NHC yanunua eneo la Urafiki lenye ekari 50 na majengo yaliyopo kwa Shilingi Bilioni Tatu

Mchakato ulianza siku nyingi wa hilo eneo kwa kuvunja baadhi ya majengo mfano Shule ya Msingi Urafiki ilianza kuvunjwa tokea mwaka juzi wanafunzi wakahamishiwa shule nyingine.

Mimi nataka kupata taarifa ya uhakika kuhusu kiwanda cha Urafiki, kitahamia eneo lingine au ndio mwisho?
 
Kiwanda kilikufa zamani ilibaki kuwa godown tu.
 
Serikali ina pesa za kuchezea urafiki ya bonyokwa inatoa kitita chote hiko, hapo wachina wamelia sana ilibidi wapewe m54
Umeamua kuchangamsha genge au? Eneo hilo la urafiki 1acre sio chini ya $1.5m
 
Sawa kabisa. Ni kama NHC wamepewa tu.
 
Eneo ni la serikali. Na aliyeuziwa NHC na yeye pia ni mali ya serikali.

Mali yako mwenyewe kwa nini ujiuzie kwa bei ghali
Wamesema ulikuwa ni mnada wa wazi. Hii inaua mawazo yako kwa sababu kama ilikuwa ni mdada wa wazi, basi walishiriki watu wengi. (Upande wangu siamini ulikuwa mnada wa wazi kwa sababu bei ya kuuzia ingekuwa kubwa sana). Nadhani aliyeleta habari hakuelewa vizuri au kama wameuza kwa bei hiyo basi kuna mazingira y aupigaji yanaandaliwa, hasa huko kwenye shirika la nyumba. Otherwise kama habari ni sahihi na hakuna makandokando, basi big up, wamefanya vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…