Ni aibu taifa letu kuwa na Waziri wa Nishati anayesisitiza mgao wa umeme bila kutuhakikishia JNHP itaanza uzalishaji lini

Porojo porojo za kipuuzi
 
Porojo porojo za kipuuzi
 
Narudia. Kwenye swala la nishati ya taifa yeyote anaye hujumu kwa namna yoyote huyo ni adui namba moja. Kwa hili Akumbukwe Magufuli. Nitasimama na msimamo huo milele na milele.
Mhujumu wa taifa kwa namuna yote hata akiwa nani lzm hatua za sheria zichukuliwe.
 
Anaulizwa bwawa litakamilika lini anajibu wanatengeneza njia za usambazaji za dola 800

Lugha gongana na Mkuu Pascal unamtetea kabisa... au ww mwenzetu umeelewa nini kwenye majibu hayo ya waziri utusaidie na sisi vichwa ngumu [emoji1787]
Kilichopo ni kwamba huyu waziri na Genge Lake walimchukia Magu sana.

Sasa zile miradi ya Magu zenye tija kwa Taifa lazima zipigwe zengwe tu.

All in all hatuna waziri wa Nishati. Narudia kusema Makamba hafai kuwa Waziri wa nishati.

Lakini sisi wa hali ya chini hatuna la kumfanya ngoja afanye apendavyo, ajisikiavyo

. Akate umeme apendavyo. But naamini machozi ya watanzania itasikiwa siku moja
 
Kama huu mradi hautakamilika kabla ya 2023 bas itaniuma sanaa
 
Huyo ni Social Media Influencer (Hususani JF), ameshapewa bahasha yake tayari kuisafisha wizara mtandaoni.
 
Nadhani Mkataba ni mmoja w kujenga bwawa na distribution lines, anayo ongea makamba hata yeye hajui ana ongea nini, kwake ni matongo tongo pia

Kuna vitu viwili ambavyo tuna takiwa tujifunze watanzania, Kuna wizara Zina hitaji waziri anaejua kwanza vitu vyenyewe, maana yake utazungumza vitu ambavyo una vielewa au uko idea , kingine ni uchapa kazi, so Kuna Makamba , Mwiguru na Nape, hawa ni waongeaji wazuri na wapenda Media, lakini vitendo ni zero,

Nape Kwa wizara yake Ile mambo yanaweza yasiwe magumu maana yeye ni kucheka Cheka na kushika miuno ya wasanii, lakini Kwa Makamba na Mwiguru hizi ni sekta muhimu unahitaji Waziri makini, mchapa kazi na mfuatiliaji na anae jua kitu chenyewe ,sio kuandikiwa na kwenda kusoma kama yalivyo,

Tz shida kubwa maneno ni mengi kuliko vitendo, watu hawako focused, mambo ya repair haya mnaweza fanya hata usiku Kwa kutoa notifications ili shughuli za uzalishaji zisisimame, wao wana chukulia Kila kitu poa na kufanya kazi Kwa mazoea miaka yote, tuna taka matokeo sio mbwembwe, kwanza ni aibu kwa taifa la miaka 60 kuwa na kukatika katika Kwa umeme.
 
Kuna watu wengine wakiambiwa ukweli wanataka walazimishe jambo wanaloliamini wao. Mnataka muambiwe Kama yule eti tunajenga kwa hela za ndani wakati tunakopa?. Na watu wakaamini hivo bila hata kujiuliza? Na ungejifafanya kuuliza sana ungeambiwa umetumwa na mabeberu.
Heshimuni watu wasikilizeni wapeni muda kama walivyoomba.
Lini mimi au wewe hatutimizi malengo kwa muda tuliojipangia.
Mnajua hali ya kisiasa ilivyokua lkn Kila jambo mnalaumu. Why guys? Taifa la kudai kudai in Mwl. Nyerere voice.
Tumepitia njia ya kutimiza matakwa ya mtu mmoja. Jiulize tulipaswa kufanya miradi hii mikubwa ya reli,na bwawa la umeme kwa wakati mmoja kwa uwiano na our real GDP?. Tuna mzingo mkubwa Kama taifa reli kufika mwanza,msongati,Kigoma, nk.
 
Mkuu hapo ulipo kuna umeme?

Huku kwetu wazo, tegeta madale yote hakuna umeme toka jana saa sita usiku. Ngoja tumpe Muda atengeneze mitambo.
 
Nadhani hiyo mitambo ya Tannesco ilikuwa imeoza. Make kila akihojiwa anasema wanafanya marekebisho.

Vinginevyo hiyo mitambo ikiwa mibovu ndiyo inafanya kazi kwa ufasaha. Ana maudhi huyo waziri huyo!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…