Kwani katika huo mstari ulio'quote' umeona sehemu yoyote ikikuzuia kuhoji chochote?Mkuu, kwani shida iko wapi? Watu wanadadavua na kuhoji maswala mazito ya Mwenyezi Mungu, ndo washindwe na waogope kudadavua na kuhoji mambo ya nyerere? Kama hapakua na tatizo si tuta conclude tu kwamba hakukua na shida, na kama palikua na uwalakini basi tutasema pia, unafki wa nin?
Sina shida na hiyo milango yako na ni kwa vipi inafunguka.Kalamu,
Nimekuonyesha na kukujulisha madarasa yangu.
Mimi nimesoma Nyaraka za Sykes na nimezungumzanao.
Kama yeyote yule angebahatika kuzisoma nyaraka hizi na kuzungumza na watu hawa angezungumza kama mimi.
Unaona baada ya kitabu kuchapwa milango mingapi nimefunguliwa mimi kuingia?
View attachment 2551783
Balozi Abbas Sykes na Mwandishi 2012
Wewe ni mpumbavu na una mitazamo duni sanaaaKi uhalisia kabisa Watu wengi wa pwani au waislamu hawana ningwa katika kuwaamini watu wawe wa imani tofauti au wawe wa makabila tofauti, wao wanawaamini sana na hupata hasara sana kwani wengi wao sio waaminifu. hata kwenye biashara watu wa bara ni mara chahche sana kuwa waaminifu. Hii ni hulka yao, hawakuanza leo.
Na mpaka leo hii asilimia kubwa ya watu wa ukanda huu pwani wengi haiwaijui Tanganyika vilivyo..Dunia yao ni ndogo sanaaa...samba na upeo wao...Sasa hawa wazee wetu akina mohamed said wanapowanywesha habar za chuki chuki na uongo uongo in the name of utafiti huku wakipalilia dini wao huwa wanaziamin kwel yani.Hizi mada zinazomhusu Mwalimu na hili kundi maalum huwa najaribu sana kuiepa nisishiriki kwa sababu najua msukumo wa mijadala hii ni nini hasa.
Sasa unaniita nijadili jambo ambalo ni wazi kabisa kwamba hao wazee wa Kariakoo dunia yao iliishia Magomeni, zaidi ya hapo hawakujuwa uwepo wa Tanganyika nzima na waTanganyika huko kwingine?
Hata hapo Kariakoo penyewe, unaweza kupata nyaraka na kumbukumbu za mikutano walizozifanya kuwa ushahidi wa kupigania uhuru wa Kariakoo?
mudi nyota ya nyerere ni kubwa mpaka kiama haiwezi kuzimwa na vipeperushi vyako vya jf.Uwe unapenda ndo' hivyo,hupendi ndo' hivyo.Jiwe...
Historia ya uhuru wa Tanganyika imeathirika sana kwa watu kutia fikra zao binafsi badala ya kuweka yale yenye ithibati ya utafiti.
Ndiyo sababu leo mimi niandikapo historia ya TANU wasomaji huwa wanasoma upya historia ya uhuru wa Tanganyika.
Viongozi wa TANU majimboni wengi wao wakitokea TAA ndiyo waliomjulisha Mwalimu kwa wanachama wao na si kinyume chake.
Soma historia yote hii vipi TANU iliingia majimboni utakuta hakuna aliyemjua Nyerere majimboni sikwambii Dar es Salaam.
Tanganyika wananchi hawakuwa wamehasimiana.
Walikuwa wamoja.
Luku...mudi nyota ya nyerere ni kubwa mpaka kiama haiwezi kuzimwa na vipeperushi vyako vya jf.Uwe unapenda ndo' hivyo,hupendi ndo' hivyo.
Kalamu,Sina shida na hiyo milango yako na ni kwa vipi inafunguka.
Kila mtu ana milango yake.
Ukweli wazee wengi hao unaowaita ni wamjini, elimu walikuwa hawana. Walikuwa wanaungaunga tu. Ujanja wa mdomoni tu
Dah!Kalamu,
Umeghadhibika.
Mimi na wewe tusitishe mjadala huu hadi baadae.
Kalamu,Dah!
Hizi mbinu za mijadala wengine tulishazisoma na kuzielewa siku nyingi sana.
Kiufupi ni kwamba hakuna "mjadala" kati yetu. Huwezi kujadili uongo, jambo ambalo ni batili.
Kalamu,Hakuna anayekuzuia kuamini upendavyo, na ni hivyo hivyo kwa wasioamini unayoamini wewe.
Wakiona unasema uongo wanayohaki pia ya kusema hivyo.
Luku...
Laiti ningeandika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika kwa nia ya kumdogosha Mwalimu Nyerere kitabu changu kingekuwa kimekufa miaka mingi na leo wewe usingeniandikia hapa JF.
Lakini sikunyanyua kalamu yangu kwa nia hiyo.
Niliandika kitabu cha Abdul Sykes (1998) kwa nia ya kusahihisha historia iliyokuwa imekwisha andikwa lakini ina makosa.
Kitabu kilipotoka kiliwavutia wengi kwa jinsi kilivyopishana na historia iliyokuwapo.
Kitabu hiki sasa kinakwenda toleo la tano.
EeeenHeeee!Kalamu,
Ingia katika historia ya Mwalimu Nyerere ndani ya kitabu chs Sykes uonyeshe uongo nilioandika.
Jopo la Prof. Shivji lililoandika Nyerere Biography wameisifia Maktaba yangu kuwa ni kati ya maktaba tatu zenye historia kubwa ya Julius Nyerere: Maktaba ya Brg. General Hashim Mbita, Dr. Salim na yangu.
Nina sababu gani ya kusema uongo?
Soma kitabu cha Mwalimu uone mara ngapi wamenifanyia rejea.
Nakuwekea picha nimeshika kitabu cha Mwalimu nilichopewa na Waandishi kwa mchango wangu katika kuwaeleza historia ya Mwalimu toka alkipofika Dsr es Salaam 1952 hadi alipostaafu urais mwaka wa 1985:
Pengine tutasimamisha shingo zetu na kusema "mzee mohammed ni mdini" lakini hatutathubutu kujiuliza hayo aliyoyafanya nyerere yalimaanisha nin! Hata bila kupepesa macho nyerere alikua na hofu dhidi ya waislam kuwa na nyadhfa za juu katika nchi hasa baada ya uhuru, na pia hakutaka ifahamike wazi kwamba vijana na wazee wengi sana wa kiislamu walikua nae bega kwa bega katika harakati za uhuru. Sababu ya kufanya hivo, anaijua ye mwenyew na pengine amekufa nayo kifuani.
Najiuliza! Mkakati huu wa kuhakikisha mashujaa na wapambanaji hawa wa tanganyika yetu, wanafichwa kabisa hata wasisomwe popote kama moja ya watu muhimu katika harakati za uhuru, ni nan aliekuwa anaushughulikia? Mana yote waliokuwa wakiyafanya wao pamoja na nyerere, hayakufanyika gizani wala mafichoni..! Mpaka miaka ya 80's, 90's na mwanzoni mwa 2000's naamini bado palikua na wazee wengi sana waliopata kuyashuhudia yote haya! Sasa nguvu kubwa ya kuwafumba midomo wote hawa ilitoka kwa nani na lengo hasa likiwa ni nin? Yani, lengo la kuwaziba vinywa kiasi asipatikane hata mmoja wa kuyanena haya nin? Ni kitu gan kilihofiwa kutokea endapo history hii ingeachwa wazi? Je kitu hicho ni positive au negative kwa taifa?
Kalamu,EeeenHeeee!
Unaji'promote' kwelikweli.
Katika kujiuza huna mfano wa kukufikia.
Tatizo ni kuweka chumvi nyingi katika baadhi ya mambo na kupotosha mengine kukidhi ajenda zinazokupa msukumo.
Sifa hii ya ku'exagerate' katika baadhi ya mambo, na kwingine kutunga uongo kabisa inaharibu taswira nzima ya unayoyasimamia.
Yoda,Jambo kubwa katika Taifa hili sio kupata uhuru tu. Wakolini wasingedumu milele, Uhuru tungepata tu katika kipindi fulani kupitia yeyote kama nchi nyingine zote za Africa zilivyopata uhuru. Jambo kubwa zaidi katika historia yetu ni Utaifa imara unaotangulia mambo yote, ni Nyerere kuweza kutengeneza Taifa moja lisilo na migwanyiko ya kikablia, kikanda na kidini kutoka eneo lenye makabila mengi sana, kanda nyingi na dini kubwa mbili.
Hili sio jambo rahisi hasa ukitizama nchi nyingine ambazo zilikuwa na makundi kama haya ya kwetu. Hapo ndipo huwa namsamehe tu Mwl. hata katika blunders zake nyingine kama sera za ujamaa na ufutaji wa demokrasia ya vyama vingi.
Yoda,Nyerere alikuwa nationalist na Pan-Africanist, kutakuwa na namna fulani "wazee wa Kariakoo" walikuwa wanataka kutanguliza maslahi mengine mbele juu ya yale ya kitaifa. Kwa Nyerere loyalty ya kwanza ni taifa, ungekuwa tofauti naye katika hilo ungepotea tu katika historia.
Sidhani pia kama wazee wa Kariakoo walikuwa wanaelewa mambo yoyote kuhusu Pan-Africanism, walikuwa kwenye league tofauti sana na Nyerere.