzi wa nyumba zote za Makazi na Majengo ya Umma hapa nchini yaani isitokee Raia yoyote afanye ujenzi wa Nyumba ya makazi ball shughuli hizo zote zinafanywe na huyu NHC.
(Nyumba zote za Wananchi zitaifishwe na kuwa Mali ya Shirika (NHC) na Majengo yote ya Umma yataifishwe na yawe Mali ya NHC)
1. Nyumba zitakazo jengwa za makazi ya Umma ziwe za kawaida zenye mahitaji muhimu ya kijamii mfano; maji, umeme, gesi na mawasiliano. Hii baada ya mtaifisho kufanyika. Nyumba zitakazo jengwa zifuate mfumo huo.
2. Nyumba na Majengo yote ya Umma ziwe za kupangwishwa. Yaani asiwepo mtu au watu au taasisi ya Umma wanaomiliki Nyumba za Makazi au Ofisi bali ziwe mali ya shirika.
3. Gharama za malipo kwa hizo nyumba zisizidi Tsh.100,000/= kwa maeneo ya Mjini (Manispaa & Jiji) na Tsh.20,000/= kwa kijijjni (Halmashauri). Hii ni kwa Nyumba za Makazi pekee.
3. Pasiwepo na mikopo ya Nyumba za makazi hapa nchini. Hii ni kwa Nyumba za makazi.
4. Mwananchi/ Raia / Shirika ataruhusiwa na NHC kubuni na kujenga jengo la biashara kwa gharama zake. Kwa upande wa makazi ni hapana. Hii itafaa kwa maslahi ya biashara pekee.
NB
1. Wananchi watakuwa na makazi bora yaliyopangilika vizuri.
2. Nchi itakuwa salama kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na kimazingira.
3. Wananchi watawaza zaidi kufanya kazi na kuliletea taifa maendeleo kuliko kuwaza upuuzi wa ujenzi wa makazi na uchafuzi wa mazingira.
Naomba niweke mchango wangu wa mawazo hapa Jamii Forums.
Napenda kuweka wazo rasmi kwa National Housing Corporation (NHC) kuwa ipewe umakini, umuhimu na umaanani katika ujenzi wa nyumba zote za Makazi na Majengo ya Umma hapa nchini yaani isitokee Raia yoyote afanye ujenzi wa Nyumba ya makazi ball shughuli hizo zote zinafanywe na huyu NHC.
(Nyumba zote za Wananchi zitaifishwe na kuwa Mali ya Shirika (NHC) na Majengo yote ya Umma yataifishwe na yawe Mali ya NHC)
1. Nyumba zitakazo jengwa za makazi ya Umma ziwe za kawaida zenye mahitaji muhimu ya kijamii mfano; maji, umeme, gesi na mawasiliano. Hii baada ya mtaifisho kufanyika. Nyumba zitakazo jengwa zifuate mfumo huo.
2. Nyumba na Majengo yote ya Umma ziwe za kupangwishwa. Yaani asiwepo mtu au watu au taasisi ya Umma wanaomiliki Nyumba za Makazi au Ofisi bali ziwe mali ya shirika.
3. Gharama za malipo kwa hizo nyumba zisizidi Tsh.100,000/= kwa maeneo ya Mjini (Manispaa & Jiji) na Tsh.20,000/= kwa kijijjni (Halmashauri). Hii ni kwa Nyumba za Makazi pekee.
3. Pasiwepo na mikopo ya Nyumba za makazi hapa nchini. Hii ni kwa Nyumba za makazi.
4. Mwananchi/ Raia / Shirika ataruhusiwa na NHC kubuni na kujenga jengo la biashara kwa gharama zake. Kwa upande wa makazi ni hapana. Hii itafaa kwa maslahi ya biashara pekee.
NB
1. Wananchi watakuwa na makazi bora yaliyopangilika vizuri.
2. Nchi itakuwa salama kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni na kimazingira.
3. Wananchi watawaza zaidi kufanya kazi na kuliletea taifa maendeleo kuliko kuwaza upuuzi wa ujenzi wa makazi na uchafuzi wa mazingira.