Ni kwa kiasi gani unaridhika na jina lako ulilopewa na wazazi wako?

Ni kwa kiasi gani unaridhika na jina lako ulilopewa na wazazi wako?

Nalipenda jina langu ila lipo common kiasi na kupita mtaa mpya ukasikia mtu anaitwa sio kitu kipya, kwenda sehemu na usikute mtu anaitwa hivyo ni nadra zaidi ya nadra. Ila bado nalipenda
 
Mimi MKUU sijaridhika nalo,,,jina langu halisi ni KISIGINO..DOLE GUMBA..naona hata aibu nikitongoza mwanamke akitaka nijitambulishe....hakuna kitu nilijisikia VIBAYA kama shuleni wakati wa kuitwa majina..inaniuma sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi MKUU sijaridhika nalo,,,jina langu halisi ni KISIGINO..DOLE GUMBA..naona hata aibu nikitongoza mwanamke akitaka nijitambulishe....hakuna kitu nilijisikia VIBAYA kama shuleni wakati wa kuitwa majina..inaniuma sana

Sent using Jamii Forums mobile app

Shuleni nafikiri hii inaumiza wengi, ukizingatia hapo mnakuwa bado watoto hivyo ikifika jina lako kuitwa wenzako wote wanacheka.... ila ukikua ukiwa na hela utaitwa vizuri tu mzee. [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Jina langu nalipenda sana, na nikiskia mtu anaitwa hilo jina hua natokea kumpenda ghafla!

Kwenye social networks pia natumia jina langu halisi, kasoro JF tu. Sijawahi tamani jina lingine lolote

Hongera sana mkuu.
 
Wakuu salama..!!

Je, ingekuwa ni utashi wako ungejiita jina lako hilo hilo.?

Nimeanza na ulizo hilo, kwa maana katika nyakati za ukuaji imebainika watu huweza kujipachika majina tofauti tofauti kulingana na mazingira au matakwa ya nyakati.

Si ajabu kwa kila mmoja wetu, basi tuseme wengi kama sio wote, tumewahi kujiita majina mbalimbali.

Mfano majina ya watu maarufu tuliowaona kwenye filamu, au hata vibonzo na wanyama wakali.

Pamoja na ukweli kuwa majina ni utambulisho tu, lakini kuna kipindi tumewahi kuhisi kuna majina mazuri na mabaya. Hivyo tumewahi kutamani jina fulani au kuchukia lingine.

Kwa kuwa tunapewa majina tukiwa wadogo sana, hii haitupi haki ya kuchagua majina tuyapendayo. Hii hutulazimu kutii na kukua hivyo, na pale tunapopata kujitambua wengi wetu tumekuwa tukijaribu kubadili majina yetu.

Mifano ni mingi ila mojawapo ni ID za JF, na hata zile mnaita ‘a.k.a’ za almaarufu ni ushahidi tosha wa kutaka kubadili jina, japo vyeti vitabaki na majina asilia ila huenda kuna namna roho yako inatamani vinginevyo.

Hebu niulize tena, ingekuwa unazaliwa unaachwa ukue bila jina, hilo ulilojichagulia sasa ndo ungependa uitwe.?

Kuna jina zuri na baya.? Ooh jina lako zuri (kinafiki likiwa baya huambiwi), ooh jina lako gumu, oooh jina lako refu etc. [hapa tafadhali tujali matamshi tu, sio nguvu za jina kiimani].

Jina lako ulilopewa na wazazi wako, unaridhika nalo au unatii tu na kuheshimu wazazi au kwamba huna namna ya kufanya.?

Cheers [emoji1635]
Nalipenda la kwangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom