NHC yanunua eneo la Urafiki lenye ekari 50 na majengo yaliyopo kwa Shilingi Bilioni Tatu

NHC yanunua eneo la Urafiki lenye ekari 50 na majengo yaliyopo kwa Shilingi Bilioni Tatu


Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limenunua rasmi eneo la Urafiki na majengo yaliyokuwa chini ya Kampuni ya Urafiki wa Tanzania na China (Tanzania - China Friendship Textile CO LTD).

Meneja wa Mawasiliano kwa Umma wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya ameyasema hayo wakati wa ziara ya kukagua maeneo mbalimbali ambayo sasa yatakuwa chini ya miliki ya NHC na kufafanua kuwa eneo hili linajumuisha nyumba, maghala, viwanja vya wazi, viwanda na mali nyinginezo.

Katika ziara yake, Saguya alielezea furaha yake na matumaini makubwa kuhusu hatua hii, akibainisha kwamba itasaidia kuboresha miundombinu na kuinua uchumi wa maeneo hayo na kuboresha mandhari ya jiji.

Amesema kuwa NHC, imelinunua eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 50 kutoka kwa mnada wa wazi kikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tatu.

Alisema kuwa, "Kupitia umiliki huu mpya, Shirika la Nyumba la Taifa limejipanga kuboresha maeneo haya ili kuendana na malengo yetu ya kutoa makazi bora na ya kisasa kwa wananchi. Tumeanza kwa kulipima eneo lote na kutambua mipaka yote inayolihusisha eneo hilo.

Eneo la Urafiki lina historia ndefu ya kuwa kituo muhimu cha viwanda na makazi, kikitoa mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania. Hivi sasa, NHC inapanga kufanyia maboresho makubwa eneo hili kwa kujenga miundombinu bora, nyumba za kisasa, na maeneo ya biashara ambayo yatavutia wawekezaji na wakazi wapya.

Shirika la Nyumba la Taifa linaamini kuwa mradi huu mpya utakuwa na manufaa makubwa kwa taifa kwa ujumla, na kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya makazi na maendeleo ya kiuchumi nchini. Katika mpango wa maendeleo ya NHC, eneo la Urafiki litawekewa mkazo maalum kwa ajili ya kuhakikisha kuwa linakuwa mfano bora wa maendeleo ya kisasa na endelevu.

Muungano alihitimisha kwa kusema, "Hii ni hatua muhimu kwa NHC na kwa taifa letu. Tunawaomba wananchi na wadau mbalimbali kuunga mkono juhudi zetu katika kuboresha na kuendeleza maeneo haya kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Wabia wakuu wa kiwanda hicho ni Msajili wa Hazina na kampuni Kampuni ya Urafiki wa Tanzania na China (Tanzania - China Friendship Textile CO LTD).
AISEE MTACHOMWAAA MOTO KHAAA MAJENGO YOTEE YALEEE NA HK ZOTE AISEE NGOJA NKAKOJOE KWANZA
 
Ni Jambo jema serekali haijapigwa sana, kama watu wengi walivyoizoea! Ila Kuna la kujifunza Kwa NHC, wajijue wao Kwa sasa Ndio tegemeo kubwa katika taifa kupunguza makazi holela, ikumbukwe kwenye hili taifa hasa hasa kwenye wananchi wengi kama Dar es salaam makazi holela ni kero kubwa!! Wizara ya Ardhi imejitoa ufahamu, manispaa wamekuwa wakijiona kama sio jukumu lao!! Sasa ujenzi holela unazidi kushamiri. Jaribu kufikiria Jiji kama Dar es salaam 70% Gari la zimamoto haliwezi kufikia nyumba husika kama Kuna dharura ya Moto!!! Na pia 40% watu hawawezi kufika majumbani na magari Yao, au hata kufikisha mizigo majumbani!! Wenye dhamana wameona ni SAWA,
Mimi sikawii kuisifu NHC ila ningependa Hawa NHC wafanye zaidi!! Kununua maeneo yaliyopimwa tayari au yenye hifadhi nzuri hayatufanyi tukaanza kufurahia, wafanye zaidi kununua maeneo kama manzese, Kawe, mikocheni nyuma ya Tanesco, Sinza uzuri, Kwa mtogole, Vingunguti, Na maeneo mengine holela, na kuyafanyia planning na kuyauza Kwa watu binafsi, hii ingesaidia kupunguza makazi holela, tuchukulie mfano kama vingunguti wenye viwanda wameamua kununua maeneo holela na kugeuza viwanda, au Maghala ya viwanda, mfano kiwanda Cha pipe industry, hii ilitakiwa ipate full support ya manispaa na wizara ya Ardhi ila hadi yote haya yamefanyika, Wizara imekuwa haitoi msukumo, je tuelewe wanafurahia makazi holela!? hii imekuwa haina msukomo wowote wa kimkakati, jamani manispaa, Wizara chini ya Waziri Jerry Silaa fanyeni chochote wananchi tuone angalau tujue mnachukizwa na makazi holela, tupo nyuma yenu!!!
 
Eneo kubwa kama hilo tena katikati ya mji kiusalama serikali naona imeona bora ijipigie pande tuu
Eneo ni mali ya serikali na NHC ni mali ya serikali.
Serikali imetoa eneo lake kwa shirika lake ili liweke makazi.
Wangeweza kuuza pesa nyingi kwa sekta binafs, lakini wafanyabiashara wanaweza kuweka bandari kavu, terminal za malori, na biashara nyingine kama hizo, hali hiyo ingeleta vurugu na usumbufu wa magari makubwa kwenye barabara zinazoingia eneo hilo.
NHC inatosha
 
Ni Jambo jema serekali haijapigwa sana, kama watu wengi walivyoizoea! Ila Kuna la kujifunza Kwa NHC, wajijue wao Kwa sasa Ndio tegemeo kubwa katika taifa kupunguza makazi holela, ikumbukwe kwenye hili taifa hasa hasa kwenye wananchi wengi kama Dar es salaam makazi holela ni kero kubwa!! Wizara ya Ardhi imejitoa ufahamu, manispaa wamekuwa wakijiona kama sio jukumu lao!! Sasa ujenzi holela unazidi kushamiri. Jaribu kufikiria Jiji kama Dar es salaam 70% Gari la zimamoto haliwezi kufikia nyumba husika kama Kuna dharura ya Moto!!! Na pia 40% watu hawawezi kufika majumbani na magari Yao, au hata kufikisha mizigo majumbani!! Wenye dhamana wameona ni SAWA,
Mimi sikawii kuisifu NHC ila ningependa Hawa NHC wafanye zaidi!! Kununua maeneo yaliyopimwa tayari au yenye hifadhi nzuri hayatufanyi tukaanza kufurahia, wafanye zaidi kununua maeneo kama manzese, Kawe, mikocheni nyuma ya Tanesco, Sinza uzuri, Kwa mtogole, Vingunguti, Na maeneo mengine holela, na kuyafanyia planning na kuyauza Kwa watu binafsi, hii ingesaidia kupunguza makazi holela, tuchukulie mfano kama vingunguti wenye viwanda wameamua kununua maeneo holela na kugeuza viwanda, au Maghala ya viwanda, mfano kiwanda Cha pipe industry, hii ilitakiwa ipate full support ya manispaa na wizara ya Ardhi ila hadi yote haya yamefanyika, Wizara imekuwa haitoi msukumo, je tuelewe wanafurahia makazi holela!? hii imekuwa haina msukomo wowote wa kimkakati, jamani manispaa, Wizara chini ya Waziri Jerry Silaa fanyeni chochote wananchi tuone angalau tujue mnachukizwa na makazi holela, tupo nyuma yenu!!!

Huu ujumbe ungefanyiwa kazi tungekuwa mbali
 

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) limenunua rasmi eneo la Urafiki na majengo yaliyokuwa chini ya Kampuni ya Urafiki wa Tanzania na China (Tanzania - China Friendship Textile CO LTD) Jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Mawasiliano kwa Umma wa Shirika la Nyumba la Taifa, Muungano Saguya ameyasema hayo wakati wa ziara ya kukagua maeneo mbalimbali ambayo sasa yatakuwa chini ya miliki ya NHC na kufafanua kuwa eneo hili linajumuisha nyumba, maghala, viwanja vya wazi, viwanda na mali nyinginezo.

Katika ziara yake, Saguya alielezea furaha yake na matumaini makubwa kuhusu hatua hii, akibainisha kwamba itasaidia kuboresha miundombinu na kuinua uchumi wa maeneo hayo na kuboresha mandhari ya jiji.

Amesema kuwa NHC, imelinunua eneo hilo lenye ukubwa wa zaidi ya ekari 50 kutoka kwa mnada wa wazi kikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi bilioni tatu.

Alisema kuwa, "Kupitia umiliki huu mpya, Shirika la Nyumba la Taifa limejipanga kuboresha maeneo haya ili kuendana na malengo yetu ya kutoa makazi bora na ya kisasa kwa wananchi. Tumeanza kwa kulipima eneo lote na kutambua mipaka yote inayolihusisha eneo hilo.

Eneo la Urafiki lina historia ndefu ya kuwa kituo muhimu cha viwanda na makazi, kikitoa mchango mkubwa katika uchumi wa Tanzania. Hivi sasa, NHC inapanga kufanyia maboresho makubwa eneo hili kwa kujenga miundombinu bora, nyumba za kisasa, na maeneo ya biashara ambayo yatavutia wawekezaji na wakazi wapya.

Shirika la Nyumba la Taifa linaamini kuwa mradi huu mpya utakuwa na manufaa makubwa kwa taifa kwa ujumla, na kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya makazi na maendeleo ya kiuchumi nchini. Katika mpango wa maendeleo ya NHC, eneo la Urafiki litawekewa mkazo maalum kwa ajili ya kuhakikisha kuwa linakuwa mfano bora wa maendeleo ya kisasa na endelevu.

Muungano alihitimisha kwa kusema, "Hii ni hatua muhimu kwa NHC na kwa taifa letu. Tunawaomba wananchi na wadau mbalimbali kuunga mkono juhudi zetu katika kuboresha na kuendeleza maeneo haya kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Wabia wakuu wa kiwanda hicho ni Msajili wa Hazina na kampuni Kampuni ya Urafiki wa Tanzania na China (Tanzania - China Friendship Textile CO LTD).
CCM HAIWEZI KUTUTOA KWENYE UMASIKINI. Viwanda inaua kisha eneo wanagawana viongozi wa CCM! Wameua Tanganyika Packers wakageuza sehemu ya kuabudu! Tazara wameua wameuza nyumba walizokuwa wanaishi wafanyakazi na karakana imekua shule! Kwa kifupi vyote alivyoanzisha Nyerere wameua badala yake wamewazalisha chawa na viroboto akina Lucas Mwashambwa wawasifie kutwa nzima, huo ndio uchumi wao!
 
Back
Top Bottom