Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Ni kosa gani ulilifanya kwenye ujenzi wa nyumba yako na usingependa wengine walirudie?

Kwa kweli sio jambo la kitoto. Ni kwamba unajenga nyumba mbili kwa wakati mmoja, na kipato chenyewe cha kuunga unga. Mpaka sasa sijapaua, ila nimeshahamia nakaa kwenye andagraundi, japo jasho linanitoka sana kumaliza jengo.
Hongera kwa kuhamia... Ila, ukimaliza, heshima mtaani lazima iwepo.
 
Nimejenga underground iliyofanywa na fundi wa mtaani (local fundi), wakati wa kumwaga slab, kwenye wiring map ya umeme hawakuweka zile hook za feni (pangaboi), sasa baada ya kumiminwa slab juu hakuna mahali pa kufunga feni au la niweke mbao za dari ili nipate mbao ya kufungia hook, kitu ambacho ni hasara, maana nitakuwa na slab na bado nimeweka dari.

Ninalazimia kutumia feni za kusimama ambazo sizipendi na zinaleta ghasia tu, sijui kama inawezekana kudrill ili tuweke hook ya feni ili nifunge pangaboi.

Kwa niaba ya wanajamii forum wote naomba nitumie ramani PM kiongozi [emoji851]
 
Nimejenga jumba kuubwa, sebule km kiwanja cha mpira, hlf vyumba ni vi 3 tu...

nawaza siku tukibaki 2(mimi na baba chanja), watoto wakipata maisha yao sijui tutaishi vipi.
Binafsi sioni shida. Baadhi vyumba mnaweza kubadilisha matumizi. Kimoja mkafanya cha mazoezi mkaweka vifaa vya mazoezi kingine home library.
 
Nimejenga underground iliyofanywa na fundi wa mtaani (local fundi), wakati wa kumwaga slab, kwenye wiring map ya umeme hawakuweka zile hook za feni (pangaboi), sasa baada ya kumiminwa slab juu hakuna mahali pa kufunga feni au la niweke mbao za dari ili nipate mbao ya kufungia hook, kitu ambacho ni hasara, maana nitakuwa na slab na bado nimeweka dari.

Ninalazimia kutumia feni za kusimama ambazo sizipendi na zinaleta ghasia tu, sijui kama inawezekana kudrill ili tuweke hook ya feni ili nifunge pangaboi.
NUnua feni za maji au AC za kusimama,, Teknolojia imekua jiachie maisha mafupi sana.
 
Vipi hapa imekaaje wakuu?
Screenshot_20230106-072248.jpg
 
Karibu mkuu ushauriwe Kira hatua vizur na wabobez wa taaluma ya ujenzi hutojuta kutupatia kaz yako na tunapunguzo la 30%kwenye labour charge huu mwaka 2023. Call/WhatsApp 0757735884 au tembelea ukurasa wetu Instagram highland _decor_solution
Jazia nyama nyama mkuu tujue shida ni nini maana hapa tayari nina ramani mkononi 2023 ikianza nijilipue
 
Nakukaribisha kufanya finishing nasi au tembelea ukurasa wetu Instagram Kama highland_decor_solution call /WhatsApp 0757735884 skiming nje ni bure ukitupatia kaz mojawapo
Kujenga kighorofa.
Jameni, hii shughuli si yakitoto. Ningejenga nyumba ya chini ya vyumba viwili, ningesha hamia kitambo!
 
Kwa ushauri na mafundi wa uhakika wanaojua kaz vema na wenye uzoefu kwenye fani ya ujenzi call/WhatsApp 0757735884 au tembelea ukurasa wetu Instagram highland_decor _solution
Wakuu na Mimi naomba Mwenye ramani ya vyumba vitatu
Vyote viwe na vyoo ndani,
Na jiko,
Anitumie PM
Naomba mawazo pia ili nisije kufanya makosa
 
Hii kuna rafiki yangu amejenga nyumba ya kisasa ila imekosa choo ndani..inamuuma saana...kwasababu alikua amejenga kidogo kidogo yani kwa kudunduliza...sasa kama unavyojua maisha yanabadilika...anajilaumu vibaya. Vyumba 5 ndani ila choo cha nje.
Kwamba haiwezekani kuvunja chumba kimoja akapata choo ...
 
Back
Top Bottom