Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Mimi nilikuwa mzee wa kutuma Ela, fundi aliniharibia kwenye Renta, aliunga Renta kienyeji, semu zingine akafunga zingine akaskip...sehemu za nje Renta ikawa juu na sehemu za ndani za milango zikawa chini..sehemu zingine pia hakuweka nondo..niligundua wakati nafanya marekebisho kibaraza Cha nje, kwAni tulivunja beam hatukuta nondo ata Moja.
 
Zamani nilikua naona wanaoacha viwanja muda mrefu hawajengi kama wajinga flani hivi.

ila nimekuja gundua kuna maana kubwa sana ya kuacha kiherehere cha kuanza ujenzi kisa una pesa na unaweza.

Kile kiwanja nilinunua enzi ni pori la maana tu,haraka haraka kimbilia jenga..

Tangu zamani nilishasema sitowahi jenga uswahilini, ila sikua najua wanaojenga uswahili hawakuwahi waza kama patakuja kuwa uswahilini.

Baada ya ujenzi miaka kadhaa mbele ule mtaa haukua na tofauti na tandale, ule uswahili,vile vijumba vilivyokua vikichipuka kama uyoga nikajikuta nimewekwa mtu kati, nmezungukwa na vijumba vingiiiiiii...

Nikaona hapa Usintanie,Madalali kazi yao nini? Nikapauza kama palivyo.

Hela yote nimenunulia kiwanja sehemu nyingine, Sijengi ng'o mpaka nihakikishe ule mtaa ni wanaojielewa.

Ntapanga hivi hivi ila siwezi jenga mtaa ambao sina uhakika nawataokuja.

Hii mambo ya kuharakisha kujenga sehemu nyumba ya maana ndio unaweza jikuta unajenga mtaa kama kwa mtogole...

Baadae watoto wanakuuliza baba ilikuaje ukaja kujenga huu mtaa... Unakosa majibu.
Hiyo mkuu imenitokea mimi, nilinunua kiwanja 2010...nikaja kujenga 2015.. siku magufuli anaapishwa ndo nahamia kwangu,, ila sahiv nimezungukwa na waswahili wasiojielewa hata pakupitisha kigari hapapo...nikija kununua gar itabid ilale (CCM.) Natamani kuuza kwa bei ya kutupa nijenge sehemu nyingine..Kijumba chenyewe cha kawaida ila unaishi na watu wenye wivu balaa....

Makosa niliyoyafanya nilijenga kwa haraka haraka lengo nihamie kwangu kutokana kugombana gombana na mwenyenyumba..
Haraka haraka haina baraka..!!
 
Hii kuna rafiki yangu amejenga nyumba ya kisasa ila imekosa choo ndani..inamuuma saana...kwasababu alikua amejenga kidogo kidogo yani kwa kudunduliza...sasa kama unavyojua maisha yanabadilika...anajilaumu vibaya. Vyumba 5 ndani ila choo cha nje.
Vyumba vitano vyote vya nini, aue chumba kimoja afanye kutengeneza vyoo vya ndani. Tena achague chumba kilichopo karibu na chumba chake ili atengeneze choo cha master na choo cha public.
 
Kuajiri plumber uchwara. Kuta maji yanavuja rangi imebanduka sana
umenikumbusha kitu hapa
nilipanga pahala, maji ni dawasco na kila mtu mita yake
nilikua nalipa 40k kila mwezi, baada ya miezi 5 nakuja kustuka kuna leakage, tena sehem ya outlet ya bomba bafuni, na ni ngumu kugundua, maji yana 'chururu' kimya kimya mno yakiambaa ukutani mpaka chini , inaambaa na kona za sakafu, yalee mpaka kwenye kashimo, yaani chururu huioni mpaka uweke macho karib kabisa na ukuta(una tiles), nikapata jibu kwanini ukuta wote wa upande wa pili(kuna room) ulikua unapukutika

nikafunga koki kubwa ya nje, ikawa nikitaka kuchota najaza jaba na ndoo then nafunga koki, bili ya maji ilikuja 8000 kwa miezi iliyobaki
 
Hata kama una uwezo mdogo na eneo linaruhusu, jenga slope yako na ubakishe paking ya gari hata km wakat huo unamilik guta, amin maisha yanabadilika ikiw we ni mpambanaji wa haki, hari na mari miaka 20 haiwez pita kapa, ukakosa hata kirikuu!

Kingne ni kutenga kaeneo kadogo ka bustan binafsi huwa sifurahi kuishi ktk nyumba ambayo haina hata mti wa kivuri
 
Hii kuna rafiki yangu amejenga nyumba ya kisasa ila imekosa choo ndani..inamuuma saana...kwasababu alikua amejenga kidogo kidogo yani kwa kudunduliza...sasa kama unavyojua maisha yanabadilika...anajilaumu vibaya. Vyumba 5 ndani ila choo cha nje.
Si kimoja akibadilshe kuwa choo mbona rahisi sanaaa... Shimo la maji taka linakua njee maana huwezi jenga choo cha shimp ndani...!! Sioni kama kuna kitu kakosea hapo
 
Back
Top Bottom