Ni kwanini K Lyn hakupata heshima anayostahili kwa mchango wake mkubwa kwenye Bongo Flava industry?

Ni kwanini K Lyn hakupata heshima anayostahili kwa mchango wake mkubwa kwenye Bongo Flava industry?

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
1725477123238.png

Mchango wake kwenye sanaa ya bongo sio wa kubeza lakini alichukuliwa poa.

Hakuwa msanii aliebahatisha kutoa Hit moja au mbili akapotea, Alihusika kwenye Hits 5, Ni wasanii wa kike wachache sana waliweza kutoa hits zaidi ya 3 (Ray C, Jide, Enika, n.k.), Sio rahisi !!

Zifuatazo ni hits zake 5 alizowahi kutu bless kwenye bongo fleva
  • Nikipata wangu
  • Crazy over you ft Squeezer
  • Nalia kwa furaha ft Bushoke
  • Nishike mkono ft Blue
  • Chochote utapata ft Noorah
kuimba alikuwa anajua, Alitoa hits ndani ya muda mchache, Alikuwa mrembo (Miss Tanzania), alikuwa mchangamfu, Shooting kali, Vionjo vya wasanii wa Marekani, n.k.

Kwa mtazamo wangu sina ushahidi lakini navyoona K Lyn alikuwa na pesa nje ya muziki, alikataa unyanyasaji na unyonyaji wa media kubwa, mapromota wanyonyaji nao walishindwa kumnasa hivyo ikapelekea kupewa airtime kidogo kinyume na ukubwa wa hits zake pamoja na kuwa shows chache ambazo hazikuendana na kiu ya mashabiki, Muziki aliufanya kama hobby ya kufurahisha mashabiki zake kuzidi maslahi.
 
Nachokumbuka nikiwa mdogo kuna nyimbo flan nlikua naskia tu inaimba
K Lynn baby wewee🎶
K lyn baby wewee🎶

Sijui nyimbo nyingine
 
Crazy over you ile nyimbo ikipigwa kama imetoka leo kuanzia audio mpaka video,shida yake hakufanya muziki kama kazi, alitegemea zaidi kudanga kwenye umiss huko ila kuimba alikuwa anajua
 
Nachokumbuka nikiwa mdogo kuna nyimbo flan nlikua naskia tu inaimba
K Lynn baby wewee🎶
K lyn baby wewee🎶

Sijui nyimbo nyingine
ndo hiyo yapili
 
Crazy over you ile nyimbo ikipigwa kama imetoka leo kuanzia audio mpaka video,shida yake hakufanya muziki kama kazi, alitegemea zaidi kudanga kwenye umiss huko ila kuimba alikuwa anajua
msimseme vibaya mtoto wa watu muacheni! hapa hatuzungumzii kudanga bali mziki wake.
 
Ray C, Lady Jay Dee, hao ni dada zake na wana hits nyingi zaidi

Lakini K Lyn naye alipaswa kupewa heshima yake, mchango wake sio mdogo
mchango gani sasa, hajadumu kwenye muziki muda mrefu akakimbilia kuolewa, sawa sawa na useme Vicky kamata ameleta mchango kwenye muziki, angekomaa angekuwa mbali
 
Mchango wake kwenye sanaa ya bongo sio wa kubeza lakini alichukuliwa poa.

Hakuwa msanii aliebahatisha kutoa Hit moja au mbili akapotea, Alihusika kwenye Hits 5, Ni wasanii wa kike wachache sana waliweza kutoa hits zaidi ya 3 (Ray C, Jide, Enika, n.k.), Sio rahisi !!

Zifuatazo ni hits zake 5 alizowahi kutu bless kwenye bongo fleva

  • Nikipata wangu
  • Crazy over you ft Squeezer
  • Nalia kwa furaha ft Bushoke
  • Nishike mkono ft Blue
  • Chochote utapata ft Noorah
Hizi ngoma zilipigika snaa enzi hizo
 
mchango gani sasa, hajadumu kwenye muziki muda mrefu akakimbilia kuolewa, sawa sawa na useme Vicky kamata ameleta mchango kwenye muziki, angekomaa angekuwa mbali
Nchango wake ni kuweza kutoa vibao vilivyoteka chati, mara 5 !!

Na hakukazia sana kama wasanii wengine, ni kwamba uwezo alikuwa nao alituonjesha kidogo alichonacho,

Tunaangalia quality sio quantity, kuna wasanii wapo kwenye game miaka mingi wametoa nyimbo kibao ila hazijaweza kutikisa chati
 
Back
Top Bottom