Ni basi gani uliwahi panda ukajuta na ukasema hutokaa ulipande tena?

Wababaishaji sana wale jamaa wanabasi lao zuri linaenda Nairobi ndio wanalotumia kuwadanganyia abiria mengine ovyo tu kwa mabasi ya arusha ndio huwa la mwisho kujaza na kuondoka hawana muda maalum wa kutoka kama unamipango yako wanakuharibia hawa jamaa
 
Sasa interview ilikuaje mkuu
Zilikua za utumishi, sikufanikiwa kufanya nilichoma nauli tu na pesa za matumizi tu ingekua kimbelembele ningewashtaki na wangenilipa. Ingekua interview ya taasisi binafsi wangenifanyia maana ingekua shughuli yote inafanyika ofisini kwao ila za utumishi si unajua taratibu zake.
 
Ndio maana niliwahama hao, ule ni kama utapeli pia. Huwezi kunikatishia tiketi kwenye gari A halafu ukanipakie gari B iliyochoka.
 
Miaka kama 6 iliyopita, nilipanda gari moja inaitwa spider kutoka dar kwenda nairobi. Kwakweli nilijuta maana siti zake zilikua zinaumiza mgongo na shingo kimsingi ilikua imechoka sana ile gari.
 
Miaka kama 6 iliyopita, nilipanda gari moja inaitwa spider kutoka dar kwenda nairobi. Kwakweli nilijuta maana siti zake zilikua zinaumiza mgongo na shingo kimsingi ilikua imechoka sana ile gari.
Vigezo gani vinatumika kuvuka mpakani
 
Basi linaitwa Arusha one kutoka Dar-Arusha.. nilileta mzozo wakanishusha kibaha mailimoja baada ya support kutoka jeshi la polisi
Kisa ilikuwa nini mkuuu
 
Vigezo gani vinatumika kuvuka mpakani
Kwa kipindi kile kigezo kikubwa kilikua ni uwe na kadi ya njano ambapo unachomwa sindano ya ugonjwa mmoja nimeusahau jina. Mnazi mmoja ndio wanatoa huduma hiyo Maana mkifika mpakani mnakaguliwa aisee usipokua nayo unaweza rudi ulikotoka
 
Air Msae enzi hizo, Arusha - Dar

Tulipofika tu Moshi stendi pale, safari ikaingia kutu maana gari ikaanza mwaga oil kama mtu anayetapika...

Huku na kule injini ikashushwa na mchezo ukaishia hapo...
Umenikumbusha mbali sana mkuu..hii gari nineipanda mara ya kwanza mwaka 2001 nikiwa bado kijana barobaro..nakumbuka ilikua tukifika kwenye tuta wote tunasimama mana gari ipo speed na viti havina spongy ya kutosha
 
Najimunisa.

Kwanza:: Begi langu nililiweka kwenye buti la basi wakanilipisha.

Pili: Konda alikuwa na kauli mbaya sana kwa abiria na Askari Polisi.

Tatu: Basi ndani abiria walikalia ndoo na vigoda kwenye njiaa ya kupita. Yaani basi lilijaa kupita kiasi.

Nne: Safari ni ya siku 1 lakini tulilala njiani siku 2.
 
Kimotco ya arusha musoma
Hoyo route gari zake zote ni balaa.

Kipindi hicho nilianza kupanda Chacha Manko kutoka arusha tumefika musoma saa 5 usiku, wakati wa kurudi gari mbovu balaa tulifika arusha saa 8 usiku.
Kuna siku ikaletwa marcopolo kufika makuyuni taa haziwaki na giza limeshaingia ikabidi dereva awe anaendesha kwa kufuata magari kwa nyuma na hapo ile barabara ilikuwa inafanyiwa marekebisho.

Coast Line alikuwa masaa ya mbele sana maana kuna siku saa kumi kasoro tumeshafika arusha japo siti zake haina tofauti na kukalia benchi maana zimechoka balaa, Ila kuna siku tulifika musoma muda wa coast line nyingine kuondoka kutokana na kupasua brake drum makuyuni na engine kuchemsha ngorongoro mpaka kifika seronera tuliporekebisha basi ndio tukaanza masaa mpaka kufika musoma saa 11 alfajiri.

Serengeti Liner sikuwahi kupata shida yeyote nayo pamoja na AM dreamline.

Hiyo kimotco nayo si mbaya japo ilikuwa inachelewa kufika na kuna kipindi walikuwa na marcopolo ikawa inachelewa zaidi.

Ila all in all ile route naipenda sana na natamani siku niende road trip nikiwa na usafiri binafsi hasa off-roaders kama land rovers
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…