Ni kosa kubwa kama tutawafunga Algeria, Waafrika wenzetu hawatatusamehe

Ni kosa kubwa kama tutawafunga Algeria, Waafrika wenzetu hawatatusamehe

Hizi Akili za Lubuva humu zinatoka wapi jamani
 
Kwani sifa ya kuwa mtanzania lazima uwe lofa na mpumbavu?

Kufikiria kwamba Taifa stars wanaweza kufuzu kucheza kombe la dunia ni sawa na kupigia ccm kura ukiamini watawafunga mafisadi na kupigania rasilimali za nchi iwanufaishe wananchi.


Kama kungekuwa na mpira wa maneno ya vijiweni angalau watanzania ipo siku tungefuzu na kuchukua kombe.

Wachache saana ndo wameona hili, na hii imeonesha kuwa Watanzania bado tunajipaga matumaini hewa. Hatuna timu ya kufuzu na kuipeleka Urusi ikacheze na akina Neymar.
 
Mkuu nakuunga mkono kama mwafrika halisi , umefikiria nje ya box , tanzania tunaitaji tuwekeze ili kufanikiwa nashangaa leo watu wamejitwisha matumaini tele ya ushindi wakati hali halisi inajulikana , tunaomba haki itendeke Tanzamia 1 Algeria 4. mungu ibariki africa

Asante!
 
Kwakweli nikikumbuka jinsi hawa Algeria walivyoikamata German kombe la dunia lililopita..nakata tamaa nasema haiwezekani..
sisi tuache porojo tujipange 2022..akina Samata na Ulimwengu hawatoshi kutuvusha hii sio siasa..
Nashkuru kwa kuliona hili.
 
mleta mada unaposema kua ni kosa kubwa kuwafunga Algeria hujioni kua wewe ni PIMBI

Hio timu unayoiona wewe kua ni bora iweje ikifungwa na Tanzania useme kua tutaonekana ni wasaliti?

Ili tuwaamini kua wao ni bora kuliko sisi lazima watufunge otherwise sisi tutakua ndio wawakilishi wazuri kama tukiwafunga

"usipokua mwaminifu kwa jambo dogo huwezi kua mwaminifu kwa jambo kubwa"

Tatizo Watanzania hawapendi kuambiwa ukweli, yaani hata kama anaumwa anataka umwambie mazuri tuu hata kama anakosea. Hii timu ni mbovu, ni mbovu kabisa. Hivi hii Algeria angeamua akomae ka alivyomkomalia Ujerumani unadhani pale Taifa tungewaza kuzuia kipigo cha 5-0!? Tushukuru majamaa wametutunzia heshima Uwanjani kwetu.
 
Tatizo Watanzania hawapendi kuambiwa ukweli, yaani hata kama anaumwa anataka umwambie mazuri tuu hata kama anakosea. Hii timu ni mbovu, ni mbovu kabisa. Hivi hii Algeria angeamua akomae ka alivyomkomalia Ujerumani unadhani pale Taifa tungewaza kuzuia kipigo cha 5-0!? Tushukuru majamaa wametutunzia heshima Uwanjani kwetu.

Usitake kusema leo wanaenda kututunzia heshima kwao kwa kutuacha tuwatoe,Tuliwazidi na tunawatoa tar 17 sasa kama ni kosa ndo tunalitenda leo kwa ufanisi mkubwa.
 
Kwa mtazamo mpana zaidi namuelewa mtoa mada, kuwa kuwafunga Algeria kwa ndulute ni kuitoa nchi ya Kiafrika ambayo walau ina dalili ya kufanya vema Kombe la Dunia, tukitazama historia yao.

Kuna ukweli fulani, kama unazingatia Uafrika wa Kimajumui.
 
Algeria inapatikana Africa lakini jamaa ni waarabu ndo mana wapo kwenye arab league na wala hawawezi jitambulisha kama yeye ni muafrica...

Wapo Afrika lakini ni Waarabu, nini unataka kusema? Ni Waarabu ndio, na sisi ni Waabantu na wengine ni Nilotics... Arab League ni muungano wa kisiasa, kuwa kule haimaanishi umejitoa Afrika au nchi yako si ya Kiafrika.

Soma: https://en.wikipedia.org/wiki/Étoile_Nord-Africaine
 
Mkuu iron finger nakupa LIKE. button ya like haipo hivyo chukua hiyo. Hata tuwafunge magoli mia tanzania hatuendi popote kamwe. Sasa roho ya kwa nini inatoka wapi. Ndio maana wenzetu weupe wanaendelea. Kung'ang'ania vitu ambavyo havina tija kwetu ya nini, itakuwa na msaa gani, pia kuwatoa algeria tutafaidika na nini, ubinafsi umetuzidi sana ndio maana tutabaki kuangalia world cup kwenye tv tu

Button ya like haipo?......
 
Kama wana kiwango si waifunge stars? As simple as that. Kama nimemuelewa vizuri mleta mada anataka stars wacheze kilege lege ili kutoa nafasi kwa Algeria kushinda na wasonge mbele kwa kuwa stars hawafai! Akili zingine hizi jamani!
Binti kiziwi umesikia matokeo?
 
Usitake kusema leo wanaenda kututunzia heshima kwao kwa kutuacha tuwatoe,Tuliwazidi na tunawatoa tar 17 sasa kama ni kosa ndo tunalitenda leo kwa ufanisi mkubwa.
Vipi mkuu? 7-0, agg 9-2
 
Kama wana kiwango si waifunge stars? As simple as that. Kama nimemuelewa vizuri mleta mada anataka stars wacheze kilege lege ili kutoa nafasi kwa Algeria kushinda na wasonge mbele kwa kuwa stars hawafai! Akili zingine hizi jamani!

Bado upo!!
 
Algeria inapatikana Africa lakini jamaa ni waarabu ndo mana wapo kwenye arab league na wala hawawezi jitambulisha kama yeye ni muafrica...

wasijitambulishe kama waafrika kwa nini? mkuu sio kila aliye muafrika ni black- african. wao ni waafrika but sio black africans
 
Taifa stars sio TP Mazembe, Yanga, Azam na Stand United tu. Tuanzie kwenye grass roots tuwapate akina Mbwana wengi. Copa coca cola iboreshwe
 
Back
Top Bottom