Ni dawa gani ya usingizi wanayoitumia wezi kupuliza madirishani?


Nasikia kuweka maji kwenye ndoo au beseni yana-neutralize hiyo dawa kwani inavutwa sana na maji!
 
Hiyo dawa haifai wadau wezi wanafika wanavuta viti wanakaa wanaorodhesha vitu vya kuiba na bei ya kuuzia
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Nacheka kama mazuri vile.ila daah kweli wahuni sio watu.hivi haya matukio yanatokea mitaa gani.mbona pande hizi sijawahi kusikia wizi wa dizaini hyo
Mkuu, wezi hula makombo,hupakua wali uliolala maarufu kiporo, hula daku nk. Kiufupi ni washenzi sana. Tena hadi kukojoa mkojo kwenye vyombo, kwa ufupi hawana utu
 
Tehe tehe tehe hayo majamaa yaliyokunywa mpaka chai ni 'noma', ukweli lazima tuyapongeze kwa umafia walioufanya kwa sababu huwezi kwenda kwenye nyumba ya mtu kuiba halafu ukanywa mpaka chai ni 'noma'.

Nakumbuka wakati naishi Kunduchi, jirani yetu mmoja alikuwa mfugaji wa bata. Alikuwa na bata wengi kama utitiri. Kumbe basi wazee wa kazi siku nyingi walikuwa wanawamezea mate wale bata.

Siku ya siku wazee wa kazi wakatia 'maguu', nafikiri walitumia hiyo dawa ya usingizi kwa maana siku hiyo usingizi ulikuwa mtamu balaa! Wazee wa kazi kama kawaida yao, wakachukua bata wote hawakuacha hata manyoa...watu tunaamka asubuhi tunakuta banda leupe, dah siku hiyo nilicheka sana kwa sauti ya chini chini kwa sababu wazee wa kazi walikuja na 'kiroliroli'... tuliona tu alama za matairi ya gari, yani wazee wa kazi kwa jeuri walikuja mpaka na gari, ule mngurumo wa gari watu hatukusikia tunakoroma tu, ha ha haa ni 'noma!'
 
Ch
Sasa kama wanatumia hiyo dawa, nini kifanyike ili kuondoa usingizi?
Ikizidi waweza kulala hadi kufa?
Nini zuio?
Chloroform inatabia ya kuwa affirnity to water. Hivyo unapolala hakikisha ndoo ya maji unayo chumani tena iwe wazi na maji mengi. Wakikupulizia hiyo dawa basi moja kwa moja inavutwa kwenda kwenye maji.
Kamwe haitakuathiri, watashangaa tu wakigusa mlango mzee umekurupuka na kulianzisha varangati nao
 
Hao dawa yao IPO, wakiiba mbona watarudisha tena wakilia, dawa ya wezi ni kuwaroga tu Mimi huwa siendi police, iba uone
Dmkali acha utapeli wako huo,wadanganye hao hao wajinga wenzako.Huo utapeli haujaanza Leo sijawahi kuona ujinga huo popote.Mamia kwa maelfu ya kesi za wizi zimejazana mahakamani na mitaani kote nchini kwa nini usiende kufunga kazi uzimalize zote na wewe uwe bilionea kwa kulipwa kwa kazi nzuri uliofanya.
 
Sio mwanamke tu mkuu hata kidume wanaweza legeza marinda.ukiona wamesepa na zagazaga na wewe wamekuacha salama unscathed ni jambo la kushukuru mungu.
Aisee nimecheka [emoji1] [emoji1] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji126] [emoji126] [emoji126] [emoji126]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…