Ni kama tumekuwa fooled kusahau kuwa UKIMWI bado upo

Ni kama tumekuwa fooled kusahau kuwa UKIMWI bado upo

Inasikitisha labda kwa sababu siku hizi kuna ARV, Maana kipindi hicho ilikuwa hakuna ARV so ukipata HIV lazma ujiandae kisaikolojia aisee Maana hakuna Dawa..

Dawa zimeanza kuingia miaka ya 2010s...
So Ndo maana wengi wana Jeuri maana Wamatumia Dawa so ni Vigumu kumjua..
Na hakuna Anayepona Ukimwi wanawadamganya Tu
Wanakwambia wanaogopa Kisukari sio UKIMWI
 
[emoji444][emoji444][emoji445]Usione soo Sema naye, Kuhusu Kusubiri ,Kuwa mwaminifu au Tumia kondom..[emoji445][emoji445]

Ishi campaign..
View attachment 2927239
Aisee... umenikbusha Kampeni hii...
Kawimbo kalikuwa kanapigwa vizuri sana kukumbusha watu juu ya janga la AIDS...

Enzi za Ben Mkapa... akiwa President..

Miaka ya 2003 na 2004 hivi...
 
Yani vijana sasa hivi ni kavu kavu huku wakiwa na fikra ya kuchukulia aids kwa uwepesi sana.

"aaah huyu haonekani kama ana ukimwi".

"aaah siku hizi sio kama zamani ukimwi haupo kirahisi rahisi".

Kama tunavyo amini siku hizi tunaweza kupatiana UTI kirahisi basi hivyo hivyo HIV/AIDS inakukamata kirahisi tu.

USE CONDOMS.
Kuna wale jamaa wa Telegram, yaan hamna anayevaa kondomu
 
Inasikitisha labda kwa sababu siku hizi kuna ARV, Maana kipindi hicho ilikuwa hakuna ARV so ukipata HIV lazma ujiandae kisaikolojia aisee Maana hakuna Dawa..

Dawa zimeanza kuingia miaka ya 2010s...
So Ndo maana wengi wana Jeuri maana Wamatumia Dawa so ni Vigumu kumjua..
Na hakuna Anayepona Ukimwi wanawadamganya Tu
ARVs zimeanza kutolewa 2004 au 2005 sio 2010's
 
ARVs zimeanza kutolewa 2004 au 2005 sio 2010's
Uko sawa kabisa mkuu!
Pengine sikufafanua zaidi..
Ila uko sawa kabisa ARV zimeanza kutolewaa mwaka 2004 mwezi wa 10 baada ya Tanznia kufikia Waathirika 1.2 Million..

Lakini Naomba kuongezea kidogo..
Kwanza kabisa mwaka huo Huduma za Matunzo (CTC) zilizolaunch dawa ya ARV zilikuwa Chache sana Nafikiri zilikuwa Hospitali za kanda na Hospitali ya Taifa..

Na mwaka 2006 Walishuka mpaka Hospitali za wilaya nazo zikawa zinatoa Huduma ya Matunzo na Tiba(CTC).. na vilikuwa vituo 96 tu Tanznia nzima..

NA report za wagonjwa zilikuwa zikitumwa Hospitali ya Taifa kwa ajili ya kutoa report rasmi ya wagonjwa wote ili kuongeza dawa..

Ilikuwa Vyepesi sana Kuhudumia Wagonjwa wa HIV ambao hawana AIDS kwa sababu kipindi hicho walikuwa hawapewi dawa Mpaka CD4 Ziwe zimeshuka kabisa kama CD4 zilikuwa Hazijashuka Bhasi ilikuwa wanapewa Only Ctx (Septrin/Cotrimoxazole) ili kuzuia magonjwa Nyemelezi..

Na mwaka 2008 Only 13% Ndo walioanzishiwa dawa ya ARV..

Na ilipatikana bahati ya kushuka mpaka vituo vingine vya Chini na Kupatikana vituo 210 tu vinavyotoa huduma ya Tiba na Matunzo..

Na hata Dawa zilizokuwa Zikitolewa zilionekana bado ni chanzo cha kupatikana kwa Drugs Resistance hence drugs failure..

Dawa zilianza kuwa Available Bila shida miakaa ya 2010s na hasa kuanza kutumika kwa Dawa zisizokuwa na burden kwa watu na zenye mauzi machache na Huduma ilikuwa Available na affordable kwa watu wengi..
Mkuu..

Hiki ndo nilichomaanisha
 
Yani vijana sasa hivi ni kavu kavu huku wakiwa na fikra ya kuchukulia aids kwa uwepesi sana.

"aaah huyu haonekani kama ana ukimwi".

"aaah siku hizi sio kama zamani ukimwi haupo kirahisi rahisi".

Kama tunavyo amini siku hizi tunaweza kupatiana UTI kirahisi basi hivyo hivyo HIV/AIDS inakukamata kirahisi tu.

USE CONDOMS.
Hivi kale kakifaa kakujipima mwenyewe kanauzwa sh ngapi 😢
 
Vyote vinasababishwa na ngono zembe,so bado mzembe hachomoki!
kwenye homa ya ini risk ni kubwa sana jasho la mgonjwa wa ini mkigusana umenasa haiambukizwi kwa ngono tu ni vile Mungu anatulinda na wala hatuna habar
 
Watu wengi umri ulioenda wanakunywa dawa kila siku
Watu wenye pressure wanakunywa dawa kila siku
Watu wenye colestrol wanakunywa dawa za colestrol kila siku
Watu wa kisukari wanakunywa dawa kila siku
Wanakunywa hata mbele ya umati bila kujificha ficha.
 
Mkuu unaweza ukawa sawa ila usiwe sahihi..
Ishi campaign ilizinduliwa Mwezi wa 11 mwaka 2001 na Waziri Mkuu wa Enzi hizo Fredrick Sumaye..
Na waliamza kuzindua Dar, Dodoma wakazindua December 2001..
Wakamalizia Iringa maana ndo kulikuwa na maambukizi makubwa January 2002..

Ila hayo mabango yote yalianza kuwekwa mwaka 2002 kama sijasahau mwezi June 2002, Mwisho wa mwkaa wa serkali 2001/2002..

Redioni ilianza mwaka 2002 na Nyimbo zilitungwa mwaka wa fedha 2002/2003..
Ile nyimbo ya usione soo ilitungwa 2003 mwezi wa nne
Umemrekebisha jambo gani katika aliyosema? Upande wa kutokuwa sahihi
 
Watu wengi umri ulioenda wanakunywa dawa kila siku
Watu wenye pressure wanakunywa dawa kila siku
Watu wenye colestrol wanakunywa dawa za colestrol kila siku
Watu wa kisukari wanakunywa dawa kila siku
kaka kuna mahali umepotosha, si wote wenye visukari na age wanakunywa dawa kila siku. Kisukari si dawa kila siku, age si dawa kila siku. Ni wanatumia muda fulan basda ya hapo wanaacha na kuendelea na maisha.
Lakin hiyo sio justification against aids
Wanasema siku hizi hawaogopi Ukimwi wanaogopa Kisukari, wengi watakwambia Ukimwi haupo ndio maana wanatoa ushuhuda feki kwa mitume na manabii feki/wa mchongo eti wamepona HIV
unajua dini zina pumbaza, unlike ukimwi kisukar unaweza kuku reverse ukapona kabisa japo inahitaji jitihada. Ila ukimwi ni CHapa ya milele. Hao wanao puuza ndio wasambazaji
Watu wengi umri ulioenda wanakunywa dawa kila siku
Watu wenye pressure wanakunywa dawa kila siku
Watu wenye colestrol wanakunywa dawa za colestrol kila siku
Watu wa kisukari wanakunywa dawa kila siku
si kweli watu wenye visukari wanakunywa dawa kila siku, i have close people naishi nao even wengine kuwapeleka hospital. Wengi sikuizi wana fuata special diet si dawa. Na pia inategemea umefika level gani. kuna level kisukar unaweza kuki reverse ukarudi normal
Na pia si wenye old age wanakunywa dawa kila siku, asilimia ndogo sana the rest but all in all magonjwa kama hiyo sio fun kabisa, yasikukute
 
Vitabu vitakatitifu na babu zetu hawakuwa wajinga kutuasa tuoe (hasa bikra) na tuikwepe zinaa, yani sex ni ruhusa ila tufanye na watu tunaoaminiana, kila moja ana jukumu la usalama wa mwenzake pamoja na familia.

Haya magonjwa yamewekwa pabaya sana, shuguhuli ya dakika kadhaa inakupa majuto mpaka kifo.
Zama zimebadilika zamani ngono haikuwa burudani
 
Na ukipata ukimwi zile kazi kubwa kubwa za mshahara mzuri huwezi kupata tena
 
Back
Top Bottom