Ni kwa kiasi gani unaridhika na jina lako ulilopewa na wazazi wako?

Ni kwa kiasi gani unaridhika na jina lako ulilopewa na wazazi wako?

Wakuu salama..!!

Je, ingekuwa ni utashi wako ungejiita jina lako hilo hilo.?

Nimeanza na ulizo hilo, kwa maana katika nyakati za ukuaji imebainika watu huweza kujipachika majina tofauti tofauti kulingana na mazingira au matakwa ya nyakati.

Si ajabu kwa kila mmoja wetu, basi tuseme wengi kama sio wote, tumewahi kujiita majina mbalimbali.

Mfano majina ya watu maarufu tuliowaona kwenye filamu, au hata vibonzo na wanyama wakali.

Pamoja na ukweli kuwa majina ni utambulisho tu, lakini kuna kipindi tumewahi kuhisi kuna majina mazuri na mabaya. Hivyo tumewahi kutamani jina fulani au kuchukia lingine.

Kwa kuwa tunapewa majina tukiwa wadogo sana, hii haitupi haki ya kuchagua majina tuyapendayo. Hii hutulazimu kutii na kukua hivyo, na pale tunapopata kujitambua wengi wetu tumekuwa tukijaribu kubadili majina yetu.

Mifano ni mingi ila mojawapo ni ID za JF, na hata zile mnaita ‘a.k.a’ za almaarufu ni ushahidi tosha wa kutaka kubadili jina, japo vyeti vitabaki na majina asilia ila huenda kuna namna roho yako inatamani vinginevyo.

Hebu niulize tena, ingekuwa unazaliwa unaachwa ukue bila jina, hilo ulilojichagulia sasa ndo ungependa uitwe.?

Kuna jina zuri na baya.? Ooh jina lako zuri (kinafiki likiwa baya huambiwi), ooh jina lako gumu, oooh jina lako refu etc. [hapa tafadhali tujali matamshi tu, sio nguvu za jina kiimani].

Jina lako ulilopewa na wazazi wako, unaridhika nalo au unatii tu na kuheshimu wazazi au kwamba huna namna ya kufanya.?

Cheers [emoji1635]
Naitwa Lambert Franklin Harrison
Jina moja la kibabe sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
‘Wengi wenu’.

Akiwa hivi anajitambulisha vile, mara huku vile.... eti ana jina la nyumbani na la kutokea [emoji16][emoji16][emoji16]
Mimi natambulika kwa jina moja tu
Hili jingine wazazi hupenda kuniita Mara chache Sana.. Tena huunganisha yote matatu.

Character yangu ni ileile sehemu zote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uzuri au ubaya wa jina hutegemea thamani ya mwenye jina hilo, wapo watu waliopewa majina ‘magumu’ ila wameyabadili majina hayo na kuwavutia wengi.

Jina kama Dangote sijui Mengi sijui Magufuli hakuna mtu angeyatamani bila kujua thamani ya wenye nayo, siku hizi kila mzazi anatamani aite mtoto wake Obama sijui Mufuruki.

Wengi hatujui hilo, tunachagua majina mazuri ili tufurahie, hakuna jina zuri wala baya au gumu.

Jina langu hili hili nikilijaza thamani mbona litakuwa rahisi na tamu kutamkwa [emoji39][emoji39][emoji39]
 
Hoja hapa sio kukataa majina, kukubali au kukataa kuna sababu nyingi nyuma yake.

Hapa ni ile tu hali ya kuwa umewahi japo kutamani jina lingine, iwe kiutani au kitoto au ni kweli unafurahia mno jina lako.

Kama hivi kujiita kwenye mitandao, hata kama sio lazima uwe incognito mfano fesibuku na Instagram lakini utakuta huandiki jina lako kwa usahihi.
 
Nilivyokua mdogo nilikua silipendi jina langu. Gumu lazma umtajie mtu zaidi ya mara moja ndo aliskie, kuandika wengi walikua wanakosea, wengine wakawa wanali modify kulitamka wanavyotaka. Nilikua nakasirika sana nikiwa form 1 nikamfata shangazi nikwambia mimi hili jina silitaki twende RITA tukalibadilishe officially. Akaniangalia akasema hilo ndo jina lako. Mengi yamekua attached na hilo jina. Bahati etc usibadilishe. Nimekua mkubwa sasa I don't care nalipenda sana jina langu. Ndo nalitumia across all social media sina haja ya kujipa nickname coz it's already Unique.

Sent From Galaxy S9
 
Nilivyokua mdogo nilikua silipendi jina langu. Gumu lazma umtajie mtu zaidi ya mara moja ndo aliskie, kuandika wengi walikua wanakosea, wengine wakawa wanali modify kulitamka wanavyotaka. Nilikua nakasirika sana nikiwa form 1 nikamfata shangazi nikwambia mimi hili jina silitaki twende RITA tukalibadilishe officially. Akaniangalia akasema hilo ndo jina lako. Mengi yamekua attached na hilo jina. Bahati etc usibadilishe. Nimekua mkubwa sasa I don't care nalipenda sana jina langu. Ndo nalitumia across all social media sina haja ya kujipa nickname coz it's already Unique.

Sent From Galaxy S9
Naomba kulifahamu 😍
 
Langu naridhika nalo ila nina marafiki hawapendi majina yao, nawataja

1. NASIBU ABDULI-DIAMOND PLATINUMZ

2.POMBE-JIWE

3. SHETA-MWANTUMU

5.DR. CHENI- ABDULKADIR RAFIQ

6. JEREMIA TUNTFYE MWAKIBOLINGUNAYE -BULLDOZA MWAMPOSA

7.RAMADHANI- RAMSO

8. OMARI NDIYAGE -OMMY DIMPOZ

9. JAKI NTUYABALIWE-K-LYNN

10. JUDI WAMBURA-J -DEE

11. MAJIZO

12. BASHITE-MAKONDA
We jamaa bhana

Sent using kidole gumba
 
Hoja hapa sio kukataa majina, kukubali au kukataa kuna sababu nyingi nyuma yake.

Hapa ni ile tu hali ya kuwa umewahi japo kutamani jina lingine, iwe kiutani au kitoto au ni kweli unafurahia mno jina lako.

Kama hivi kujiita kwenye mitandao, hata kama sio lazima uwe incognito mfano fesibuku na Instagram lakini utakuta huandiki jina lako kwa usahihi.
Jina langu nalipenda sana, na nikiskia mtu anaitwa hilo jina hua natokea kumpenda ghafla!

Kwenye social networks pia natumia jina langu halisi, kasoro JF tu. Sijawahi tamani jina lingine lolote
 
Tuttyfruity
Lakini ni kwa mbinde, yaani ni baada ya kujaribu na kushindwa.... au ni baada ya kuaminishwa hizo attachments ndo ukaanza kuuona uzuri wa jina lako.

That’s the reality, wengi wetu tunapitia hayo at some point in our life.... hasa majina ya mizimu [surnames] ila ukiwa mkubwa ndo unaelewa.

Mimi vijana wangu nimewapa majina yao kama kawaida, ila cha ajabu hawapendi kujitambulisha kwa ‘Surname’ yetu ambayo sijui wanahisi ni ushamba.... furaha yao ni majina ‘mazuri’ hivyo wanataja jina lao na la baba [mimi] tu japo surname lipo kwa cheti.

Inaenda na umri na utambuzi.
 
Back
Top Bottom