Ni gari gani huwezi kununua Wala kumshauri mwingine anunue?

Ni gari gani huwezi kununua Wala kumshauri mwingine anunue?

1. nissan extrail, hii imeshachangiwa na members wengine humu tayari, cha kuongezea tu ni kwamba hizo nissan wenyewe walitoaga tamko kwama walibugi kwenye hizo gari, kuchemsha hilo gari ni ugonjwa mkubwa, labda ubadilishe rejeta uweke kubwa_modification

2. European cars ambazo hazijathibitshwa na wenyewe, kwamba umenunua kwa third part owners kama sbt, kwa mtu, befoward etc..yaani iwe bmw, volvo, honda etc kama umenunua used kwa mtu basi jua asilimia ya kuwajua mafundi wote hapa mjini ni mkubwa sana, nunua hata ikiwa used iwe imethibitishwa iko okay na authourised European car agent wa hayo magari..itakupa garantii kwamba sensor hazijawa bypassed etc etc engine haijawahi chezewa ili kukunusuru otherwise buy 0 km car.
ukitaka kuthibitisha hili nenda kuna mtaa mmoja hapo mwenge kule karibu na mapambano yamejaa mabmw, nenda kinondoni hananasif mtaa wote umejaa rangerover..au tembelea mitaa ya mbezi beach, makumbusho uone bmw na rangerover zimekuwa mapagale..

3. Daihatsu Terrios/ camry...automatic gear box zake mbovu

4. mazda tribute, hyundai , isuzu trooper, bighon, honda oddesy..hamna spare utachina na hela unayo, litaishia kupaki uwani liwe jumba la panya..spare mpaka nairobi au japan
5. Nissan kwa ujumla: ie terrano, navara.. hazikopeshi hizi gari, hazivumilii watu maskini, ihudumie ikuhudumie, ikose maji tu au oil mlimani inakukaangia engine dakika 0 tu..iwekee shock up og ukiweka za 80k wiki tu unayaingia mashimo mazima mazima.

Pendekezo.
Toyota ndo magari yako made for us, yanavumilia, hata ukiyawekea oil ya boda boda yatakuvumilia..nenda milimani mahenge uko utakua toyota corolla ya mwaka 89 inakilometa laki 6 na inapiga kazi mzee.
Uzi huu utanifaa sana huu kwa Next time
 
Nissan Xtrail generation ya kwanza. Binafsi nimemiliki na waliomiliki ambao nipo nao karibu wamepatwa na mauza uza.

Inaweza chemsha isionyeshe kwenye dash, inaweza amua isiwake tu bila sababu ukaita fundi akifika akawasha tu ikawaka na asione tatizo. Unaishia kumlipa usumbufu.

Kuna moja iligoma kuwaka ikashtakia sensor, sensa mpya ikawekwa ikagoma, kila sensor ikiwekwa inagoma ikarudishiwa ya kwake iliyokuwepo mwanzo ikakubali.
Kichefuchefu cha mimba changa ***** 😀
 
Any

Toyota

Toyota

Toyota

Toyota

Toyota

Again

Gari gani kama unaendesha mashine ya kusaga barabarani
 
Wana Jf salaam,

Ikiwa ni weekend tulivu kabisa.
Kama tujuavyo, kumiliki gari sasa hivi ni miongoni mwa vitu vya muhimu sana.

Wamiliki wapya wanaongezeka kila kukicha, na kwa bahati mbaya wengi hujikuta wanamiliki magari ambayo baadae yanakuja kuwapa changamoto na kujutia kabisa, hiyo inatokea mara nyingi kama kipato cha mmiliki hakiendani na aina ya gari analomiliki.

Leo tuambiane ukweli, pengine kupitia uzi huu utakuwa msaada kwa mtu au watu kabla ya kufanya maamuzi ya kuingia kwenye dunia ya umiliki wa gari.

Ni gari gani ambayo hauwezi kumshauri mtu kununua na ni kwanini?
Lamborghini
 
Kwanza mtoa mada elewa kila gari haikosi changamoto zake hasa kama imetengenezwa na wanadamu.Ukilifahamu hiki utakuta kila myu anapendelea gsri kutokana na matumizi yake au mapenzi yake.Ukimiliki gari yeyote uwe na matarajio ya mapungufu pia.Tutafute pesa tu kuyamudu msgsri yetu. Samahani kwa typing errors
 
Back
Top Bottom