Ni kosa gani ulilowahi kusingiziwa au kuadhibiwa wakati hukulitenda ng’o?

Ni kosa gani ulilowahi kusingiziwa au kuadhibiwa wakati hukulitenda ng’o?

Umenikumbusha mbali. Wakati niko mdogo (shule ya msingi), nilipokea barua ya babu shuleni. Wakati huo mawasiliano ni ya barua tu (S. L. P. la shule ama kijiji). Hakukuwa na simu wala internet. Basi katika utoto wangu, nikafungua bahasha na kuisoma ile barua. Kulikuwa na sh 20/= ndani yake. Alikuwa ametumiwa babu na mjukuu wake aliyekuwa anafanya kazi mjini. Baada ya kuisoma, nikampa mpwa wangu aipeleke nyumbani ikiwepo ile sh 20/=. Mimi nilikuwa nakwenda sehemu nyingine wakati yeye alikuwa anaelekea nyumbani.

Ilipofika nyumbani ile sh 20/= haikuwemo. Basi akatafutwa aliyeichukuwa. Yule mpwa wangu akasema ni mimi. Ni kweli nilisoma barua lakini sikuchukuwa ile sh 20/=. Mi nikakataa kuwa sikuichukuwa. Mpwa anasema ni mimi niliyeichukuwa. Basi nilipigwa kipigo cha mbwa mwizi (Mroto = mbwakoko). Bahati mbaya yule mpwa wangu alifariki utotoni. Angekuwepo sasa, ningemkumbusha siku moja.
 
Wakati nipo shule ya msingi kulikuwa na tabia ya walimu kuanzisha miradi yao na kuwapa wanafunzi wauze wakati wa mapumziko wanafunzi wa darasa husika mlikuwa mnagawanywa watatu watatu kila siku sasa siku hiyo sikwenda shule wale wenzangu walipopewa ile hela wakagawana wakaila wakamwambia mwalimu hela wamenipa mimi nikanunue mihogo na sikuja shule daah baada ya siku mbili nimefika shule mwalimu ananidai hela nikabaki nashangaa sitamsahau yule mwalimu alinichapa fimbo na huku anawaambia wanafunzi wanizomee darasani baada ya hapo ananiambia nirudishe pesa ambayo sikuchukua kabisa nilikaa nyumbani miezi mitatu sitaki kusikia shule kabisa hili tukio lilitokea nikiwa darasa la tatu
Kwa nini hukuwaeleza wazazi wako? This is beyond imagination, inasikitisha sana

Ingekua ni zama hizi ningemtafuta huyo mwalimu nimrushe kwenye social media zote ndio angejua hajui
 
Daaa mchumba alikuwa na mahusiano na jamaa mmoja katika kitengo cha kubambikia watu kesi, kuchepuka kulipo noga jamaa akampanga waniwekee madawa ya kulevya ili nitupwe sero wao wale maisha. Acha tu niishie hapa
Hii ni zaidi ya ukatili
 
Watu kunitaja taja kuwa mimi ndo niliyekuwa chini kwenye video ya Meena Ally ki ukweli imeniharibia Carier yangu na sio kweli.
 
Yule mama wa kambo kuniambia nimeiba elfu kumi (miaka ile 2002 ilikuwa pesa ndefu sana) na akanitembezea bakora za kutosha na kwenda kunitangaza darasani. Hii scene ilishagoma kunitoka akilini na leo mimi ni mtu mzima aisee Nimemsamehe tu.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Nikiwa sekondari o-level kuna binti tunafananishwa sana hususani na watu wa madarasa mengine.

One day, mwalimu wa Chemistry akiwa laboratory akaona mtoto wa mlinzi wa shule ameenda kwenye majani nyuma ya lab akaficha mzigo chini ya kanga iliyokuwa imetandikwa pale.

Mwalimu akajua tu ni ishu ya magendo. Akaenda kuangalia akakuta package za kutosha za chips mayai. Alipofika eneo lile kulikuwa na binti mmoja wa a-level amekaa kwenye majani akijisomea. Mwalimu akashawishika kuwa ule ni mzigo wake. Binti akaukataa kata kata.

Mwalimu akamwambia adhabu yake anamfungia ndani ya laboratory awe mlinzi aangalie nani atakuja kuchukua mzigo ule.

Kwa bahati mbaya, mzigo ule ulikuwa wa yule mtu ambaye tulikuwa tunafananishwa na alikuja kuuchukua. Mwalimu aliporudi yule mtuhumiwa namba moja akasema ni Zurie ndo amekuja kuuchukua ule mzigo.

Kesho yake mwalimu ananiita na kuniambia “siamini na wewe unafanya matendo ya kuvunja sheria za shule, umeanza lini?” I was so shocked. Maana nilikuwa a law-abiding student sina makuu zaidi ya kusoma.

Aisee mwalimu kuona nakataa nikapelekwa kwa matron, kufika kwa matron nikakataa, nikapelekwa kwa mkuu wa shule. Nikasema sio mimi na nikademand yule mtoto wa mlinzi aje aseme kama nimewahi hata kuzungumza naye.

Dogo alipokuja ndo ikawa pona pona yangu. Akamtaja mhusika. Ila cha kushangaza nilichukiwa na karibu darasa zima eti ni snitch, kwamba nilitakiwa kulikubali kosa.
Hiki kisa chako kimenisisimua mno mkuu Zurie . Hii ni shule gani ya ajabu hivi? Kwani kula chips ilikuwa marufuku au walimu walitaka wanafunzi wote mpigike sawasawa ili kujenga equality shuleni? Shule niliyosoma wasichana walikuwa hawaruhisiwi kuvalia mikanda sketi zao kwa kisingizio cha kujenga usawa wa kiuanafunzi. Nadhani hii sheria ni mbaya sana, hasa for mature students. Kwa watoto wadogo wa chekekechea na shule za msingi inaleta mantiki fulani. Hii shule yenu bila shaka ilikuwa seminary kama sikosei 🤣 🤣 🤣
 
Kwa nini hukuwaeleza wazazi wako? This is beyond imagination, inasikitisha sana

Ingekua ni zama hizi ningemtafuta huyo mwalimu nimrushe kwenye social media zote ndio angejua hajui
Ingekuwa zama hizi za wazazi wa mwendokasi pangechimbika mbona. Mwanafunzi angeenda kuripoti kwa mzazi wake awaibukie walimu vibaya sana hukohuko shuleni. Ujue zamani walimu walikuwa wanaheshimika na kuogopeka sana tofauti na zama hizi.
 
Yule mama wa kambo kuniambia nimeiba elfu kumi (miaka ile 2002 ilikuwa pesa ndefu sana) na akanitembezea bakora za kutosha na kwenda kunitangaza darasani. Hii scene ilishagoma kunitoka akilini na leo mimi ni mtu mzima aisee Nimemsamehe tu.


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Enzi zile watoto walikuwa wakisingiziwa sana na kuadhibiwa kwa makosa wasiyotenda. Haki za watoto zilikuwa hazizingatiwi; hakukuwa na watetezi wa asasi za kiraia.
 
Manjiani majuzi tu hapa..

Kuna Khenge iliniovateki ndani ya eneo la 50 wakati huo Niko below 50, cha kushangaza eti tukasimamishwa wote kuwa Tume Over speed.. Wale Mbwa nilibishana nao mpaka nikamua waniandikie tu 30 kuliko niwapooze na 10..

Jamaa angu akanitonya kuwa kuna namna huchukua speed ya Wa mbele yako Ila Picha wanakupiga wewe.
Hao vibaka wa 50 waangalie sana. Kuna mkaka mmoja analipa 30 lkn haiendi bure
 
Hiki kisa chako kimenisisimua mno mkuu Zurie . Hii ni shule gani ya ajabu hivi? Kwani kula chips ilikuwa marufuku au walimu walitaka wanafunzi wote mpigike sawasawa ili kujenga equality shuleni? Shule niliyosoma wasichana walikuwa hawaruhisiwi kuvalia mikanda sketi zao kwa kisingizio cha kujenga usawa wa kiuanafunzi. Nadhani hii sheria ni mbaya sana, hasa for mature students. Kwa watoto wadogo wa chekekechea na shule za msingi inaleta mantiki fulani. Hii shule yenu bila shaka ilikuwa seminary kama sikosei [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787]

Shule moja ya kanisa katoliki. Chips ilikuwa marufuku. Wote mnakula ugali/wali maharage. Chips zinauzwa siku ya visiting day mara moja kwa term.

Na ile shule wangeruhusu hizo mambo kwa kila mtu yaani labda chips ziuzwe kuna wanafunzi wangeweza kuwa depressed. Maana watoto wa members wa cabinet ya kipindi hicho (akiwemo Marehemu Mwendazake) walikuwa wamejaa, watoto wa wabunge, businessmen n.k.

Wenzangu na mie aidha wangeiba au kunyong’onyea.
 
Shule moja ya kanisa katoliki. Chips ilikuwa marufuku. Wote mnakula ugali/wali maharage. Chips zinauzwa siku ya visiting day mara moja kwa term.

Na ile shule wangeruhusu hizo mambo kwa kila mtu yaani labda chips ziuzwe kuna wanafunzi wangeweza kuwa depressed. Maana watoto wa members wa cabinet ya kipindi hicho (akiwemo Marehemu Mwendazake) walikuwa wamejaa, watoto wa wabunge, businessmen n.k.

Wenzangu na mie aidha wangeiba au kunyong’onyea.
Ni kweli kabisa kuhakikisha wote mnakuwa sawa kimavazi, nk; ndio maana hata siku za wikendi baadhi ya shule zinalazimisha kila mwanafunzi akitoka nje ya shule sharti aombe ruhusa na avae sare za shule ili kumtambulisha popote awapo asije ama akakengeuka au akajiingiza kwenye magenge ya ajabu. Ila kwa seminary wapo strict zaidi ya hapo.
 
Back
Top Bottom