Unafuatilia nini ?!!!
Hivi ukijiamini unabaguliwaje ?!!
Unaanzaje kubaguliwa??!!!
Iwe na mwarabu ,mhindi ,mzungu ama mchina?!!!
Waafrika tu wako wabaguzi dhidi ya wenzao....kikabila ,rangi ,kipato....ssmbuse watu wenye rangi nyeupe?!!!
Dunia ya sasa ya SOKO HURIA na MAARIFA mapana...vilio vya kubaguliwa havina maana....
Unakuwa wapi mpaka mtu anakubagua?!!
Mfukoni mwake ?!!! [emoji15][emoji1787][emoji1787]
Kwanini uwe mfukoni mwake ?!!
Why desperation?!!!
Umesema kuwa mwafrika hata awe muislam na kuwa (Qari) fundi wa kusoma Quran hawezi kuoa hao waarabu...right?!!!
Nisikilize....watu wengi hawana imani ya dini vile wanavyojionyesha ukubwa wa kuwa nayo....iwe hao waarabu ama wengineo....[emoji1787]
Sasa unataka mwarabu asiye na IMANI kubwa ya dini akupe binti yake kwa kuwa tu wewe "una sauti " kinanda ya kusoma Quran ?!!!
Hao waarabu wengi ni wafanyabiashara....akili zao ziko katika biashara na KUPATA FEDHA eti wakuhusudu wewe MRANGI ,MDIGO ,MUHA uliyehifadhi msahafu kwa kichwa na huna kitu wakupe BINTI YAO kwa kigezo hicho tu [emoji15][emoji15][emoji15][emoji15] labda zamani....sikatai..ziko familia chache ila wengi wakitaka KUZISIKIA HIZO SAUTI NZURI zikisoma QURAN(tajweed ,tartil na hukumu zake) wanawaita walimu wa madrassa wakitoa elfu 50...walimu hao wanakuja na vitoto vya madrassah na kuanza kusoma Quran tukufu ,ikifuatiwa na WASSILATU SHAFI ,Kitabu cha Maulid Barzanji ,wanapiga madufu na nari zake wakimaliza wanajipiga BIRIANI chuzi zitooo...nyumba ya mwarabu tena ,kitonga mseleleko....shughuli ikiisha wanawaaga mpaka siku nyingine...ustadh anakwenda kutamba kijiwe cha kahawa na Al Kasus....[emoji1787][emoji1787]
Ya nini mwarabu "afuge mkwe" wa kirangi ,kiha ,kisambaa ,kinyaturu ,kimeru kisa tu NI FUNDI WA KUSOMA QURAN?!!![emoji1787][emoji1787]
Dunia imebadilika....fedha fedha fedha si hao waarabu si wewe Mngoni.....[emoji1787]
#SiempreJMT[emoji7]
#MamaAnaupigaMwingi[emoji7]
#DP World ndio habari ya mjini [emoji7][emoji7]
Sent from my TECNO F1 using
JamiiForums mobile app