Ni ipi official anti-malaria Mseto?

Ni ipi official anti-malaria Mseto?

Zipo kwenye maduka ya dawa, japo WHO kweny ripoti ya mwaka 2014,walielezea imepungua makari,... Kuna alternative nadhani ni kuhusisha sulphur ila zinapatikana, kwenye maduka na hospital near you
 
Dawa mseto ya malaria yenye dawa mbili; Artemether na Lumefantrine (ALU), kwa hapa nchini bado inaonekana kuwa na ufanisi mkubwa wa kutibu malaria.
Numbisa tufahamiane basi. Uko wapi? NIMR? Ifakara?
 
Dawa mseto ya malaria yenye dawa mbili; Artemether na Lumefantrine (ALU), kwa hapa nchini bado inaonekana kuwa na ufanisi mkubwa wa kutibu malaria.
Efficacy studies kwa sasa mnafanya wapi? sentinel sites ni zipi?
 
Soma guidelines for Diagnosis treatment of malaria 3rd edition ya WHO (2015),majibu utapata pia soma National Guideline for malaria diagnosis and treatment ya Tanzania, ingawa kwa upande wa Tanzania tuna edition ya 2005 kama sijasahau
 
Kama ni patient ndo ana uliza uoni utakuwa huja msaidia kwaku mwambia asome guidelines for diagnosis treatment of malaria..??
Soma guidelines for Diagnosis treatment of malaria 3rd edition ya WHO (2015),majibu utapata pia soma National Guideline for malaria diagnosis and treatment ya Tanzania, ingawa kwa upande wa Tanzania tuna edition ya 2005 kama sijasahau
 
NI IPI OFFICIAL ANTI-MALARIA MSETO ?

1. Artemether + Lumartem ?

2. Dihydroartemisinin + Piperaquine
Mchanganyiko wa Artemether na lumefantrine ndio unao tumika zaidi kwnye guidelines ya trearment of malaria Tz
Japo mara nying mtu uanza na injection (sindano) 3 za Artemether evry 8 hrs last 24 hrs.
Then mseto wa( ALU). Kama drugs of choise.
Quinine ndo last option ya MP( malaria parasite)
 
Kama ni patient ndo ana uliza uoni utakuwa huja msaidia kwaku mwambia asome guidelines for diagnosis treatment of malaria..??
Swali lilivyoulizwa,anayeuliza anaonekana ana mwanga wa mambo ya tiba, nikuulize wewe pia kwani kusoma references ukapata mwanga ni hatia? au elimu ya tiba ni siri kubwa sana amabayo muulizaji hatakiwa kupata ufafanuzi kutokana na kusoma miongozo ya Mamlaka zinazohusika,sijakueelewa lengo lako ni lipi,kumuelekeza pa kupata official clarification? Nahisi ungekuwa ni mtengenezaji wa dawa basi usingeweka hata leaflet ndani ya product zako ila ungeaandika namba ya simu yako tu wakitaka ufafanuzi wakupigie.
 
ALu 1st line for uncompicated malaria
DPQ 2nd for uncomlicafed malaria
 
Nadhani dawa ya malaria kuwa official au sio official ni siasa. Dawa inayokutibu na kuondoa vimelea vya malaria ndio dawa official kwako. Kwa hiyo inaklazimu ujue dawa ambayo ni tiba kwako.
 
Mchanganyiko wa Artemether na lumefantrine ndio unao tumika zaidi kwnye guidelines ya trearment of malaria Tz
Japo mara nying mtu uanza na injection (sindano) 3 za lumefantrine evry 8 hrs last 24 hrs.
Then mseto wa( ALU). Kama drugs of choise.
Quinine ndo last option ya MP( malaria parasite)
Jiridhishe tena,guideline ya matibabu ya malaria imekaa hivi? Dawa ya msingi kwa malaria kali(Severe but not complicated) ni Artesunate injection inatolewa kwa njia ya mishipa au kwenye nyama (itramascular)amabayo kwa Watu wazima na watoto wenye uzito wa zaidi ya kilo 20 hutolewa kwa 2.4mg/kg body weight katika 0 hour ,12 hour na kwa saa ya 24 kisha mgonjwa anaendelea na Dawa za kumeza endapo hatakuwa akitapika ,na kwa watoto walio chini ya kilo ishirini (infants & neonates) dose yao inakuwa ni kubwa kidogo ni 3.0 mg/kg body weight hii ni kulingana na maelekezo ya wizara.Kwa malaria isiyo kali ni Dawa ya msingi ni dawa mseto (ACTs)-Artemisinin Combination therapy (Artemether + Lumefantrine), kwa bandiko lako hapo juu Sindano za Lumefantrine plain kifupi sijawahi kuiiona kwenye ulimwengu wa tiba na hata kwenye muoongozo wowote ule duniani kwenye matibabu ya malaria au imetoka jana ,au ulitaka kumaanisha Artemether inection? kama ni artemether basi huwa haitolewi in every 8 hour in 24 hours utamuumiza mgonjwa ,hii huwa inatolewa kila baada ya 24 hour,ukiaanza na loading dose 3.2kg/body weight kisha kwa siku zinazofuatia ni 1.6mg/kg body weight kama mainatanace/shunting dose,amabapo waweza kutoa kama tiba kamili kwa siku tano au kwa siku moja kisha mgonjwa akaendelea na tiba kwa kutumia dawa mseto.
Niko wazi kusahihishwa elimu ya Tiba ni pana.
 
Nadhani dawa ya malaria kuwa official au sio official ni siasa. Dawa inayokutibu na kuondoa vimelea vya malaria ndio dawa official kwako. Kwa hiyo inaklazimu ujue dawa ambayo ni tiba kwako.
Principals are not social worship,Sheria na mioongozo ipo hata kama huifurahii lazima ifuatwe.
Kuna watu wamefanya tafiti za kina na kutengeneza mioongozo hii wala si siasa.
Mfano Tanzania ilipoacha kutumia Chloroquine mwaka 2001 Agust na kuaanza kutumia Sp,ni miaka kama minne tu dawa hii ya Sp ilishindwa kupambana na vimelea hivi kwa karibu asilimia 25.5,Second line yake ilikuwa ni Amodiaquine nayo ilioonyesha kushindwa kwa asilimia 12.WHO inasema dawa yoyote inayoonyesha resistance kwa takribani asilimia 25 kwenye kutibu malaria ni ishara tosha kuonyesha hitaji la mabadiliko katika Tiba ya Malaria.
Mapendekezo yalikuwa mengi ikiwa ni pamoja na kuwa na combination ya Sp+Amodiaquine,Artesunate +Amodiaquine ,Pamoja na Artemether + Lumefantrine,Tafiti za kina ziliendelea kulingana na miongozo ya WHO,na mwishoni tukapata muoongozo tunaoutumia hivi sasa.
ACT/ALU= Dawa mseto ,pamoja na Quinine kama dawa ya malaria iliyo kali na malaria kwa waja wazito.
 
Injection ni Artemether mchanganyo kidogo. Kuhusu mg/kg ni swala dogo ata nurse wana lijua. Ila moja kwa moja kwaku andka mg/kg za Adult& infant ina onysha ume soma mahali naku andka na ndio maana unasema injction inatolewa evry 24. Injection hutolewa every 8hrs last ndo 24 hii ni baada ya patient kuonekana hayuko response to quinine therapy ivyo tuna ifafanua kama persistence of clinical features of severe malaria
Or failure of reduction of parasites after 3 days of treatment.
Hapo ndipo tunapo switch to Artemether injection 3.2mg/kg loading dose i.m followed by 1.6mg/kg im kwa 6 days kama huto mchoma 3.
kilicho andkwa kwnye guidelines au kwnye module sicho kinacho tumika kazini 100%. Yote ya yote uko vzr na ume andka vizuri @selekwa.
 
Injection ni Artemether mchanganyo kidogo. Kuhusu mg/kg ni swala dogo ata nurse wana lijua. Ila moja kwa moja kwaku andka mg/kg za Adult& infant ina onysha ume soma mahali naku andka na ndio maana unasema injction inatolewa evry 24. Injection hutolewa every 8hrs last ndo 24 hii ni baada ya patient kuonekana hayuko response to quinine therapy ivyo tuna ifafanua kama persistence of clinical features of severe malaria
Or failure of reduction of parasites after 3 days of treatment.
Hapo ndipo tunapo switch to Artemether injection 3.2mg/kg loading dose i.m followed by 1.6mg/kg im kwa 6 days kama huto mchoma 3.
kilicho andkwa kwnye guidelines au kwnye module sicho kinacho tumika kazini 100%. Yote ya yote uko vzr na ume andka vizuri @selekwa.
Let us stop there,nahisi bado uko College haujaanza ku-practise siku moja utaelewa , jinsi ulivyo comment hapo juu ni idea dhaifu kabisa katika tiba ya malaria na sidhani kama iko kwenye guideline yeyote ile kwenye ulimwengu wa tiba ya malaria,ila chukulia kama sehemu ya kujifunza dont be so rigid nimeoongelea dawa mbili Artemether & Artesunate kama hutajali kasome Dose & administration, solubility zake zote na pia limitation ya kutumia Lumefantrine through Iv/Im route, HATUNA SINDANO YA LUMEFANTRINE TANZANIA Hakuna Di-amino pyrimidine derivative (Lumefantrine plain) injection kwa matibabu ya malaria,Dose ni kipimo makini cha kutofautisha dawa kama tiba au sumu,usirudie kusema dose ni jambo dogo,kama ni mwana taaluma wa Tiba huitendei haki taaluma yako.Hapa ndipo wazungu wanapotuzidi umakini tunapofanya negligence kwa vitu ambavyo ni very critical.
Huwezo kujua bila kusoma au kutenda kama, vyote nilivyoviaandika ni kweli nilivisoma ingawa ni miaka mingi kama wewe hupendi kusoma utakuwa unaiingia chaka kila siku maana hata artemether unasema ni mchanganyiko kidogo sijui wa nini na nini,?Ok sijajua refereance mnazotumia siku hizi mnazipata wapi.
Hatutakiwa kukariri kuwa tunajua inatakiwa tujiridhishe kweli tuko sahihi au bado tunatakiwa maarifa zaidi.
 
Back
Top Bottom