Ni kwa kiasi gani unaridhika na jina lako ulilopewa na wazazi wako?

Ni kwa kiasi gani unaridhika na jina lako ulilopewa na wazazi wako?

Wakuu salama..!!

Je, ingekuwa ni utashi wako ungejiita jina lako hilo hilo.?

Nimeanza na ulizo hilo, kwa maana katika nyakati za ukuaji imebainika watu huweza kujipachika majina tofauti tofauti kulingana na mazingira au matakwa ya nyakati.

Si ajabu kwa kila mmoja wetu, basi tuseme wengi kama sio wote, tumewahi kujiita majina mbalimbali.

Mfano majina ya watu maarufu tuliowaona kwenye filamu, au hata vibonzo na wanyama wakali.

Pamoja na ukweli kuwa majina ni utambulisho tu, lakini kuna kipindi tumewahi kuhisi kuna majina mazuri na mabaya. Hivyo tumewahi kutamani jina fulani au kuchukia lingine.

Kwa kuwa tunapewa majina tukiwa wadogo sana, hii haitupi haki ya kuchagua majina tuyapendayo. Hii hutulazimu kutii na kukua hivyo, na pale tunapopata kujitambua wengi wetu tumekuwa tukijaribu kubadili majina yetu.

Mifano ni mingi ila mojawapo ni ID za JF, na hata zile mnaita ‘a.k.a’ za almaarufu ni ushahidi tosha wa kutaka kubadili jina, japo vyeti vitabaki na majina asilia ila huenda kuna namna roho yako inatamani vinginevyo.

Hebu niulize tena, ingekuwa unazaliwa unaachwa ukue bila jina, hilo ulilojichagulia sasa ndo ungependa uitwe.?

Kuna jina zuri na baya.? Ooh jina lako zuri (kinafiki likiwa baya huambiwi), ooh jina lako gumu, oooh jina lako refu etc. [hapa tafadhali tujali matamshi tu, sio nguvu za jina kiimani].

Jina lako ulilopewa na wazazi wako, unaridhika nalo au unatii tu na kuheshimu wazazi au kwamba huna namna ya kufanya.?

Cheers 🥂

Langu naridhika nalo ila nina marafiki hawapendi majina yao, nawataja

1. NASIBU ABDULI-DIAMOND PLATINUMZ

2.POMBE-JIWE

3. SHETA-MWANTUMU

5.DR. CHENI- ABDULKADIR RAFIQ

6. JEREMIA TUNTFYE MWAKIBOLINGUNAYE -BULLDOZA MWAMPOSA

7.RAMADHANI- RAMSO

8. OMARI NDIYAGE -OMMY DIMPOZ

9. JAKI NTUYABALIWE-K-LYNN

10. JUDI WAMBURA-J -DEE

11. MAJIZO

12. BASHITE-MAKONDA
 
Jina langu ikitokea binti kafall lazima ataanza kuniita kifupi chake so naridhika sana na hili jina linanipambania katika kuhakikisha sitokufa na upweke.

Hayo majina yanayofupishwa mara nyingi ukamilifu wake ni majanga, jina yafaa litamkike full.
 
Langu naridhika nalo ila nina marafiki hawapendi majina yao, nawataja

1. NASIBU ABDULI-DIAMOND PLATINUMZ

2.POMBE-JIWE

3. SHETA-MWANTUMU

5.DR. CHENI- ABDULKADIR RAFIQ

6. JEREMIA TUNTFYE MWAKIBOLINGUNAYE -BULLDOZA MWAMPOSA

7.RAMADHANI- RAMSO

8. OMARI NDIYAGE -OMMY DIMPOZ

9. JAKI NTUYABALIWE-K-LYNN

10. JUDI WAMBURA-J -DEE

11. MAJIZO

12. BASHITE-MAKONDA
huyu namba sita ana jna gumu balaa halali abadilishe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfano wewe umezaliwa ukaitwa Makenzi[emoji847] [najua wajua kikwenu linamaanisha nini], wewe ukajifanya mjanja kuliremba ukajiita Kenzy[emoji847]... wengine wanajiita McKenzie 🤣🤣
Hasa watu wa Dini ilee, hawapendi majina yao , utaskia Ramso, Muddy, Mwajei, mwakifilimbitulingijaho etc
 
Halafu kwanini wasanii wengi wa nyimbo na maigizo na Watangazaji wa Kiislam hupenda kuwapa CHARACTERS wao majina ya Kikristo?? Angalia Bongo Movies au Nyimbo za Kibongo au wao wenyewe A.K.A zao wajipa majina ya kikristo?? (Samahani kama nipo nje ya mada)
 
Halafu kwanini wasanii wengi wa nyimbo na maigizo wa Kiislam hupenda kuwapa CHARACTERS wao majina ya Kikristo?? Angalia Bongo Movies au Nyimbo za Kibongo au wao wenyewe A.K.A zao wajipa majina ya kikristo?? (Samahani kama nipo nje ya mada)

Nafikiri mambo ya sanaa na maigizo ni kinyume na maadili ya SAW, so wanamzunguka kumpoteza kiaina.... sina uhakika.
 
Back
Top Bottom