Ni kwanini DC Sabaya hajawajibishwa baada ya kubainika kuwa tuhuma alizotoa kwa wamiliki wa mabasi kuhujumu miundo mbinu ya reli ni za uongo?

Ni kwanini DC Sabaya hajawajibishwa baada ya kubainika kuwa tuhuma alizotoa kwa wamiliki wa mabasi kuhujumu miundo mbinu ya reli ni za uongo?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Siku chache zilizopita DC wa Hai, Ole Sabaya alijitokeza mbele ya vyombo vya habari akiwatuhumu wamiliki wa mabasi ya Limu Safaris na Machame Safaris kuwa wameunda magenge ya kiuhalifu ya uhalifu ya kuhujumu reli kati ya Moshi na Arusha na hivyo akawataka wamiliki wa mabasi hayo wajisalimishe kituo cha polisi cha Boma ng'ombe ili wajibu tuhuma zao

Wamiliki hao wa mabasi walitii amri hiyo ya DC Sabaya ya kuripoti kituo cha Boma ng'ombe kwa wakati alioagiza DC huyo Sabaya

Baada ya wamiliki hao wa mabasi kuripoti Polisi, RPC wa Kilimanjaro, Salum Hamdun, alijitokeza hadharani kueleza namna wamiliki hao waliivyoweza kutii amri bila shuruti na akaeleza pia namna Polisi hao waliivyofungua jalada la uchunguzi na namna uchunguzi wao ulivyoenda

RPC huyo akaeleza waziwazi kuwa baada ya uchunguzi wao, wamebaini kuwa hakuna hujuma yoyote iliyofanyika katika kipande hicho cha reli kati ya Moshi na Arusha kama aliivyodai DC Ole Sabaya

Ndipo hapo ninapojiuliza ni kwanini Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, hamfukuzi kazi DC Sabaya kwa kusababisha usumbufu mkubwa kwa wamiliki hao wa mabasi ambao imekuja kuonekana kuwa tuhuma ambazo walipewa na Mkuu huyo wa wilaya kuthibitidhwa kuwa ni za uwongo?

Vile vile hii si Mara ya kwanza kwa Mkuu huyo wa wilaya ya Hai kukumbwa na kashfa za aina hiyo za kuwasingiziia wafanyibiashara kuwa wanahujumu uchumi kwa kukwepa kulipa kodi na baadaye kuja bainika kuwa ni uwongo aliowazushia

Hivi tutaendelea kufanya kazi na wakuu wa wilaya wa "dizaini" ya huyo Mkuu wa wilaya ya Hai hadi lini?

Tafsiri tunayoipata wananchi ni kuwa kumbe baadhi ya wateule wa Rais wana "impunity" na hawawezi wajibishwa kwa makosa ya wazi kabisa wanayowafanyia wananchi kwa chuki tu kwa kutumia vyombo vyetu vya dola, kama vile Jeshi letu la Polisi kuhalalisha uharamia huo!
 
Mkuu hebu edit kidogo bandiko lako...

Ni kweli ulichokiandika....na hii inatupa picha kwamba awamu hii ni jinsi gani watu wengi wapo magereza kwasababu ya kusingiziwa na kutengenezewa mashtaka ya uongo na kuambiwa ni wahujumu uchumi
 
Mkuu hebu edit kidogo bandiko lako...

Ni kweli ulichokiandika....na hii inatupa picha kwamba awamu hii ni jinsi gani watu wengi wapo magereza kwasababu ya kusingiziwa na kutengenezewa mashtaka ya uongo na kuambiwa ni wahujumu uchumi
Tunao kina Kabendera ambao wamefunguliwa kesi za kubambika za kuhujumu uchumi, huku wakiendelea kusota mahabusu.........

Ambapo sasa ni zaidi ya miezi 6 kesi hiyo inaendelea tu kuahirishwa huku Polisi hao walioipeleka "chap chap" kesi hiyo mahakamani, wakidai kuwa uchunguzi wa kesi hiyo bado haujakamilika!

Hivi unawezaje kumpekeka mtuhumiwa "chap chap" mahakamani hapo wakati ukijua kuwa upelelezi bado haujakamilika?
 
kumbe wateule wa Rais wana "impunity" na hawawezi wajibishwa kwa makosa ya wazi kabisa wanayowafanyia wananchi kwa visa tu kwa kutumia vyombo vyetu vya dola, kama vile Jeshi letu la Polisi kuhalalisha uharamia huo!
Wateule wa rais, hawafanani, kuna ambao hata wakikoseshwa wanatumbuliwa na wengine hata wakosee vipi wataendelea.

P
 
Wateule wa rais, hawafanani, kuna ambao hata wakikoseshwa wanatumbuliwa na wengine hata wakosee vipi wataendelea.

P
Naunga mkono bandiko lako kwa asilimia 100 Mkuu Pascal Mayalla kwa ukweli ulioeleza
 
Yapo mengi mazuri DC Sabaya kafanya, ila baadhi hususani hili la karibuni kubambika watu na brand zao tuhuma nzito kuhujumu miundombinu reli na maamlaka uchunguzi kutoa taarifa hakuna hujuma, tutarajie kauli ya mkuu " Siwezi kuwa mnafiki kwa hili NASEMA HAPANA.." Kama DC hata jiuzulu hadi siku uapisho wa waziri mambo ya ndani na Zungu ,tunataraji kauli nzinto vinginevyo itakuwa mwendelezo wa UNAFIKI.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kusema uongo na kubambikia watu makosa kwa kichaka cha uzalendo, ni moja ya sifa kubwa kwa sasa ndani ya hii nchi. Hakuna hatua yoyote atachukuliwa maana huo ndio utamaduni wa sasa.
 
Mystery,
Huyo huyo kijana hata sifa za kuwa kiongozi hana lakini ndio chaguo la bwana mkubwa .
Mkuu Isakhamisi tunamwambia Jiwe kuwa wananchi ndiyo waliokupa madaraka hayo na wananchi hao hao ndiyo wanaosema kuwa DC Sabaya hafai kwenye nafasi hiyo ya u-,DC

Kwa hiyo kazi kwake Jiwe, kusuka au kunyoa
 
Kumbukeni mteule wa bodi ya VETA hapa majuzi alikuwa na tuhuma nzito za uhujumu na utakatishaji fedha lakini kesi iliondolewa mahakamani kwa amri ya DPP.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo hali inaleta visasi vikubwa sana nchini.......

Kwa kuwa inaleta picha kuwa kuna kikundi Fulani hapa nchini kina "impunity" wakati kundi jingine ndilo linaloonewa kwa kubambikiwa kesi na kusoteshwa rumande kwa kipindi cha muda mrefu
 
Siku chache zilizopita DC wa Hai, Ole Sabaya alijitokeza mbele ya vyombo vya habari akiwatuhumu wamiliki wa mabasi ya Limu Safaris na Machame Safaris kuwa wameunda magenge ya kiuhalifu ya uhalifu ya kuhujumu reli kati ya Moshi na Arusha na hivyo akawataka wamiliki wa mabasi hayo wajisalimishe kituo cha polisi cha Boma ng'ombe ili wajibu tuhuma zao

Wamiliki hao wa mabasi walitii amri hiyo ya DC Sabaya ya kuripoti kituo cha Boma ng'ombe kwa wakati alioagiza DC huyo Sabaya

Baada ya wamiliki hao wa mabasi kuripoti Polisi, RPC wa Kilimanjaro, Salum Hamdun, alijitokeza hadharani kueleza namna wamiliki hao waliivyoweza kutii amri bila shuruti na akaeleza pia namna Polisi hao waliivyofungua jalada la uchunguzi na namna uchunguzi wao ulivyoenda

RPC huyo akaeleza waziwazi kuwa baada ya uchunguzi wao, wamebaini kuwa hakuna hujuma yoyote iliyofanyika katika kipande hicho cha reli kati ya Moshi na Arusha kama aliivyodai DC Ole Sabaya

Ndipo hapo ninapojiuliza ni kwanini Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, hamfukuzi kazi DC Sabaya kwa kusababisha usumbufu mkubwa kwa wamiliki hao wa mabasi ambao imekuja kuonekana kuwa tuhuma ambazo walipewa na Mkuu huyo wa wilaya kuthibitidhwa kuwa ni za uwongo?

Vile vile hii si Mara ya kwanza kwa Mkuu huyo wa wilaya ya Hai kukumbwa na kashfa za aina hiyo za kuwasingiziia wafanyibiashara kuwa wanahujumu uchumi kwa kukwepa kulipa kodi na baadaye kuja bainika kuwa ni uwongo aliowazushia

Hivi tutaendelea kufanya kazi na wakuu wa wilaya wa "dizaini" ya huyo Mkuu wa wilaya ya Hai hadi lini?

Tafsiri tunayoipata wananchi ni kuwa kumbe wateule wa Rais wana "impunity" na hawawezi wajibishwa kwa makosa ya wazi kabisa wanayowafanyia wananchi kwa visa tu kwa kutumia vyombo vyetu vya dola, kama vile Jeshi letu la Polisi kuhalalisha uharamia huo!
"immunity"

Sabaya hawezi kuchukuliwa hatua kwa kua anayoyafanya ndiyo aliyotumwa kufanya na wakubwa wake , I mean anayoyafanya ndio mabosi wake wanataka afanye huko HAI .

Sent from my SM-J700H using Tapatalk
 
Back
Top Bottom