Ni kitu gani kinakukata Sitimu unapotaka kumtongoza mwanamke

Ni kitu gani kinakukata Sitimu unapotaka kumtongoza mwanamke

Hapa kwetu Njombe Mwez wa kumi na mbil mwaka 2021 nilikutana na binti flani ambaye kwa macho yangu namuona mzuri Sana, nlimuelewa sana yule dada. Alikuwa anapita sana kwenye kachochoro ambako ndipo ofisi yangu ilipo.

Basi ikawa kila akipita namuangalia sana naishia kusema kesho ntamsimamisha ila akipita tena napata uoga. Sasa wiki iliyopita nikawa nimejipanga kabisa kwamba leo lazima nimsimamishe hata niongee nae kidogo, Ile nimekaa sina hili wala lile mtoto huyo namuona anakuja, basi mwanaume nikajitosa nkamuita.

Dada wa watu akasimama nikasogea taratibu, sasa hapa ndo tatizo lilipoanzia,Nilipokuwa namkaribia nilishtuka sana, alikuwa ameshika cm mkono mmoja af mwingn kashika pochi, sasa nilipokuwa nampa mkono tusalimiane.. alinipa ule mkono wenye cm kumbe kwenye kidole kimoja alikuwa kaingiza ile ring ya funguo ambazo zilikuwa zimekaa kwa nyuma ya kiganja, mm nikawa naona cm tuu kumbe mtoto mkono huohuo kaning'iniza funguo za ndinga na remote ya BMW.

Kiukwel nlipoziona nilishtuka sana, mistari yote niloipanga kichwani ikayeyuka. Mwanaume nikakosa point kwa sababu nlianza kupata hofu kwamba mtu huyu sikumdhania kama anaweza kuwa na pesa ivoo. Nliona nimeparamia sehem sio level yangu

Nliishia kumwambia samahan sister nmekufananisha na dada mmoja huwa anapita sana hapa. Saivi huwa anapita ananipa hai mana nipo kwenye kabanda flan kana geti tuu so kila anapopita lazma tuonane.

Zile hisia za kumpenda zilishakata asee
Hujajua tu brother, achana na hawa wanaopata pesa kutoka kwa madanga ila ambae ametokea maisha mazuri wengi wastaarabu alafu ni wako desperate kwasababu wanaogopwa na watu wengi. Kwaio wakibahatika kupata mwanaume wanakuwa wapole na adabu tele labla insecurity yako ndio ikufanye uwe mkorofi, uwe mkali nk umpoteze.
 
Vikuku mguuni😪, kucha kama Nsyuka, mijiKope na vijicho nkonyezo pamoja na makeup sipendagi!

Huwa akili inaniambia “atakudanga huyo”
Kaka mimi mwenye nikionaga tu dem makucha marefu sana naghairi hata kumwangalia😂😂
 
Ivi vikuku ni urembo kweli au na mengineyo yamejificha umo?Unakuta mdada anautafuta urembo mpaka basi.Sura nzuri tu lakini mwili kauharibu na matattoo nywele kaweka breach vikuku mguuni n nn?Halaf unatafuta mme!Kwel??Mme gan atakuchukua uko ivyo. Utabak wa kuliwa tu had body count ikose hesabu[emoji35][emoji35]
 
Umenikumbusha kuna rafiki yangu mmoja shule alikuwa ananisema eti mwanamke gani una macho makavuu, mwanamke unatakiwa uwe na jicho la aibu japo kidogo
kutongoza raha, asikuambie mtu, hasa ukute unatongoza afu mwanamke anakurembulia mikono kaelekeza mdomoni anang'ata kucha akiwa kapindisha shingo kidizain flani hivi, huku akikujibu kwa sauti ya chini kwa umbaliii tena nyororoo

Lazma ujimwagie uji surualini. Tena ukute unammbembeleza maeneo watu hawapiti ovyo, unajikuta na denda ushamla.

Kutongoza raha sana, ukutane na mwanamke anaejua kutongozwa.
 
daah nikiona dem mkali afu kavaa vikuku, au kope bandioa stongozi hata bure
 
Back
Top Bottom