Ni Kwanini Mdude Nyagali hakamatwi na hachukuliwi Hatua Kali Kwa Kuendelea Kumchafua Rais Samia Bila Ushahidi?

Ni Kwanini Mdude Nyagali hakamatwi na hachukuliwi Hatua Kali Kwa Kuendelea Kumchafua Rais Samia Bila Ushahidi?

Mkuu, Afrika huwa tunakosea sana kuamini kuwa Rais ana immunity ya maisha! Tukumbuke naye ni binadamu, anakosea kama tunavyokosea wengine! Anakwenda msalani kama sisi, na ana kila kitu cha ubinadamu kama wewe vile, idadi sawa ya vidole, meno, na mifupa. Tunapata wapi ujasiri na nguvu ya kumuona mtumishi wa umma kama mungu?! Samia sio Aphrodite wala Athena ni binadamu kama binadamu wengine.

Akikosea lazma aambiwe kwa sababu ni tabia na asili ya kila mwanadamu kukosea. Wengi wanafanya kumuogopa na kumtukuza ila bado atabakia kuwa mwanadamu tu. Kina Mobutu Sese Seko na fujo zake sasa hivi yupo wapi!? Joseph Stalin na ubabe wake wote sasa hivi yupo wapi!? Unataka kusema Samia huwa hafanyi makosa, hatukani watu, hana mawazo mabaya?! Je haombi toba na msamaha kwa Mola wake!? Kama tu wateule wa Mungu walikuwa wanamuomba Mungu tobacco na msamaha mara kibao sembuse Samia?! Acheni kujionesha kama mnajua Samia sio binadamu!

Mdude amekosea wapi!? Tatizo kila mtu anataka kuonekana ni kama mtume wa Samia! Ujinga wa kiwango cha lami kabsa. Kuna wahuni wanampatia heshima kubwa kuliko hata wazazi wao.​
 
Unaweza weka ushahidi wako wa kauli ,maneno,tuhuma na shutuma atoazo Mdude? Unaweza kumtuhumu mtu bila ushahidi? Mara ngapi mdude amekuwa akimtukana, kumdhalilisha,kumtweza ,kumchafua na kumvunjia heshima? Unaona ni sawa kwa afanyayo Mdude? Nasema tena kuwa hiyo haikubaliki na lazima ifike mwisho kwa mtu huyu kuwajibishwa ipasavyo.
Wewe ni hakimu wa mitandaoni?

SATIVA amemtaja Mafwele kama mmoja wa watesi wake na aliyetoa amri auawe. Mbona haujasema lolote kuhusu hilo?

Wewe unaashiria ni mmoja wa wanaoshangilia utekaji nyara na mauaji ya raia. Labda ni mmoja wa watekelezaji wa mpango huo.
 
Wewe ni hakimu wa mitandaoni?

SATIVA amemtaja Mafwele kama mmoja wa watesi wake na aliyetoa amri auawe. Mbona haujasema lolote kuhusu hilo?

Wewe unaashiria ni mmoja wa wanaoshangilia utekaji nyara na mauaji ya raia. Labda ni mmoja wa watekelezaji wa mpango huo.
Kumtaja tu mtu pasipo ushahidi haitoshi kumtia mtu hatiani.
 
Mkuu, Afrika huwa tunakosea sana kuamini kuwa Rais ana immunity ya maisha! Tukumbuke naye ni binadamu, anakosea kama tunavyokosea wengine! Anakwenda msalani kama sisi, na ana kila kitu cha ubinadamu kama wewe vile, idadi sawa ya vidole, meno, na mifupa. Tunapata wapi ujasiri na nguvu ya kumuona mtumishi wa umma kama mungu?! Samia sio Aphrodite wala Athena ni binadamu kama binadamu wengine.

Akikosea lazma aambiwe kwa sababu ni tabia na asili ya kila mwanadamu kukosea. Wengi wanafanya kumuogopa na kumtukuza ila bado atabakia kuwa mwanadamu tu. Kina Mobutu Sese Seko na fujo zake sasa hivi yupo wapi!? Joseph Stalin na ubabe wake wote sasa hivi yupo wapi!? Unataka kusema Samia huwa hafanyi makosa, hatukani watu, hana mawazo mabaya?! Je haombi toba na msamaha kwa Mola wake!? Kama tu wateule wa Mungu walikuwa wanamuomba Mungu tobacco na msamaha mara kibao sembuse Samia?! Acheni kujionesha kama mnajua Samia sio binadamu!

Mdude amekosea wapi!? Tatizo kila mtu anataka kuonekana ni kama mtume wa Samia! Ujinga wa kiwango cha lami kabsa. Kuna wahuni wanampatia heshima kubwa kuliko hata wazazi wao.​
Ushahidi wa tuhuma za za Mdude upo wapi? Au mtu ukijiamkia zako huko unaanza kuropoka ropoka Hovyo hovyo na kutuhumu watu bila ushahidi? Ndio democrasia hiyo? Ndio uhuru huo?
 
Unaweza weka ushahidi wako wa kauli ,maneno,tuhuma na shutuma atoazo Mdude? Unaweza kumtuhumu mtu bila ushahidi? Mara ngapi mdude amekuwa akimtukana, kumdhalilisha,kumtweza ,kumchafua na kumvunjia heshima? Unaona ni sawa kwa afanyayo Mdude? Nasema tena kuwa hiyo haikubaliki na lazima ifike mwisho kwa mtu huyu kuwajibishwa ipasavyo.
Jinsi damu itakavyozidi kumwagika hapa nchini mjue hata ninyi ha mtakuwa salama!
Hamkumbuki Nani alım piga risasi Karume na kwasababu gani? Samia ajue damu Hii inayomwagika haiendi bure itakuja kumlilia .
 
Jinsi damu itakavyozidi kumwagika hapa nchini mjue hata ninyi ha mtakuwa salama!
Hamkumbuki Nani alım piga risasi Karume na kwasababu gani? Samia ajue damu Hii inayomwagika haiendi bure itakuja kumlilia .
Acheni ujinga wa kuropoka ropoka vitu Ndivyo na ushahidi navyo .kwa lengo la kutafuta umaarufu na sifa tu za kijinga jinga tu
 
Ushahidi wa tuhuma za za Mdude upo wapi? Au mtu ukijiamkia zako huko unaanza kuropoka ropoka Hovyo hovyo na kutuhumu watu bila ushahidi? Ndio democrasia hiyo? Ndio uhuru huo?
Hoja kuu ilikuwa ni "Ni Kwanini Mdude Nyagali hakamatwi na Kuchukuliwi Hatua Kali Kwa Kuendelea Kumchafua Rais Samia Bila Ushahidi?"​

Naomba unisaidie kujibu hizi hoja mbili tu:
1. Mdude kuhoji kuhusu utendaji wa kazi wa Samia ni kosa!? Na kama ni kosa je kwaninj liwe kosa? Mdude amepata kuhoji udhaifu wa jeshi la polisi huku akionesha wazi namna ambayo maafisa polisi wakitumia chombo hicho kama familia zao ilihali wanalipwa na kodi zako! Je Mdude amekosea kuhoji jambo hili?!

2. Umezungumzia kuhusu uhuru na demokrasia, safi sana Mkuu, lakini unadhani Samia anatimiza kiapo chake cha kuheshimu na kulinda Katiba, katiba ambayo inatoa ruhusa ya kipekee ya kila raia kulindwa yeye na mali zake? Au Mdude amekosea kuzungumza jambo hilo!??​
 
Hoja kuu ilikuwa ni "Ni Kwanini Mdude Nyagali hakamatwi na Kuchukuliwi Hatua Kali Kwa Kuendelea Kumchafua Rais Samia Bila Ushahidi?"​

Naomba unisaidie kujibu hizi hoja mbili tu:
1. Mdude kuhoji kuhusu utendaji wa kazi wa Samia ni kosa!? Na kama ni kosa je kwaninj liwe kosa? Mdude amepata kuhoji udhaifu wa jeshi la polisi huku akionesha wazi namna ambayo maafisa polisi wakitumia chombo hicho kama familia zao ilihali wanalipwa na kodi zako! Je Mdude amekosea kuhoji jambo hili?!

2. Umezungumzia kuhusu uhuru na demokrasia, safi sana Mkuu, lakini unadhani Samia anatimiza kiapo chake cha kuheshimu na kulinda Katiba, katiba ambayo inatoa ruhusa ya kipekee ya kila raia kulindwa yeye na mali zake? Au Mdude amekosea kuzungumza jambo hilo!??​
Mbona umejibu na kuandika nje kabisa na hoja yangu? Nimeuliza kwanini Mdude hakamatwi kwa uzushi na kutoa tuhuma za uongo na uchonganishi pasipo ushahidi? Umeona tuhuma alizozitoa ? Au umekuja tu kutoa maoni yako bila kujuwa kinachoendelea?
 
Mbona umejibu na kuandika nje kabisa na hoja yangu? Nimeuliza kwanini Mdude hakamatwi kwa uzushi na kutoa tuhuma za uongo na uchonganishi pasipo ushahidi? Umeona tuhuma alizozitoa ? Au umekuja tu kutoa maoni yako bila kujuwa kinachoendelea?
Uzushi upi au tuhuma zipi za uongo ambazo Mdude amezitoa! Tuanzie hapo Mkuu!
 
Kumtaja tu mtu pasipo ushahidi haitoshi kumtia mtu hatiani.
Ushahidi unatolewa mahakamani.
Mtu yeyote anaweza kutuhumiwa na ana haki ya kujitetea dhidi ya tuhuma zake.

Wewe na wenzako humu si mlianzisha tuhuma dhidi ya Boni Yai, Mnyika na Mbowe kuhusiana na kifo cha mzee Kibao? Je ukiombwa ukatoe ushahidi mahakamani upo tayari kuthibitisha uhusika wao?
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ikiwa tutaacha Taifa likajenga utamaduni wa watu wakatumia mitandao ya kijamii kuchafua viongozi wetu,kuwapaka matope, kuwadhalilisha, kuwatukana matusi bila kuchukuliwa hatua wala kukamatwa ili watoe ushahidi tutakuwa tunariharibu Taifa letu.tutakuwa tunaharibu maadili na utamaduni mzima wa kuheshimiana na kukosoana kwa staha.

Imeshakuwa kero sana kwetu wananchi kuona mara nyingi sana Mdude Nyagali akitumia mitandao ya kijamii kumtolea RAIS wetu lugha za matusi, kumdhalilisha ,pamoja na kumhusisha ,kumzushia tuhuma za uongo, uchonganishi na zenye lengo la kumchafua pasipo ushahidi wa aina yoyote ile.

Amekuwa akifanya hivyo mara nyingi sana.na kitendo cha kukaliwa kimya pasipo kuchukuliwa hatua za kukamatwa,kuhojiwa,kufikishwa mahakamani kumemfanya ajione yupo juu ya sheria,kujiona anaogopwa ,kujiona yeye anaweza kufanya lolote,kusema chochote, kumtukana yeyote, kumdhalilisha yeyote,kumvunjia heshima yeyote,kumzushia yeyote pasipo kuchukuliwa hatua wala kukamatwa wala kuhojiwa wala kukemewa.

Imefanya watu wabaki wanashangaa inakuwaje mtu huyu anayefanya kazi ya kumchafua Mheshimiwa Rais kila siku anaachwa bila kuchukuliwa hatua? Watu wanashangaa kwanini anafumbiwa macho muda wote? Wahusika mnasubiri mtu huyu aropoke au aseme nini au amchafue vipi na kwa kiasi gani Rais wetu ndipo mumchukulie Hatua? Je sheria zinatumika kwa baadhi ya watu na kufungwa pingu kwa wengine kutokutumika?

Kwanini hamumkamati na kumhoji ili atoe ushahidi wa tuhuma anazozitoa? Yeye ni nani katika Taifa hili? Hii haikubaliki wala kuvumilika kuona akimchafua Rais wetu Pasipo kuchukuliwa hatua kali za kisheria. ni lazima tufahamu ya kuwa hakuna uhuru usio na mipaka,hakuna uhuru au demokrasia kwa ajili ya kutukana , kudhalilisha,kuwashushia heshima wengine pamoja na kuwapaka matope wengine. Uhuru una kwenda sambamba na wajibu wa kuzingatia haki za watu wengine .

Huwezi ukawa unachafua watu wengine halafu ukasema ni demokrasia au uhuru.uhuru na demokrasia ina mipaka yake. Nawakumbusheni ya kuwa Mbali ya kuwa RAIS Samia ni Mama mwenye watoto, wajukuu lakini kubwa ni kuwa Ni Rais wetu ,ni kiongozi wetu tunaye muangalia na anayegusa Maisha yetu moja kwa moja. Kwa hiyo hatufurahishwi wala kupendezwa kuona Rais wetu akichafuliwa na mtu au kuzushiwa mambo yasiyo na ushahidi wa aina yoyote ile.hii haikubaliki hata kidogo.

Ni lazima tabia hii mbaya na chafu inayofanywa na watu aina ya Mdude Nyagali waliokosa adabu na staha tuipinge,kuikemea ,kuishambulia na kuikataa kabisa hapa Nchini.ni lazima tuseme tunataka uhuru na demokrasia lakini siyo uhuru wa kuwatusi na kuwachafua wengine bila ushahidi wa aina yoyote ile.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Nenda KAMKAMATE!!
 
Muite huyu mwenyekiti wako sindie amejipa hiyo kazi
Six5b0TZWlBbGx71.jpg
 
Ndugu zangu Watanzania,

Ikiwa tutaacha Taifa likajenga utamaduni wa watu wakatumia mitandao ya kijamii kuchafua viongozi wetu,kuwapaka matope, kuwadhalilisha, kuwatukana matusi bila kuchukuliwa hatua wala kukamatwa ili watoe ushahidi tutakuwa tunariharibu Taifa letu.tutakuwa tunaharibu maadili na utamaduni mzima wa kuheshimiana na kukosoana kwa staha.

Imeshakuwa kero sana kwetu wananchi kuona mara nyingi sana Mdude Nyagali akitumia mitandao ya kijamii kumtolea RAIS wetu lugha za matusi, kumdhalilisha ,pamoja na kumhusisha ,kumzushia tuhuma za uongo, uchonganishi na zenye lengo la kumchafua pasipo ushahidi wa aina yoyote ile.

Amekuwa akifanya hivyo mara nyingi sana.na kitendo cha kukaliwa kimya pasipo kuchukuliwa hatua za kukamatwa,kuhojiwa,kufikishwa mahakamani kumemfanya ajione yupo juu ya sheria,kujiona anaogopwa ,kujiona yeye anaweza kufanya lolote,kusema chochote, kumtukana yeyote, kumdhalilisha yeyote,kumvunjia heshima yeyote,kumzushia yeyote pasipo kuchukuliwa hatua wala kukamatwa wala kuhojiwa wala kukemewa.

Imefanya watu wabaki wanashangaa inakuwaje mtu huyu anayefanya kazi ya kumchafua Mheshimiwa Rais kila siku anaachwa bila kuchukuliwa hatua? Watu wanashangaa kwanini anafumbiwa macho muda wote? Wahusika mnasubiri mtu huyu aropoke au aseme nini au amchafue vipi na kwa kiasi gani Rais wetu ndipo mumchukulie Hatua? Je sheria zinatumika kwa baadhi ya watu na kufungwa pingu kwa wengine kutokutumika?

Kwanini hamumkamati na kumhoji ili atoe ushahidi wa tuhuma anazozitoa? Yeye ni nani katika Taifa hili? Hii haikubaliki wala kuvumilika kuona akimchafua Rais wetu Pasipo kuchukuliwa hatua kali za kisheria. ni lazima tufahamu ya kuwa hakuna uhuru usio na mipaka,hakuna uhuru au demokrasia kwa ajili ya kutukana , kudhalilisha,kuwashushia heshima wengine pamoja na kuwapaka matope wengine. Uhuru una kwenda sambamba na wajibu wa kuzingatia haki za watu wengine .

Huwezi ukawa unachafua watu wengine halafu ukasema ni demokrasia au uhuru.uhuru na demokrasia ina mipaka yake. Nawakumbusheni ya kuwa Mbali ya kuwa RAIS Samia ni Mama mwenye watoto, wajukuu lakini kubwa ni kuwa Ni Rais wetu ,ni kiongozi wetu tunaye muangalia na anayegusa Maisha yetu moja kwa moja. Kwa hiyo hatufurahishwi wala kupendezwa kuona Rais wetu akichafuliwa na mtu au kuzushiwa mambo yasiyo na ushahidi wa aina yoyote ile.hii haikubaliki hata kidogo.

Ni lazima tabia hii mbaya na chafu inayofanywa na watu aina ya Mdude Nyagali waliokosa adabu na staha tuipinge,kuikemea ,kuishambulia na kuikataa kabisa hapa Nchini.ni lazima tuseme tunataka uhuru na demokrasia lakini siyo uhuru wa kuwatusi na kuwachafua wengine bila ushahidi wa aina yoyote ile.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kawaulize MAKABURU na NDULI kilichowapata.......vivaa na MOZAMBIKIESINS
 
Ushahidi unatolewa mahakamani.
Mtu yeyote anaweza kutuhumiwa na ana haki ya kujitetea dhidi ya tuhuma zake.

Wewe na wenzako humu si mlianzisha tuhuma dhidi ya Boni Yai, Mnyika na Mbowe kuhusiana na kifo cha mzee Kibao? Je ukiombwa ukatoe ushahidi mahakamani upo tayari kuthibitisha uhusika wao?
Umepiga kwenye mshono
 
Back
Top Bottom