Ni kitu gani kilikupelekea mpaka ukajiunga na mtandao wa jamiiforum

Ni kitu gani kilikupelekea mpaka ukajiunga na mtandao wa jamiiforum

Nilianza kufuatilia JF ikiitwa Jambo forums miaka ya 2006, mleta mada ulikua na umri gani kipindi hicho? Mwaka 2008 nikawa member, so hadi Leo Nina miaka 13 humu ndani as a registered member na nimekua ONLINE na mchangiaji kwa miaka yote hio
Aisee mkuu hongera yani kipindi icho mimi bado kinda kabisa sielewi chochote pia nyie wakongwe ndo mmefanya jf imekua kimbilio la wengi hongera sana mkuu
 
Aisee huyo nae alikua na maringo sasa au alikua kakolea kwa mumewe
Kutokana na comments zake nyingi, ni binyi fulani mwenye maadili sana, na hata hapa jukwaani hakuwa mtu wankujichanganya sana kwenye mambo ya kipuuzi ila anaonekana ni msomi na mwrlewa wa mambo
 
Kutokana na comments zake nyingi, ni binyi fulani mwenye maadili sana, na hata hapa jukwaani hakuwa mtu wankujichanganya sana kwenye mambo ya kipuuzi ila anaonekana ni msomi na mwrlewa wa mambo
Duh itakua kweli kama usemavyo maana wangekua hawa wanawake wengine angekuchangamkia pia sema humu jf mpaka mdada akujibu message nahisi mpaka uwe maarufu humu.
 
Binafsi nilikua nasoma Jamii Forum kama guest lakini kuna dada alinivutia sana sijui siku hizi yupo wapi, nilijikuta ninampenda yule dada kuanzia naman anavyowasilisha mada, anavyochangia katika majukwaa mbalimbali na hata vile anavyojielewa, she was the best yani nilikua mpaka natamani nimpate nimuoe kabisa
Mwaka 2014, nikaamua kujiunga Jamii forum ili nijiweke karibu na huyo dada, nilitumia mbinu zote kumpata ila nikagonga mwamba kwanza hata PM alikua hajibu , sikumoja nikajitosa kumfungulia uzi, wakati uzi unatrend huyo dada akapotea hapa jukwaani moja kwa moja sijui aliamua kuikimbia JF au ana ID mpya, nilitamani niondoke JF moja kwa moja lakini najipa moyo kwamba atarudi
Duuh we jamaa si uliambiwa yule ni Mwanaume lakini au
 
Nakumbuka mwaka 2016 kipindi icho nikiwa kidato cha 3 nilipata demu flani hivi na kusema ukweli nilitokea kumpenda sana huyu mwanamke, kiasi kwamba nikawa namchunguza maana nilihisi uwenda akawa anatoka na wadau wengine, hali hii ilinipelekea nikawa nagoogle sana kuhusu dalili za mwanamke anaekupenda, mara nagoogle dalili za mwanamke mwenye wapenzi ya mmoja, sasa katika kugoogle nikawa napata majibu ambayo yanayonipeleka moja kwa moja kwenye jukwaa la mapenzi, hivyo nikawa mlevi wa jukwaa la mapenzi.

Pia mwaka 2018 kipindi nipo A level nikapata tena demu mwingine aisee nae nae nilimpenda sana na nikawa namfatilia sana hivyo nikajikuta nagoogle sana mada za mapenzi ambazo majibu yake nikawa nayapata kwenye jukwaa la mapenzi nahisi kwa watu wanaongoza kufatilia mada za mapenzi ni mimi maana nilikua kama mlevi tena wa mapenzi.

Mwisho kabisa siwezi kusahau jukwaa la mambo ya technology maana nilikua nalifatilia sana mambo ya simu, laptop na games mbali mbali, naweza kusema kwa kifupi mambo ya mapenzi na technology ndio yamenileta humu jf.

Karibuni sana wadau na nyie mueleze sababu zipi ziliwapelekea mpaka mkajiunga na mtandao wa jamiiforum.

NAWASILISHA.
Kuna bro wangu mmoja alikua anatumia jamii forum na jukwaa lake pendwa lilikua ni la jokes so tukiwa tumekaa nae anakua anasoma na tunacheka kwel na ndo alinishawishi sana kuingia hum lakin me baada ya kuingia hum nilipenda sana jukwaa la technology maana najifunza vitu vingi sana
 
Duuh we jamaa si uliambiwa yule ni Mwanaume lakini au
Hakuwa mwanaume, mimi nimeshakwambia nimemfuatilia for 6 yrs angekua mwanaume ningegundua tu sema tu hakua interested na mimi
 
Wewe jiulize kwanini Hakujibu pm zako
Akishaweka wazi kwamba ameolewa na ana watoto, pengine hakutaka kujiingiza kwenye mahusiano au aliniona lofa you never kno, au labda sikua type yake, hawa wanawake wana mengi mkuu
 
Kuna bro wangu mmoja alikua anatumia jamii forum na jukwaa lake pendwa lilikua ni la jokes so tukiwa tumekaa nae anakua anasoma na tunacheka kwel na ndo alinishawishi sana kuingia hum lakin me baada ya kuingia hum nilipenda sana jukwaa la technology maana najifunza vitu vingi sana
Yaah jukwaa la technology ni zuri pia linasaidia sana maana kuna wabobezi mule
 
Me ni ushakunaku tu ulinileta nilikua na tabia ya kujua kila kitu kwenye simu kuna siku niliingia FB then nikaingie free mode nikakutana na vifile file huko sijui elim afya bbc nikavipitia vyote nijue mara nikakutana na jamiiforus nikazama huko ilikua 2015 nikanogewa ndio nikajiunga
 
Me ni ushakunaku tu ulinileta nilikua na tabia ya kujua kila kitu kwenye simu kuna siku niliingia FB then nikaingie free mode nikakutana na vifile file huko sijui elim afya bbc nikavipitia vyote nijue mara nikakutana na jamiiforus nikazama huko ilikua 2015 nikanogewa ndio nikajiunga
Aisee alafu watu wanaojiunga jf uwa ni wajanja wajanja kidogo mkuu yani wale wanaotaka kujua vitu ila hongera mkuu
 
Back
Top Bottom