Ni faida gani ataipata Mungu kwa kuwachoma moto binadamu siku ya mwisho?

hyooo kama inaukweli ndani yake

ur a great thinker
 
Huu Uzi utajenga wengi na kubomoa wengi
 
Chunguza sana njia zako za fikra.
Na hakika mshahara wa dhambi ni mauti.
Katika ulimwengu wa kawaida unavuna ulichopanda. Vivyo hivyo ktk ulimwengu wa kiroho.
Na ktk ulimwengu wa kiroho unapanda na kuvuna wapi? Ndugu unapanda ktk mawazo na fikra zako.
 
Tumuache Mungu aitwe Mungu
Atakacho amua yeye ndicho sahihi kwetu

Yeye ndo mwamuzi wa kila kitu


Na ni vizuri atoe makazi tofauti kwa WAKENGEUFU MOTONI

na WALIOMTII wakaeee PEPONI
 
Fika mbinguni kwanza ndo utamuuliza Mungu, au mwanao wa miaka 6 akikuuliza njia za kujikinga na mimba utamwambia? Kuna vitu huwezi jua mpk ufikie vigezo vya kujua.... Km ww ni mwanaume unaweza je unaweza kuelewa uchungu wa mimba kwa kuhadithiwa? Kua uyaone
 
Nabii MUSSA[a.s] wa kwenye QUR-AN alikua ni miongon mwa manabii waliopata nafasi ya kuongea na MUNGU direct siku moja alimuuliza MUNGU "Ewe MUNGU kwann utawachoma watu ambao umewaumba wewe mwenyewe?!,MUNGU hakumjibu swali hilo kwa mda ule,kikapita ktambo kidogo miez/miaka nabii MUSSA akamua kulima ngano,akaandaa shamba,akapanda na akavuna ngano yake,lakini baada ya mavuno akasafisha shamba na akachoma masalia,mabaki na takataka zote za ngano zilizobak shamban,sasa MUNGU akamuuliza "Ewe Mussa mbona unachoma hizo ngano wakati ulitumia nguvu zako na muda wako mwingi kuandaa shamba,ukatumia malighafi na nyenzo mbalimbali za kilimo,IWEJE LEO UNACHOMA MOTO??"Nabii MUSSA[a.s] akajibu hapana sichomi ngano haya ni masalia na mabua tu ngano safi nimeshaichukua nimeihifadhi mahala pazuri" MUNGU akamwambia MUSSA basi lile swali lako linafanana na hili ""NAMI NITAWACHUKUA NA KUWAWEKA PAZURI WALE WASAFI NA NITAWACHOMA WALE .......!
 
Kwan nabii Musa wa kwenye qur'an na yule wa kwenye biblia wana tofautiana nini??
 
Ni kisa maarufu.. na nadhani jibu ndo hilo majadala umefungwa rasmi

Tuendelea na mada nyingine..!
 
"Na tumeeleza katika hii Qur'an kwa watu mifano ya kila namna, na amekuwa mwanaadamu akikithiri kujadili kila jambo" (Qur'an 8:54)

Kabla sijajibu swali lako, nimenukuu aya ya Qur'an ikiwa na muradi wa kueleza namna mwanaadamu alivyo. Binadamu amekuwa hasimu na mwingi wa kujadili hukumu, amri na muongozo wa kuyaongoza maisha yake licha ya kila kitu kuwa wazi.

Mwenyezi Mungu anasema fanya hiki na kile usifanye, binadamu anahoji "kwani nisipofanya (kilichoamrishwa) ama nikafanya (nilichokatazwa) itakuwaje?

Majibu ni kwamba; ukifanya ulichokatazwa au kutofanya ulichoamrishwa utaadhibiwa. Na utakapoadhibiwa haiwi faida wala haiwi hasara kwa Mwenyezi Mungu bali ni hasara kwa nafsi yako.

Mfano: Wewe unamiliki shamba, ukaamua kuwapa bure wakalima wawili hekari moja moja zenye rutba nzuri na zenye kufanana kwa kila hali. Kisha ukawapa mazao, mbolea na kila kinachohitajika katika kulima kwao kwaajili ya maslahi yao wenyewe.

Kisha mkulima mmoja kati yao akafauta maelekezo na akavuna mazoa mengi kwa faida yake na mwingine hakuzingatia chochote kile, akapuuza na hakuambulia chochote katika zao.

Katika hao wawili unadhani kwa aliyepata na aliyekosa vinamuongeza au kumpunguzia faida yoyote yule mwenye shamba?

Halkadhalika, Mwenyezi Mungu hanufaiki wala hapungukiwa pindi mja anapoonja adhabu kwa kuzembea, kubisha ama kukaidi amri za muumba wake. Kama ambavyo kwa watakaolipwa ujira mzuri hawampunguzii chochote Mungu bali ni faida kwa viumbe wenyewe.
 
asfaghafurulhaaa.........!! kwa upande wangu kama muislamu nisingeliuliza swali hilo kwa kuwa ktk kitabu kitakatufu cha Quran jibu liko. nikikusaidia mwenzangu kwanza unatakiwa ujuwe lengo la wewe kuumbwa na kuletwa hapa Duniani, MUNGU hakutuumba pasi na sababu.baada ya hapo unaweza kuuliza hayo maswali kama hapana budi ukiwa wewe ni muumini wa imani ya uwepo wa MUUMBA WA HII DUNIA.
 
Nafurahi sana Kuona watu wanajiuliza maswali kama haya kweli tunaonesha nia ya kutaka kutoka nje ya box Tuhimize zaidi watoto wetu kusoma ili wajitoe ktk upofu wa kuamini na kutegemea mungu bila kihoji lolote. Elimu Elimu Elimu
 
Mungu hahitaji wala hatafuti faida yoyote kutoka kwa viumbe wake
 
mawazo ya Mungu sio kama ya wanadamu, utavuna ulicho panda, huwezi ukapanda matembele utegemee kuvuna mtama, hapana! MUNGU anakanuni zake, na afanani na akili za binadamu na hajutii kwa lolote, mwingi wa rehema na mwenye huruma unapo kuwa hai lakini ukifa hauta pata tena neema ya kubadili maisha yako,
kumbuka MUNGU akuumba moto kwa ajili ya binadamu, aliumba moto kwa ajili ya shetani na malaika zake, sasa unapo ungana na shetani na kumsikiliza na kumfuata automatically unakuwa mtoto wake.
ndio maana amesema tutubu mapema kabla hatujafa lakini sisi binadamu hatutaki tunafikiri tutaingia mbinguni kwa kulazimisha! ndio hayo mkuu.
 
Ukitaka kutanua mjadala huu uwe mpana zaidi,jiulize kwanza kwanini Mwenyezi Mungu(aonaye yote,yaliyokuwako,yaliyoko na yajayo) aliamua kuumba viumbe huku akijua wapo watakaoasi na kuleta shida katika creation yake?Kwanini hakuchagua kuumba wale tu ambao alijua hawataasi?Can u see any image of God in the likes of Lucifer and his fallen angels?Idd Amin,Hitler,all the weaked people we have today?If not then kwanini Mungu aliendelea na kuwaumba huku akijua haya?Je,Mungu aliumba uovu?Aliumba dhambi?Mungu aliumba viumbe waovu?
 
Majibu ya watu wa Mungu yanagurahisha wanaamini tu na viongozi wao wanakataza sana kuhoji mambo haya ya kidini....
Mtazamo wangu hakuna moto wala kuungua milele Mungu wetu ni wahuruma sana lile ni fumbo tumewekewa tulitatue
 
Musa hakuchoma milele yale masalia..mbona tunaambiwa tutachomwa milele.
enye QUR-AN alikua ni miongon mwa manabii waliopata nafasi ya kuongea na MUNGU direct siku moja alimuuliza MUNGU "Ewe MUNGU kwann utawachoma watu ambao umewaumba wewe mwenyewe?!,MUNGU hakumjibu swali hilo kwa mda ule,kikapita ktambo kidogo miez/miaka nabii MUSSA akamua kulima ngano,akaandaa shamba,akapanda na akavuna ngano yake,lakini baada ya mavuno akasafisha shamba na akachoma masalia,mabaki na takataka zote za ngano zilizobak shamban,sasa MUNGU akamuuliza "Ewe Mussa mbona unachoma hizo ngano wakati ulitumia nguvu zako na muda wako mwingi kuandaa shamba,ukatumia malighafi na nyenzo mbalimbali za kilimo,IWEJE LEO UNACHOMA MOTO??"Nabii MUSSA[a.s] akajibu hapana sichomi ngano haya ni masalia na mabua tu ngano safi nimeshaichukua nimeihifadhi mahala pazuri" MUNGU akamwambia MUSSA basi lile swali lako linafanana na hili ""NAMI NITAWACHUKUA NA KUWAWEKA PAZURI WALE WASAFI NA NITAWACHOMA WALE .......![/QUOTE]
Musa hakuchoma milele yale masalia..mbona tunaambiwa tutachomwa milele.
 
Ufunuo unasema moto wa 'sulphur'
 
Kama kweli kuna free choice kwanin atoe hukuma kwa wanao mpinga?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nafasi ya wanawake bado ipo chini hadi mbinguni wanaenda kutumiwa kama vyombo vya starehe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…