Ni biashara gani inaweza ingiza atleast faida ya TZS 5M kama nikiwekeza TZS 30M?

Kwa biashara za kuuza bidhaa za jumla huwa faida inapigiwa 20%-25% ya mauzo inaweza pia chini ya hapo kutegemea na aina ya bidhaa.

Twende kwenye hisabati nyepethii

Tufanye makadirio madogo.

kama profit margin tukipigia ya 20%

25/100 * x=5,000,000

x itakua jumla ya mauzo yanayoweza kutupa faida ya 5m kwa PM ya 25%

x= 20,000,000/=

tukigawanya kwa siku 30 tunapata mauzo ya wastani ya 666,666/=

swali linakuja je ni kweli 30m inaweza kukupa mauzo ya 20m kwa mwezi jibu linaweza kuwa ndio na hapana kulingana na aina ya biashara, ila kwa biashara nyingi jibu ni hapana.

Wengine wataongeza zaidi nimepigia kwa makadiro ya kawaida tu yanaweza kuwa sio sahihi pia.
 
mchanganuo mzuri. asante
 
Kama yeye ni businessman inawezekana sana tu ila kama anategemea maoni ya hapa wadau ndo aanze simshauri.

Biashara sio kwenye maandishi kama hivi.
 
kama yeye ni businessman inawezekana sana tu ila kama anategemea maoni ya hapa wadau ndo aanze simshauri

biashara sio kwenye maandishi kama hivi
Ulichoandika ni sahihi, ila hapa tunampa taswira tu ila katika uhalisia anaweza kupata zaidi ya hapo au kukosa zaidi ya hapo kama inavyofahamika katika biashara mpya nyingi, kuna asilimia kubwa zinafeli kwa changamoto mbalimbali na pia zipo zitakazofanya vizuri.
 
Mkuu tafuta wilaya yoyote Tanzania ambayo haijachangamka Wala supply kuwa wengi...nenda azam pakia fullload ya juice mixer energy,malt,ember,ukwaju nakuhakikisha hiyo m5 unaipata oneza hapo ifike m38 maana ndio coast ya semi Zima tan28
Uko sahihi, nili liona hili pia sehemu
 
zitakazofanya vizuri ni only 1%

na i bet huyu mkuu anaenda kuchoma ela
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…