Ni kwanini kila migogoro ikitokea Dangote Cement lazima Obasanjo atue nchini?

Ni kwanini kila migogoro ikitokea Dangote Cement lazima Obasanjo atue nchini?

Ninakumbuka awamu ya nne kuna mama Mtanzania alisema yeye ni mke wa Mzee Obasanjo na alitapeliwa kiwanja wakati anataka kuwekeza Tanzania.

Lakini katika profile ya Obasanjo hakuna maelezo ya kuwa na mke Mtanzania. Inawezekana mama ni mpango wa kando.

Huyu mzee ni shemeji yetu.
Jaribu kuwa na fikra hata kidogo.
 
Kipindi cha Mzee Magufuli Dangote waliyumba na kusuasua sana kwenye biashara yao.. Nadhani sasa bei ya Cement itarudi kule ambako Dangote waliplan ifike.. Na hilo la makaa sina shaka lazima limezungumzwa.

Muda ni wakati mzuri sana Mkuu, ngoja tuone..
Afanye yote lakini ajue kwamba ata colombia na haiti kulikuwa na madini leo kuna mashimo tu na hao wanaoitwa wawekezaji hawapo tena.
 
Ninakumbuka awamu ya nne kuna mama Mtanzania alisema yeye ni mke wa Mzee Obasanjo na alitapeliwa kiwanja wakati anataka kuwekeza Tanzania.

Lakini katika profile ya Obasanjo hakuna maelezo ya kuwa na mke Mtanzania. Inawezekana mama ni mpango wa kando.

Huyu mzee ni shemeji yetu.
Punguza utundu.
 
Vijana wa JF walizani unamaanisha huyo Mama alikua Mama Samia,kumbe ni Mwanamke mwingine sema nae ni Mtanzania!!,kwa jinsi nilivyokuelewa Mimi!!
Ndio hivyo mkuu....wasijifungie kwenye boksi na tafsiri zisizo sahihi

Huyo mama ni mfanyabiashara tu
 
GAZPRON na bomba la mafuta huko Ujerumani kutoka Russia, Mwenyekiti wa Bomba ni Chancelor Mstaff Shoda.

Yaani viongozi wengi lazima wawe kwenye makampuni makubwa
Nakumbuka kina John Major na hata Gordon Brown ni wamoja wa wanufaika wa makampuni makubwa
Yaani jamaa wanakula hela taratibu
 
Hawa ni marafiki kwelikweli. Dangote alifadhili kampeni za Obasanjo. Ni wazi alipata mikataba minono ya serikali.
 
Na popote aingiapo Dangote, anapenda kuanzia nyumba kuu, kisha anakuwa na nguvu ya kiimla kwa mwenye nyumba baada ya kufanikisha ya mwenye nyumba.

Aliletwa na nani umesema? Amefanyaje hii wiki umesema?

Kazi iendelee
 
Kama aliiba na kuwekeza hapa hapa Afrika hio hela inasaidia waafrika wao ni umiliki na maaamuzi tu.
Khadaf i aliiba akaenda kuficha ufaransa kilichojiri mnakijua, kuna matrilioni ya dola yaliibwa na viongozi wa Afrika na kufichwa ulaya yanawasaidia wazungu.
 
Wasalaam Wakuu,

Hivi ni kwanini kila kunapotokea changamoto/ mgogoro kwenye kiwanda cha Dangote Cement Mtwara basi ndani ya siku chache tu lazima Rais Mstaafu wa Nigeria Obasanjo atue nchini na kuzungumza na Mkuu wa Nchi?

Ilitokea hili mara mbili wakati wa Rais Hayati Magufuli, na hivi majuzi badala ya mgogoro wa kiwanda na madereva nasikia leo hii Obasanjo ameonana na kufanya mazungumzo na Rais Mama Samia.

Kuna nini nyuma ya pazia Kati ya Dangote Group na Obasanjo?
Ukiwa na kampuni lazima uwe na Public Relation team itakayokusaidia kufanya lobbying kwa viongozi wa juu wa nchi wenye maamuzi ili kufanikisha malengo ya kampuni ndiyo maana Dangoti hapati shida kumwona Rais.
 
Wasalaam Wakuu,

Hivi ni kwanini kila kunapotokea changamoto/ mgogoro kwenye kiwanda cha Dangote Cement Mtwara basi ndani ya siku chache tu lazima Rais Mstaafu wa Nigeria Obasanjo atue nchini na kuzungumza na Mkuu wa Nchi?

Ilitokea hili mara mbili wakati wa Rais Hayati Magufuli, na hivi majuzi badala ya mgogoro wa kiwanda na madereva nasikia leo hii Obasanjo ameonana na kufanya mazungumzo na Rais Mama Samia.

Kuna nini nyuma ya pazia Kati ya Dangote Group na Obasanjo?
Uchumi ni siasa,Dangote ni home grown company ya Nigeria,imeitangaza nigeria duniani,Ili mambo ya Dangote yanyooke lazima uwatumie watu kama Obasanjo Rais mstaafu katika PR,na mahusiano ya nje na wakuu wa nchi nyingine,
Ebu fikiria Kikwete akipewa Kazi ya kuitafutia Wasafi media deal marekani,China,UK,kitendo Cha kumtimua mtu kama Raisi mstaafu katika mambo ya kibiashara Ili kufanikisha deals ni akili kubwa.
 
Ukiwa na kampuni lazima uwe na Public Relation team itakayokusaidia kufanya lobbying kwa viongozi wa juu wa nchi wenye maamuzi ili kufanikisha malengo ya kampuni ndiyo maana Dangoti hapati shida kumwona Rais.

Yaani kama kina Kikwete wangekuwa na shareholders tuseme kwa mfano sekta binafsi ya madini au biashara kubwa kama kina bakhressa
Hapo kuingiza biashara moja kwa moja kwenye soko la dunia bila mikwara ni kawaida sana

Tatizo viongozi wetu hawaoni hizo fursa ila wote wanaishia Kulima mihogo na kufuga ng’ombe tu
 
Mzee Obasanjo hanaga shuguli maalumu..anazurura tu. Hata wewe ukiwa na harusi unaweza kumualika
Nafasi aliyoshika inamfanya kuwa PR mzuri kutengeneza mahusiano na kampuni na nchi mbalimbali, ndiyo maana makampuni kama Pepsi.Nike au Adidas wanawatumia Messi au Ronaldo
 
Back
Top Bottom