Ni halali CCM kufanyia vikao Ikulu?

Ni halali CCM kufanyia vikao Ikulu?

lipo tatizo kubwa na tatizo dogo; kubwa ni matumizi ya raslimali za serikali kwa ajii ya CCM. Watumishi wanaowahudumia ni wa serikali, vinywaji (I suppose) ni vya serikali n.k Lakini tatizo hili kubwa vile vile linakuja pale ambapo muda wa kazi za serikali unafanywa na kiongozi wa serikali kufanya kazi za chama kwenye jengo la serikali.

Ukubwa wa tatizo hili unaweza kuja hivi zaidi - kiongozi wa chama cha siasa (sema cdm) anaweza kuitisha kikao cha chama kwenye ofisi ya serikali na kikahudumiwa na raslimali za serikali? NIna u hakika mkubwa watu wengi watakataa kuwa haifai lakini tukifuata mfano wa Rais leo (na ameshawahi kufanya hivyo huko nyuma tukazungumza) jibu ni kuwa kuanzia sasa ni ruhusa kwa viongozi wa kisiasa (bila kujali vyama) kufanya vikao na mikutano yao sehemu zao za kazi. hili ni tatizo kubwa.

Tatizo dogo - nani atamwambia Rais ukweli huu kwa sababu hili linawezekana kwa sababu moja tu - anayefanya hivyo ni Rais; kiongozi mwingine hawezi kufanya hivyo akaachiliwa!

Hili linatuleta kwenye swali jingine angavu: je Rais anaongozwa na sheria/taratibu nyingine ambazo zinafuatwa na viongozi wengine wa umma? Do we have another set of laws zinazompa Rais impunity rais ya kufanya lolote?

Mwanakijiji umenena iliyo kweli tupu, tukiendelea kunyamazia huu utovu wa nidhamu wa CCM tujue kinachoendelea sasa ni kisemwacho; "Mazoea hujenga tabia" na sasa yametimia imeshakuwa tabia na wanaona wana haki kuyanya watakavyo. Magamba yameshikamana mno vigumu kuchubuka.
 
nadhani hiki kikao hakihusiani na nchi wala hakina faida kwa wananchi .... chama kama chama kina ofisi na kumbi nyingi sana ni kweli wanataka kusema walishindwa au kulikuwa na ulazima kufanyia ikulu??? au walienda kuuza sura kupajua ikulu?
 
katika dunia ya sasa lazima ufanye 'lateral thinking', hebu soma tena posti ya mwanakijiji hapo juu kuhusu tatizo kujenga matatizo

Nimesoma. Hayo ndio mambo tunayolalamika hapa Marekani. George Bush alipokuwa rais, Democrats walikuwa wanasema anatumia F1 kwa safari za kisiasa. Sasa hivi yupo messiah Obama. Yeye anafanya yale ya Bush.
 
Nimesoma. Hayo ndio mambo tunayolalamika hapa Marekani. George Bush alipokuwa rais, Democrats walikuwa wanasema anatumia F1 kwa safari za kisiasa. Sasa hivi yupo messiah Obama. Yeye anafanya yale ya Bush.

kwa hiyo hakuna mbadala? kila atakayekuja atakuwa kama aliyepo? "there is nothing new under the sun" ala king solomon ?
 
je gharama ya kikao hiki imekasimiwa kwenye kitabu cha bajeti 2011/2012?
 
ccccm.JPG


ccccm1.JPG

JK Aongoza Kamati Kuu Ikulu Leo February 27, 2012

Halafu umwachie mtu kama huyu aunde tume ya kuratibu katiba. Afadhali kuendelea kupigania katiba mpya kuliko upumbavu tunaotaka kuufanya under these obvious conditions of one party system supremacy.
 
kwa hiyo hakuna mbadala? kila atakayekuja atakuwa kama aliyepo? "there is nothing new under the sun" ala king solomon ?
there you go. Mrema akishinda urais, mnataka akafanyie mikutano ya chama Ajentina?
 
Ya Luthuli House ni ya Luthuli House !

Unashangaa ccm kufanya kikao ikulu? Hukumbuki harusi ya mdogo wake nyo aliifanyia ikulu na ma-alhaji na hajats? Nchi hii ndiyo tz inayoongozwa na wanaodhani nchi hhi yao (CCM)
 
Kwasababu ya mazingira tuliyonayo sasa, kadri inavyowezekana, shughuli za vyama vya siasa ikiwemo chama tawala, visiingiliane na shughuli za serikali. Tunalipia watu wanaostahili kulipiwa na chama chao wenyewe for no good reason
 
there you go. Mrema akishinda urais, mnataka akafanyie mikutano ya chama Ajentina?

Ndo maana hajawahi kushinda maana imagine foleni atakayoisabisha kwa kwenda agentina,lol!
 
baadhi ya mambo huwa yanafanyika tanzania tu
 
Tatizo nchi hii hatuna mazoea ya kufauata taratibu na sheria kuanzia huyo CITIZEN No. 1.

Mkapa aligombana na Mama Anna Mkapa hadi wakaishia kuvunjana mikono na miguu kwasababu
Mkapa alimkatalia mama Anna Mkapa kumfanyia mtoto wa kufikia wa Mkapa harusi IKULU.

Kama hiyo haitoshi CCM imechukuwa viwanja tulivyojenga kwa nguvu na kodi yetu an kuvifanya
vya kwake kama Vile CCM Kirumba, Ali Hassan Mwinyi etc.

Watu wa ITIFAKI kweli hakuwepo kumsghauri this obvious UKIUKWAJI wa sheria. Next time Mbowe
akiitisha kamati kuu ya CDM kwenye ukumbi wa Bunge itakuwaje?
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Na watakua wamefanya makusudi hii... anyway wananchi wenyewe ndio hao tunahojia kwenye screen zetu
 
Hii ni saratani iliyokaa kwenye ubongo wa magamba! Ni kifo tu.
 
Clinton alikula uroda na Monica Lewinsky wapi? Oval Office.
 
Back
Top Bottom