Je, Mungu Atahukumu Watu
kwa Moto wa Mateso?
Je, umewahi kuona mtu akiteswa? Tunatumaini
kwamba hujawahi. Kumtesa mtu kimakusudi ni
jambo lenye kuchukiza sana. Hata hivyo,
namna gani Mungu mwenyewe kumtesa mtu?
Je, kweli anaweza kumtesa mtu? Dini nyingi
zinafundisha kwamba Mungu hufanya hivyo.
Hebu wazia jambo hili lenye kuogofya: Mtu
anakaangwa kwenye kikaangio chenye moto
mkali. Kwa sababu ya maumivu yake makali
analia kwa nguvu sana akiomba ahurumiwe,
lakini hakuna anayemsikiliza. Anazidi kuteswa,
saa baada ya saa, siku nenda siku rudi—
mfululizo!
Hata mtu huyo awe amefanya kosa gani, je,
hungemsikitikia? Vipi yule aliyeagiza ateswe? Je,
kweli ana upendo? Haiwezekani! Mtu mwenye
upendo huwa na huruma naye huwasikitikia
wengine. Baba mwenye upendo anaweza
kuwatia nidhamu watoto wake, lakini hawezi
kamwe kuwatesa!
Hata hivyo, dini nyingi hufundisha kwamba
Mungu huwatesa watenda-dhambi katika moto
wa milele. Tendo hilo linaitwa eti ni hukumu ya
Mungu. Ikiwa ni kweli, ni nani basi
aliyetengeneza mahali hapo pabaya sana pa
mateso ya milele? Na ni nani anayepasa
kulaumiwa kwa sababu ya maumivu makali
ambayo watu wanapata humo? Basi, majibu pia
ni wazi. Ikiwa kuna mahali kama hapo, Mungu
ndiye aliyepatengeneza, naye ndiye anayepasa
kulaumiwa kwa sababu ya mambo
yanayotendeka humo.
Je, unakubaliana na jambo hilo? Biblia
inasema: “Mungu ni upendo.” ( )
Je, Mungu mwenye upendo anaweza kuwatesa
watu kwa njia ambayo hata wanadamu
wenyewe wanaiona kuwa yenye kuchukiza
sana? Haiwezekani!
Fundisho Lisilopatana na Akili
Hata hivyo, watu wengi wanaamini kwamba
waovu wataenda motoni ambapo watateswa
milele. Je, fundisho hilo linapatana na akili?
Mwanadamu anaweza kuishi miaka 70 au 80.
Hata ikiwa mtu alifanya uovu mkubwa sana
maisha yake yote, je, angestahili kuteswa
milele? Hapana. Haingekuwa haki hata kidogo
kumtesa mtu milele kwa sababu ya dhambi
alizofanya katika maisha yake mafupi.
Ni nani anayejua ukweli wa mambo kuhusu
yanayotupata baada ya kufa? Ni Mungu tu
anayeweza kutueleza, naye amefanya hivyo
katika Neno lake lililoandikwa, Biblia,
iliyotangulia kutajwa. Biblia inasema hivi:
“Anavyokufa [mnyama], ndivyo anavyokufa
[mwanadamu]; nao wote wana roho moja . . .
Wote wanaenda mahali pamoja. Wote
wametoka katika mavumbi, nao wote wanarudi
mavumbini.” ( ) Andiko hilo
halitaji moto wa mateso. Wanapokufa,
wanadamu hurudi mavumbini katika hali ya
kutokuwapo.
Ili mtu ateseke, lazima awe na fahamu. Je, wafu
wana fahamu? Hapana. “Walio hai wanajua
kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote
kamwe, wala hawana malipo tena, kwa maana
kumbukumbu lao limesahauliwa.” ( )
Basi, wafu ambao “hawajui lolote kamwe,”
hawawezi kupatwa na maumivu makali ya moto
wa mateso.
Fundisho Hatari
Watu fulani hudai kwamba fundisho la moto wa
mateso, liwe ni la kweli au si la kweli, lina
faida. Kwa nini? Wanasema kwamba fundisho
hilo huwazuia watu wasifanye makosa. Je, hilo
ni kweli? Je, kiwango cha uhalifu katika maeneo
ambayo watu wanaamini kwamba kuna moto
wa mateso ni cha chini kuliko katika sehemu
nyingine? Hata! Kusema kweli, fundisho la
moto wa mateso ni fundisho hatari sana. Je,
mtu anayeamini kwamba Mungu anawatesa
watu atayaona mateso kuwa jambo lenye
kuchukiza? Kwa nini aone hivyo? Wale
wanaomwamini mungu mkatili mara nyingi
huwa wakatili kama mungu wao.
Vyovyote vile, mtu anayetumia akili hawezi
kukubali kwamba kuna mahali penye moto wa
mateso. Hilo ni jambo lisilopatana na akili hata
kidogo. Halipatani kamwe na utu wa
kibinadamu. Isitoshe, Neno la Mungu halisemi
kwamba kuna mahali kama hapo. Mtu
anapokufa, “hurudi kwenye udongo wake; siku
hiyo mawazo yake hupotea.”— .
Adhabu ya Dhambi Ni Nini?
Je, hilo linamaanisha kwamba hatuadhibiwi kwa
sababu ya dhambi zetu? Hapana, sivyo ilivyo.
Mungu wetu mtakatifu huwaadhibu watenda-
dhambi, lakini hawatesi. Nao watenda-dhambi
wanapotubu, yeye huwasamehe. Adhabu ya
dhambi ni nini? Biblia inatoa jibu la moja kwa
moja: “Mshahara ambao dhambi hulipa ni
kifo.” ( ) Uhai ni zawadi kutoka
kwa Mungu. Tunapotenda dhambi hatustahili
tena kupata zawadi hiyo, nasi hufa.
Huenda ukauliza: ‘Je, hiyo ni haki kweli? Kwani,
kila mtu hufa!’ Hilo ni kweli kwa sababu sisi
sote ni watenda-dhambi. Kwa kweli, hakuna
yeyote anayestahili kuishi. “Kupitia mtu mmoja
dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo
kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa
watu wote kwa sababu wote walikuwa
wamefanya dhambi.”— .
Huenda kufikia sasa unajiuliza: ‘Ikiwa sisi sote
hutenda dhambi, na kwa hiyo sisi sote hufa,
kuna haja gani ya kujaribu kuwa wema?
Inaonekana kwamba mtu mwovu hutendewa
sawasawa na yule anayejitahidi kumtumikia
Mungu.’ Lakini sivyo ilivyo. Ingawa sisi sote ni
watenda-dhambi, Mungu huwasamehe wale
wanaotubu kikweli na kujaribu kubadili
mwenendo wao. Yeye hutupa thawabu
tunapojitahidi ‘kufanya upya akili zetu’ na
kufanya mema. ( ) Kweli hizo
hutupa tumaini zuri ajabu.
Thawabu kwa Ajili ya Mema
Tunapokufa huwa hatupo tena. Lakini hilo
halimaanishi kwamba huo ndio mwisho wa
mambo yote. Ayubu aliyekuwa mwaminifu
alijua kwamba angeenda kaburini baada ya
kufa. Lakini hebu sikiliza jinsi alivyomwomba
Mungu: “Laiti ungenificha katika Kaburi,
kwamba ungenificha mpaka hasira yako igeuke,
kwamba ungeniwekea kikomo cha wakati na
kunikumbuka! Mtu akifa, je, anaweza kuishi
tena? . . . Wewe utaita, na mimi mwenyewe
nitakujibu.”— .
Ayubu aliamini kwamba ikiwa angekuwa
mwaminifu mpaka wakati wa kufa kwake,
Mungu angemkumbuka na kumfufua. Hivyo
ndivyo watumishi wote wa Mungu wa nyakati
za kale walivyoamini. Yesu mwenyewe
alithibitisha tumaini hilo aliposema hivi: “Saa
inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya
makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake
na kutoka, wale waliotenda mambo mema
kwenye ufufuo wa uzima, wale waliokuwa na
zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo
wa hukumu.”— .
Ufufuo huo utaanza wakati gani? Kulingana na
Biblia, utaanza karibuni sana. Unabii wa Biblia
unaonyesha kwamba katika mwaka wa 1914,
ulimwengu huu uliingia katika “siku za
mwisho.” ( ) Hivi karibuni,
Mungu ataondolea mbali uovu na kuanzisha
ulimwengu mpya chini ya utawala wa
kimbingu. Watu wengi wanauita wakati huo
‘mwisho wa ulimwengu.’—
.
Kisha dunia nzima itakuwa paradiso
inayokaliwa na watu ambao walijitahidi kikweli
kumtumikia Mungu. Watu waovu
hawatateketezwa katika moto, lakini
hawatakuwapo katika Paradiso inayokuja.
Katika , tunasoma hivi: “Mtu
mwovu hatakuwako tena; nawe hakika
utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo.
Bali wapole wataimiliki dunia, nao watapata
furaha yao tele katika wingi wa amani.”
Je, hayo yote ni ndoto tu? Hapana, ni ahadi ya
Mungu. Katika Biblia tunasoma hivi: “Ndipo
nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha
ufalme ikisema: ‘Tazama! Hema la Mungu liko
pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao,
nao watakuwa watu wake. Na Mungu
mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta
kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo
hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala
kilio wala maumivu hayatakuwapo
tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.’”—
.
Je, unaamini maneno hayo? Unapaswa
kuyaamini. Neno la Mungu hutimia sikuzote.
( ) Tunakuhimiza ujifunze mengi
zaidi kuhusu kusudi la Mungu kwa ajili ya
wanadamu. Mashahidi wa Yehova watafurahi
kukusaidia. Ikiwa ungependa wakusaidie,
tafadhali waandikie ukitumia mojawapo ya
anwani zilizo hapa chini.
Isipokuwa imeonyeshwa vingine, Maandiko
yote yamenukuliwa kutoka katika Biblia
Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.
SOURCE. Mashahidi wa YEHOVA tembea JW.ORG PIA UNAWEZA OMBA UFUNDISHWE BIBLIA NI BURE