Ni dawa gani ya usingizi wanayoitumia wezi kupuliza madirishani?

Ni dawa gani ya usingizi wanayoitumia wezi kupuliza madirishani?

Hao dawa yao IPO, wakiiba mbona watarudisha tena wakilia, dawa ya wezi ni kuwaroga tu Mimi huwa siendi police, iba uone
Nigawie mm walinichapa Mfuko mzima wa IT equipments , external hard disc ya Terabit 1/na mazagazaga kibao to a May mganga ananiambia vitarudi subiri
 
Daah!!!kuna jamaa yetu mwez uliopta alifanyiwa mchezo huo wakamchukulia lak mbili na cm yenye laki nane kweny tigopesa alipoamka kakuta vitu vimetimuliwa cm na pesa havipo bahat nzur pesa iliyokua kwenye cm aliipata ila baada ya cku nne akaanza kusumbuliwa na kichwa,bahat mbaya mwez huu amefarik hsptl ya muhimbili baada ya kugundulika ana KANSA YA UBONGO.
So Sad.

Dah, marehemu, kuna uwezekano dawa ili muathiri sana. Kwa ufupi tuseme hiyo dawa ni sumu tena sumu kali inayokumaliza taratibu!
 
Ipo dawa ya spry pia ipo dawa ya asili yapo majani jina siyajui ila kw macho nawajua hayo majani yakiwa mabichi ukiyapikicha hutoa harusi ya kinyesi basi ukitaji yatumia huyakausha kisha yakikauka mwezi akija huyachoma nnkurusu ule moshi upenyeze ndani yani ukivuta tu ile harusi unakuwa nusu kaput ndani ya masaaa mawili

Ili kuepuka wizi wa namna hii unashauriwa kuwa na maji ndani either kwenye jagi au kikombe maji yawe wazi kwani inasemekana spry yoyote ile au moshi wowote ule ukifulizwa sehemu ambapo maji yapo wazi ile dawa hukimbilia kwenye maji kwanini miye sijui ila nimepata huu uzoefu kwani tuliishi maeneo ambayo wizi wa namna hiyo ulikuwepo mkubwa sana na kina pekee ilikuwa kulala na maji ndani
 
Salaam jf.

Nilikuwa naomba uzoefu wenu wana jf, hasa katika hizi dawa wa wanazotumia wezi kuwaibia raia wema kuwapulizia madirishani wakati wa usiku wanapolala, kwanza nilikuwa nataka kufahamu jina lake na pili wapi wanapozipata lengo si kwa ajiri ya matumizi binafsi lengo ni kufahamu. Sababu wizi wa kuvunjiwa milango na madirisha umekithiri kibaya zaidi wezi wanathubutu kuwaibia walala hoi hadi maafisa wa serikali wenye silaha, juzi kati mh. Fulani ambaye anacheo kikubwa tu serikalini alipigwa vitu vyake vyote sebureni na mwengine kasafishwa sebure yote na watoto wa mjini, akiwemo pia mwanajeshi mstaafu nae alivunjiwa nyumba na wezi kusafisha sebure lakini kabla ya kuiba wezi walikunywa chai iliyokuwa sebureni na kuondoka. Inavyooshesha hii dawa inawapa kiburi sana, usishangae hadi usalama huwa wanapigwa.

= ajili
=sebuleni
= sebule
 
Daàaaah, umenikumbusha jirani yangu alinunua TV ya m1.25 na subwoofer la nguvu katumia wiki moja wezi wakaja wakawapulizia wakalala usingizi hadi tunawaamsha saa tano asubuhi baada ya kuona kimya sana hiyo nyumba hali tumegana nao usiku wa kulala na hawakuwa na safari yoyote.
Kuwakuta ndani wakaamka kila mmoja akitokea chumba tofauti wezi walibeba na kuwatenganisha mke na mme na kupeleka vyumba tofauti. Wezi ao hao walikula msosi kwanza ndo wakabeba mzigo na hela kidogo iliykuwa around.
Wezi wa namna hii washenzi sana ila dawa yao ni ndogo tu wanapuliza lakini wanakukuta uko macho unakimbizana nao.
 
Back
Top Bottom